KASHFA BoT: Tume, tume , tume mpaka lini!?

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,792
287,994
Hakuna haja ya tume nyingine tena itumie mabilioni for doing nothing! Tunachotaka ni kuona wahusika wote wanatiwa ndani haraka sana na kufikishwa mahakamani kujibu hatia dhidi ya ufisadi na wahusika wote wafilisiwe mali zao. Tumechoka na tume zisizokuwa na manufaa yoyote!

Posted Date::1/22/2008
Tume ya kufuatilia ufisadi BoT yaanza kazi
Na Tausi Mbowe
Mwananchi

TIMU iliyoteuliwa kufuatilia taarifa ya ukaguzi katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kuhusu upotevu wa fedha za akaunti ya Malipo ya Kigeni (EPA) imeanza kazi yake rasmi kwa kukusanya maoni kutoka kwa wananchi.

Tume hiyo iliyoteuliwa na Rais Jakaya Kikwete kufutia kampuni ya Ernest & Young kubaini kuwa kulikuwa na upotevu wa zaidi ya Sh133 bilioni katika mazingira ya kutatanisha ndani ya benki hiyo na hatimaye Rais Kikwete kutengua wadhifa wa aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu, Daud Ballali.

Taarifa ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambaye ni Mwenyekiti wa Timu hiyo, Johnson Mwanyika ilisema tayari timu hiyo imeshaanza kazi yake na wamekuwa wakipata ushirikiano mkubwa wa wananchi.

Timu hiyo imesema kuwa itakuwa makini kwa nia ya kuhakisha kuwa ukweli unajulikana na kuweka wazi hadharani ili kulinda heshima ya Taifa kwa kila chembe ya habari itakayopatikana itafuatiliwa kwa makini. Kwa mujibu wa Mwanyika nia ya timu ni kufanya kazi yake kwa uhakika na kuwaomba wananchi kuwa na subira na kutoa kila ushirikiano utakaoiwezesha timu hiyo kukamilisha majukumu yake.
 
Hakuna haja ya tume nyingine tena itumie mabilioni for doing nothing! Tunachotaka ni kuona wahusika wote wanatiwa ndani haraka sana na kufikishwa mahakamani kujibu hatia dhidi ya ufisadi na wahusika wote wafilisiwe mali zao. Tumechoka na tume zisizokuwa na manufaa yoyote!

Posted Date::1/22/2008
Tume ya kufuatilia ufisadi BoT yaanza kazi
Na Tausi Mbowe
Mwananchi

TIMU iliyoteuliwa kufuatilia taarifa ya ukaguzi katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kuhusu upotevu wa fedha za akaunti ya Malipo ya Kigeni (EPA) imeanza kazi yake rasmi kwa kukusanya maoni kutoka kwa wananchi.

Tume hiyo iliyoteuliwa na Rais Jakaya Kikwete kufutia kampuni ya Ernest & Young kubaini kuwa kulikuwa na upotevu wa zaidi ya Sh133 bilioni katika mazingira ya kutatanisha ndani ya benki hiyo na hatimaye Rais Kikwete kutengua wadhifa wa aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu, Daud Ballali.

Taarifa ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambaye ni Mwenyekiti wa Timu hiyo, Johnson Mwanyika ilisema tayari timu hiyo imeshaanza kazi yake na wamekuwa wakipata ushirikiano mkubwa wa wananchi.

Timu hiyo imesema kuwa itakuwa makini kwa nia ya kuhakisha kuwa ukweli unajulikana na kuweka wazi hadharani ili kulinda heshima ya Taifa kwa kila chembe ya habari itakayopatikana itafuatiliwa kwa makini. Kwa mujibu wa Mwanyika nia ya timu ni kufanya kazi yake kwa uhakika na kuwaomba wananchi kuwa na subira na kutoa kila ushirikiano utakaoiwezesha timu hiyo kukamilisha majukumu yake.

Watanzania tumeliwa.

By the time Kikwete anaondoka madarakani (au kuondolewa), vipande vya nchi ambavyo vitakuwa havijauzwa kwa Sinclair na Barrick vitakuwa vimebakia mashimo na makorongo na mabilionea mia moja tu na familia zao.
 
Haki ya nani! Bongo ni nchi ya werevu! Tulishafungwa bao la kisigino kinachoendelea hapa ni mchezo wa kuigiza.
 
Jamani ndo ajira zenyewe hizi. Tume inapoundwa baada ya nyingine ni ulaji kwa wengine pia. Ajira milioni moja si mchezo, ni muhimu kuanza kidogo kidogo.
 
Unajua vitu vingine ni vinatengenezwa bila mantiki. report imeonyesha ni nani aliyekula fedha za BOT,kilichokuwa kinafuata ni kuwatia nguvuni wote waliotajwa na report hiyo. Unaunda tume hili kutafuta ukweli wa nani kahusika wakati report imeshakuambia Mkono na kampuni yake wamekamata mshiko wa BOT visivyohalali,ukweli gani tunaoutaka katika hili au ni mchezo wa delying techinique dakika zisogee,game lisahaulike vichwani mwa watu. Hizi tume ni aina ya ulaji nyingine kama si ufisadi type 2
 
msiniambie wameunda tume nyingine tena ya kuchunguza mafisadi wa BOT...siamini!
 
Baada ya blah blah zote hizi inabidi tuelezwe kama hizo b133 zimerudi kwenye hazina yetu otherwise naona maluweluwe. Kutumia gharama kuuubwa kwa tume, halafu gharama nyingine kushtaki/kufunga watu wawili au watatu bila kurudisha fedha zetu ni mchezo usiolezeka.
 
Vigogo wa Usalama Wachunguza Ripoti ya BOT.

UCHAMBUZI wa taarifa ya ukaguzi wa Benki Kuu Tanzania (BoT) kuhusu upotevu wa fedha za Akaunti ya Malipo ya Kigeni (EPA) umeanza.

Taarifa iliyotolewa jana na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ilisema wananchi wengi wamejitokeza kutoa taarifa zinazoendelea kuisadia timu iliyoundwa kufanya kazi hiyo.

Ili kuhakikisha kuwa kazi hiyo inafanyika kwa uhakika na kikamilifu zaidi, timu hiyo iliyoteuliwa na Rais Jakaya Kikwete kufanya kazi hiyo imetoa namba za simu za wajumbe wake, ili kuwarahisishia wananchi kuendelea kutoa taarifa.

Wajumbe na namba zilizotolewa kwenye mabano ni Inspekta Jenerali wa Polisi, Bw. Said Mwema (0754 785557) na Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Bw. Robert Manumba(0754 206326).

Wengine ni Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Dkt. Edward Hosea (0754 763741) na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Bibi Lilian Mashaka (0754 336116).

Taarifa hiyo iliwahakikishia wananchi wote, kwamba taarifa watakazotoa zitakuwa msaada mkubwa kwa timu na taarifa ya Mkaguzi na Mdhibiti wa Mahesabu ya Serikali ambayo inafanyiwa kazi.

"Kila mwananchi atakayetoa taarifa, atapata hifadhi ya faragha kwa mujibu wa sheria," ilisema taarifa hiyo ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambaye ni MWenyekiti wa Timu hiyo.

Source; Majira.
 
Mi kinachonishangaza, ripoti kutoka kwa rais ilisomwa tarehe 09-01-08. Tume inatangaza kuanza kazi tarehe 22-01-2008.Tume hii yenye watu 3(IGP,Attorney General na PCCB) ina chukua siku 13, kuanza kazi?Huu ni muda mrefu mno kwa tuhuma nzito kama hizi.Kama agizo la rais linachukua siku 13 kuanza kutekelezwa, jee maagizo mengine ya watu wenye madaraka madogo zaid yanachukua siku ngapi kutekelezwa. Je hii ndio kasi mpya, nguvu mpya na ari mpya ya utendaji wa kazi? Au ndo ilikuwa mbinu ya kuwawezesha watuhumiwa waondoe mali zao?
Halafu tume after tume, hizi tuhuma ni nzito na zinatosha kuwafikisha watu hawa mahakamani.Kwani ushahidi wote si upo BOT sasa wananchi wakatoe ushahidi gani tena? Ernest & Young walichukua ushahidi kwa wananchi?
Kuna mtu alisema humu we jaribu tu kutuhumiwa na jirani yako kuwa umechimba mihogo yake, uone jamba jamba ya polisi,ila hawa aah, wanangoja ushahidi wa wananchi.

Mimi naamini kitu kimoja kuwa 'THERE IS HONOR AMONG THIEVES'GEOFREY ARCHER.
 
Terms of Reference za Tume nini? Report ya jinsi pesa zilivyoibwa? Kwani hiyo repoti ya CAG haitoshi?

Wadanyanyika bwana tunapenda kuchezea raslimali na mda!

Huu ulaji tu mwingine.. tungependa kujua pesa iliyotengwa ktk hii tume mpya ni Shilingi bilioni ngapi?
 
Tume inasema inapata ushirikiano toka kwa wananchi . What do they know about the scam huko BOT ? Au ni mimi nimesoma sijaelewa ? Tume inaenda tena kwa Wananchi wapi ambao wana habari za wizi wa BOT .Kama Serikali iliktaa kuwako wizi hadi wakapewa facts na JF na Upinzani leo hao wananchi wanaweza kweli kuwa na lolote wajualo ? JK ama kweli una usanii ndiyo maana nasema acheni kumsakama Ballali hapa mmenasa .
 
Huko nyuma nilisema tatizo la watanzania ni kuridhika kwa vitu vidogo saana!!JK alipotangaza hatua ya kumfukuza Balali watu walipiga makofi.Lakini tunashindwa kuelewa kuwa niya yake sio kuwachukulia hatua wabadhilifu walianikwa wazi katika ripoti,bali ni jinsi gani afanye ili chati yake ipande kwa kutumia hili saga.

Hakuna watu wenye viburi,jeuri na dharau kama hawa viongozi wetu wa serikali toka CCM.Watanzania tunajifanya watu wa Amani kumbe tumejawa na upumbavu tu.
 
Hivi ile Ripoti BOT tume "Kamati ya Bunge" hiko wapi ? Kwa nini inakuwa ni sahihi kutumia hela za walipa kodi kufinance kazi za hizi tume lakini hawataki kuwapatia feed back . This is totally ridiculous...
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom