Kashfa mpya Nishati na Madini; Kikwete na Pinda wajiuzulu au wawajibishwe!

Lakini mimi nina tatizo moja tu ya kwamba Mhando ni sehemu tu yan matatizo yote. Utamwondoa Mghando na kumweka mtumwingine ambaye atakuta utaratibu ni ule ule. Nimesema wazi hata mimi leo ukinambia nishike nafasi hiyo Tanesco nitavuta na kuwapa ndugu na jamaa zangu tender kwa sababu tatizo zima ni la kimfumo sio nani anaweza kutokuwa na tamaa..

Huu mpango wa kukata matawi wakati unajua kabisa mti mzima umeoza ndio naupinga miye.. Viongozi wangapi wameshakuja Tanesco toka Mwinti aondoke au IPTL kuinga mkataba.. Tumebadilisha viongozi wee hadi tunaishiwa watu kwa sababu hatutaki kukubali ama ku face the real problem..

Mfumo mzima wa mikataba na utawala ni mibovu kwa nchi yote. Hapa kilichobakia ni kata mti panda mti - ndio tutaweza pata miti safi.. Kupurura matawi ya mti ulooza unauwezesha mti kukua kustawi tena japo umeoza!..Hivi mnafikiria Ufisadi kufikia stage hii iloyopo leo ni bahati mbaya?..

Kinachotakiwa ni kuwa na reform ambayo inaweza kuisaidia nchi iondokane na mikataba feki yasiyo na tija yeyote. Mfano mzuri ni Ghana walipopata uongozi mpya Prof Atta Mills (Mwenyezi Mungu amlaze mahali pema peponi) alirekebisha mikataba mingi ya kinyonyaji. Ikiwepo ya bonus kubwa ya rais mstaafu.
 
.....

Inadaiwa kuwa kulikuwa na wabunge waliopangwa kimkakati kushawishi wenzao wasiisulubu serikali kwa kukwamisha Bajeti ya Nishati na Madini leo.

Miongoni mwa wabunge wanaotajwa ni Waziri Mkuu Pinda, William Lukuvi, Jenista Mhagama na Mbunge wa Muleba Kaskazini, Charles Mwijage. Inadaiwa kuwa Mwijage ana maslahi katika Puma Energy iliyopewa zabuni ya kuiuzia mafuta IPTL na Maswi.

Mbunge wa Simanjiro Christopher Ole Sendeka, anadaiwa kutaka iundwe kamati teule ya Bunge kuchunguza uozo ulio ndani ya wizara na TANESCO.

Baadhi ya wabunge wakasema wazo lake ni sawa, lakini katika mazingira ya sasa ya kisiasa ya CCM, tume itaibua uchafu mwingi ambao utaimaliza serikali mbele ya umma.

Sendeka alisema: "Mbona katika sakata la Richmond iliundwa kamati iweje hivi sasa isiundwe wakati kosa la Maswi linafanana na la Lowassa?"

Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango, inasemekana alijenga hoja kuwa CCM na serikali walifanya makosa kwenye sakata la Richmond ambalo lilimfanya aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa, kuachia ngazi.

"Tulimtosa Lowassa, baadaye ukweli umejulikana, na sasa makosa yetu yanaigharimu serikali na CCM. Tusirudie makosa yale yale, tuwaache hawa kwa maslahi ya CCM," alisema.
 
"Tanzania Daima, ilidokezwa kuwa wajumbe wote walikubaliana kwamba Katibu Mkuu wa Nishati na Madini alifanya makosa na alivunja sheria.

Wabunge wa CCM walitaka Maswi na Muhongo watoswe ili kujenga heshima ya serikali na kusimika utawala wa sheria.
"


Fikiri, yaani udokezwe wajumbe wote wakubali mkosaji mmoja halafu ghafla waamue na kumsulubu Waziri ambaye hawajaona hana kosa na tena baadaye wawepo wengine waliopangwa kuwatetea, sijui wanatoka wapi wakati mwazoni unasema wote??

Kama timu nzima ya upinzani - NCCR Mageuzi ilivyosema; ni kweli bomba la ulaji la watu limekatwa sasa lazima watu watoe mapovu sana. Uchafu wa mtu mwovu ni adhabu yake mwenyewe huyo MD na hata Bodi nzima ya TANESCO inapaswa kufumuliwa!
 
Salary slip

Nashukuru kwa maoni yako huria.Lakini mi binafsi naona wewe unashabikia uozo mtupu.

Suala ni kwanini serikali iendelee kununua mafuta kwa bei ya juu wakati kunauwezekano wa kununua kwa bei ya chini, Hoja ya kuwawajibisha hawa haipo. Kila siku watu wanavunja sheria, sheria ikivunjwa kwa manufaa ya uma sawa...ila ikivunjwa kwa manufaa ya mafisadi hapo si sawa. Hongera Maswi,pambambana na mafisadi.
 
Last edited by a moderator:
hapa haijulikani nani mkweli! wizara wanavuta upande wao TANESCO inavuta upande wao! then nini mwisho wa hili sakata??
 
Ninashawishika sana kukubali ya kwamba jk na pinda nao wanavuta mpunga kwenye hizi deal..haiwezekani kabisa mamvo yawe hivi
 
Hii ndio mimi sikubaliani nayo ya kusema this is what we have right now.. Unataka tuwaeleze madudu ya nani ktk wizara ya nishati na Madini? au mnataka tuanzie wapi ili mfahamu kwamba Mhando ni product ya kile tulichokipanda.. Unapurura mti ulokwisha oza zamani kwa sababu wamesema hizo mil 800 kwa mkewe - changa la macho, wakati wao wanaiba mabillioni kila siku tunavyoongea hapa.

Je unajua ya kwamba Tanesco miaka yote matumizi yao huzidi Mapato! miaka yote wanafanya kazi ya kanisa kwa sababu wanalipia hadi miradi ya mawaziri na viongozi wetu. Unamkumbuka yule katibu mkuu Patrick Rutabanzibwa aloachishwa baada ya kumwaga radhi ktk zengwe la IPTL ilikuwa vipi na yumo ktk list of shame?..Nadhani mwaka jana alikuwa katiba mkuu wizara ya ardhi kama sikosei nilimuona Kigamboni ktk sakata la mji mpya..
Je, tuliwafikisha mahakamani kujua ukweli uko wapi..The guy will die being mistaken for Fisadi kwa sababu tu tuliamua
kumtundika yeye..

Mkuu unakataa kila attempt to change.........can you please propose a plot for change???? With priorities in order
 
Huku madini kuna mambo!, hebu angalieni hii nimeipata mahali na kuiposti kule jamii inteligence!.

After studying the experience from other countries, the following lessons were learnt:

  • Location of LNG Plant – should be constructed on land (not floating LNG
on sea)

  • Reasons: Mainly for monitoring and control purposes – monitoring is challenging because of lack of technology and control means

  • There should be only one plant.
  • The GoT/Tanzanians/Public should have majority shares to the entire
Infrastructure say not less than 51% – to have authority say and decision
making for the benefit of the country. It may be on PPP model.

  • The proposed land for construction of LNG and other industries utilizing natural gas should be owned by the government. Facilities like roads, water and electricity should be put by GOT and appropriate tariff should be determined for the government.


  1. KWA GESI ALIYOTUJALIA MWENYEZI MUNGU, TUKIJIPANGA VIZURI, TUTAPATA MAENDELEO MAKUBWA KULIKO AMA KAMA SOUTH AFRICA.
  2. MAKAMPUNI MAKUBWA YA UTAFUTAJI WA MAFUTA NA GESI YANAELEWA NA YANATAKA TUBAKI KWENYE HALI YA KUTOELEWA HALI YA BIASHARA YA GESI. YANATULAGHAI KWA NJIA YA UZOEFU NA WALIONAO.
  3. GAS HATA KAMA IKO CHINI YA BAHARI AU CHINI YA ARIDHI NI MALI YETU NA INAYO VALUE YAKE NA SIO MWENYE UWEZO WA KUITOA ARIDHINI BASI NDIE MWENYE GAS DARWIN THIORY ISITUMIKE KWA MALIASILI YA NCHI YETU.
 
hapa inawezekana makundi yote haya mawili ni ya mafisadi kwani katibu bw.maswi kama issue ya kutaka kununua mafuta kwa bei ya kuokoa fedha nyingi namna hiyo angeipeleka kwenye bodi moja kwa moja ni nani angempinga ??

Na kama huko ingeshindikana anageweza hata kwenda kumuona rais ambaye anayo mamlaka dhidi ya wahusika? lakini naye akaamua kuacha njia zote hizo akaenda moja kwa moja PUMA huenda hao Puma wameshamkatia kile kipande kidogo ambacho wangekula ma middle man.

Yaani hawa wote mwisho wa siku wanaweza kuwa ni mafisadi waliozidiana kete na jawabu hapa ni kuunda tume huru.
 
Actually hao IPTL, Symbion na mashirika mengine - what are their expenses for real..kuwa na generator 100mw au 45 tu basi unapewa, kiwanja, supply ya mafuta au gas bure kisha unawauzia tena Tanesco umeme kwa kutumia gharama za Tanesco!.. I mean something is very wrong here!.

Mkuu Mkandara, something is real wrong!, leo nimeipata hii ya gesi asilia, kumbe ile gesi yote ni ya wawekezaji, wakishaichimba, wanatuuzia kwa bei ya soko, eti sisi tiutafaidika na kodi!. Wanamaani kitendo tuu cha kuwekeza kwenye mitambo yao kuichimba ile gesi, sasa gesi ndio imekuwa mali yao!, sisi tunauziwa!. Tanzanite ni yao, dhahabu ni ya hawa wachimbaji!, hata na gesi asili pia kumbe sio yetu?!.

Niliposikia tumevumbua gesi asili, nilidhani kitu chenye thamani, ni hiyo gesi asili, nakajua wawekezaji wanakuja kuichimba ili taifa letulifaidike!. Kumbe gesi yetu hapo ilipo thamani yake ni zero!, mwekezaji anayeichimba ndiye mwenye gesi na sisi tunauziwa!.

Tungekubali wawekezaji kutoka China, wangetukopesha mitambo na kuichimba gesi ikiwa yetu, mitambo yetu, sisi tungelipa deni tuu la mitambo na uwekezaji, ila gesi ingekuwa yetu na mitambo ya kuchimbia ni yetu na viwanda ni vyetu, tukiuza faida ni yetu!. Kumbe tumewapa maeneo ya kuchimba, ardhi tumewapa, mitambo ni yao, viwanda ni vyao, gesi ni yao, watatuuzia sisi kwa bei ya soko eti faida yetu itakuwa kuyitumia gesi na serikali kupata kodi!.

Tena wajimbaji wakubwa wako off shore, nani anaweza kujua gesi kiasi gani inachimbwa?, huko ni juu kwa juu!. Wakati nikitumika balozi fulani, niliona pilika pili kubwa za kusaka maeneo Mtwara, ndege zinakodiwa kwa dola elfu 20 per day na watu wanalipa ma trip na matrip like nothing!, kumbe gesi bure!.
 
Huku madini kuna mambo!, hebu angalieni hii nimeipata mahali na kuiposti kule jamii inteligence!.

After studying the experience from other countries, the following lessons were learnt:

  • Location of LNG Plant – should be constructed on land (not floating LNG
on sea)

  • Reasons: Mainly for monitoring and control purposes – monitoring is challenging because of lack of technology and control means

  • There should be only one plant.
  • The GoT/Tanzanians/Public should have majority shares to the entire
Infrastructure say not less than 51% – to have authority say and decision
making for the benefit of the country. It may be on PPP model.

  • The proposed land for construction of LNG and other industries utilizing natural gas should be owned by the government. Facilities like roads, water and electricity should be put by GOT and appropriate tariff should be determined for the government.


  1. KWA GESI ALIYOTUJALIA MWENYEZI MUNGU, TUKIJIPANGA VIZURI, TUTAPATA MAENDELEO MAKUBWA KULIKO AMA KAMA SOUTH AFRICA.
  2. MAKAMPUNI MAKUBWA YA UTAFUTAJI WA MAFUTA NA GESI YANAELEWA NA YANATAKA TUBAKI KWENYE HALI YA KUTOELEWA HALI YA BIASHARA YA GESI. YANATULAGHAI KWA NJIA YA UZOEFU NA WALIONAO.
  3. GAS HATA KAMA IKO CHINI YA BAHARI AU CHINI YA ARIDHI NI MALI YETU NA INAYO VALUE YAKE NA SIO MWENYE UWEZO WA KUITOA ARIDHINI BASI NDIE MWENYE GAS DARWIN THIORY ISITUMIKE KWA MALIASILI YA NCHI YETU.

pasco nchi hii haiwezi kuendelea mpaka pale tutakapoamua kuwa serious na swala la ufisadi bila hivyo hakuna maendeleo kwani adui mkubwa wa maendeleo ni ufisadi nenda nigeria uangalie maeneo kampuni za shell na chevron zinaponyonya mafuta uone shule na hospitali za maeneo hayo unaweza hata kulia machozi watoto wanakaa chini kwenye mavumbi blackboard imeningizwa kwenye mti na mwalim mwenyewe ukimuangalia anaweza kuwa ajalipwa mshahara miezi 6.
tanzania as long as tumekubali tuwaachie watu wachache jk na marafiki zake watafune nchi kwa niaba yetu hatutoona maendeleo kamwe mpaka pale tutapoamka tukasema enough is enough.
 
Mkandara, ukiangalia hii issue ya TANASECO kwa sasa utaona kuna uwezekano mtando wa Dowans umekeweza sana kwenye hili shirika na huyu bwana mdogo Mhando alikuwa ni dalali wao mzuri. Kuondoka kwake kunatoa mwanya wa kufumua mambo na sasa ndio sakarasi zinaanza ili kutisha watu na kama itabidi kuondoka na shingo ya katibu mkuu basi wako tayari kufanya hivyo.

Nitataka kuona wabunge (regardless ni chama gani) watakao mtetea huyu Mhando na hapa itatoa picha 'uwekezaji' TANESCO ni mpana kiasi gani.

Katibu mkuu anaweza akawa amekiuka sheria za manunuzi, lakini aliruka kwa manufaa ya mapana zaidi maana alisitisha utaratibu uliokuwepo wa kununua mafuta kupita kwa middleman na badala yake amemua mafuta yanunuliwe moja kwa moja toka kwa supplier (PUMA). Upindishaji wa sheria wa namna hii mimi naukubali kabisa. Tusibiri bunge bado linaendelea.
Absolutely.... tatizo maslahi ya watu yameguswa. Wengine pia tunao humu...kama sheria haina manufaa sioni sababu ya kuwa watumwa wa sheria zinazozidi kuteketeza rasilimali zetu. Let us be objective....
 
Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi bwana James Mbatia ameanisha ufisadi mkubwa Tanesco katika kununua mafuta ya kuzalisha umeme wa IPTL ikiambatana na kupeana tenda za 10%

Akitoa mfano wa tenda ya mafuta mazito amabapo BP waliotoa tenda ya shilingi 1460 kwa lita wakati tenda waiopewa na Tanesco watanunua 1900 kwa lita ikiwa ongezeko la zaidi ya sh. 400/= ya mtu hiyo
 
Suala hili watanzania tunahitaji kuliangalia kwa makini bila ushabiki usio kuwa na msingi na wenye malengo ya kuhamasisha maslahi binafsi.

Siyo tu suala ya kujiuzulu mtu, wengi wamejiuzuluna hatujaona kama kuna mabadiliko kutokana na kujiuzulu kwao. Mimi nadhani tatizo liko kwetu umma kwa ujumla, wataalam na tamaa za makapuni yetu kuwanyonya watanzania na kujipatia faida bila hata mitaji ndicho kinauma wengi katika hili.

Nakubaliana kabisa na Mh. Mbatia kuwa sina imani na kamati ya Nishati ya Madini, kwa jinsi wanavyolichukua hili suala utaona kabisa si kwa maslahi ya waliowengi, bali ni watu ambao wameahidiwa kitu kama ilivyozoeleka, ugomvi wote huu ni kwamba kuna watu wamekosa maslahi fulani katika mchakato huu.

Imeelezwa kabisa sheria ya manunuzi kanuni ya 42 ina mruhusu Katibu Mkuu kuamua vinginevyo juu ya manunuzi pale itakapoonekana uamuzi huo unafanywa kwa maslahi ya umma. Kipengele hiki kiliwekwa kwa lengo la kuwabana watu wenye taamaa na kufikiria faida bila kujali maslahi ya umma. Ni nani asiyejua leo ukiitisha tender hata ya kununua kalamu za kawaida zinauzwa rejareja madukani kwa 500 utauziwa kwa bei ya tender kwa 1500? je hizi ndizo sheria tunazotetea? ningewaelewa wanaolilia uongozi wa nishati na madini kuvuliwa madaraka kama wangelilia sheria ya manunuzi iangaliwe upya ili kulinda maslahi ya taifa.

Imeelezwa kabisa kamba kampuni zilizoomba hiyo tender zingepata, tungenunua mafuta hayo hayo kwa bei ya 1800 kwa lita badala ya 1460 iliyotolewa na Puma. Kununua mafuata kutoka Puma kunaokoa Tsh. Bill.3 kila baada ya wiki mbili, halafu mbunge anaenda kukaa na kuongea tu kuwa maamuzi hayajafanyika kwa maslahi ya taifa na yamevunja sheria. Napata mashaka juu ya uelewa wao juu ya maana ya maneno maslahi ya taifa, inaonekana wao kugawana hizo bilioni 3 kila mwezi ndiyo maslahi ya taifa lao la njozi?

No way kama ndiyo soko huria hilo sasa Tanzania tunaelekea kujizika wenyewe, vipo vitu vya kushabikia na vipo ambavyo tunatakiwa kuwa makini na kuuweka ushabiki pembeni kabisa.Na pale unapoona ujanjauja wako wa kibiashara na kujipatia fedha kwa njia za mkato umebainika usijidhalilishe kwa kuendelea kupiga kelele na kulobby, bila kujali kuwa unawaibia watanzania.

Katibu Mkuu Maswi amefanya kitendo cha kizalendo na anastahili kutetewa katika hili na kama angekuwa fisadi kama ambavyo mafisadi wanataka kutuaminisha asingefanya haya ambayo amefanya kwa maslahi ya taifa na siyo kwa maslahi ya wachache wakiwemo wanakamati ya madini ya nishati.

Wabunge wengi sasa wamepata mtaji kwa njia ya kutaka kulazimisha kuundwa kwa kamati za kuchunguza, hii ni mbinu ambayo inaendeleza matumizi mabaya ya fedha, nashauri maamuzi yafanyike hizi kamati zinapoundwa zisilipwe fedha kama utasikia kuundwa kwa hizo kamati.

Watanzania tufanye kazi, tutumie akili tulizopewa na mwenyezi Mungu kujiletea maendelea kwa kadri ulivyojaliwa na siyo kuendeleza hoja za kujinufaisha kwa njia za mkato.

Yapo makosa yanayofanywa na Wizara au Serikali ambayo ni kinyume na maslahi ya taifa/umma lakini siyo hili. Ni vigumu kuamini katika hali ya kawaida kwamba mtu anayeokoa 3 bill. kwa kila wiki mbili leo anaambiwa ni fisadi na hafai na yule anayelia usiku kucha kuwanyonya watanzania ndiye anayetetewa kuwa apewe hizo bill tatu kila wiki mbili. Kwa maana nyingine apewe mtaji na faida vyote viwe vyake. Tumeelezwa Kampuni hizo zinanunua mafuta kutoka Puma na kuiuzia Serikali kwa Bei ya Juu bado tunalzimisha sheria imepindishwa, jamani.

Mungu saidia Tanzania na hawa wanaotaka kutetea huu wizi washindwe kwa nguvu za Jina lako Mola. Amina.
 
Kwa utaratibu huu wa kutibu matatizo kwa kuziba viraka autatusaidia kila siku tutaishia kwenye sintofahamu :wacko:
 
hapa haijulikani nani mkweli! wizara wanavuta upande wao TANESCO inavuta upande wao! then nini mwisho wa hili sakata??
Ni kweli hii kitu inachanganya sana, kila upande unakuja na shutuma na maelezo ambayo ukiyasoma unaanza kuwa convinced. Lakini the next day inakuja nyengine inakuchanganya zaidi. Well, ngoja tuone mwisho wake ni nini hasa.
MY TAKE:Kitu kimoja kinajirudia mara kwa mara ni kwamba kuna ufisadi ume/unafanyika.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom