Lady Whistledown
JF-Expert Member
- Aug 2, 2021
- 1,021
- 1,609
BUNGENI: Mbunge Hawa Mwaifunga amesema Wizara ya Ardhi imekopa Zaidi ya Tsh. Bilioni 345, bila Kamati kuwa na Taarifa ya Mkopo huo na kuhoji Matumizi na vipaumbele vya Wizara.
Mkopo huo umeidhinishwa kwa matumizi ya Upimaji wa Vijiji 250 kwa Miaka 5 kati ya zaidi ya Vijiji 9,000 vinavyopaswa kupimwa, wakati Tume ya Upangaji wa Ardhi waliomba Tsh. Bilioni 10 kupima Vijiji 600 kwa Mwaka.
Miongoni mwa Matumizi ya Mkopo huo, Bilioni 5 zimetengwa kwa ajili ya Semina, Uratibu zaidi ya Bilioni 40, uboreshaji wa Ofisi za Wizara, Ujenzi wa Ofisi ya Kila Mkoa na Matengenezo ya Magari ya Wizara.
Mkopo huo umeidhinishwa kwa matumizi ya Upimaji wa Vijiji 250 kwa Miaka 5 kati ya zaidi ya Vijiji 9,000 vinavyopaswa kupimwa, wakati Tume ya Upangaji wa Ardhi waliomba Tsh. Bilioni 10 kupima Vijiji 600 kwa Mwaka.
Miongoni mwa Matumizi ya Mkopo huo, Bilioni 5 zimetengwa kwa ajili ya Semina, Uratibu zaidi ya Bilioni 40, uboreshaji wa Ofisi za Wizara, Ujenzi wa Ofisi ya Kila Mkoa na Matengenezo ya Magari ya Wizara.