Karatasi nakamata,kueleza yalosibu
Nna kipande cha kashata,nlichonunua Bububu
Kashata yenye utata,utamuwe wasulubu
Nimeziona kashata,ya bububu ni pekee
Kitaka kula najing'ata,kwa utamu so kifani
Nikimung'unya nadata,Sijui sababu gani
Tamu zaidi ya bata,Alopakwa Asumini
Nimemung'unya kashata,ya bububu ni pekee
Sikuinunua kwa shaka,nlipoiona bububu
Ulimi ulinitoka,nilitamani kutubu
Nilijiona kishoka,rudi bara nliona tabu
Nimezing'ata kashata,ya bububu ni pekee
Utamuwe wa milele,nnapoilamba ni tabu
Chachu kama uwele,hata sijui sababu
Ina sukari kichele,ni dawa tena tabibu
Nimeshaonja kashata,ya bububu ni pekee
Kashata yangu naficha,simpi mtu yeyote
Naila usiku kucha,wala sendi kokote
Utamu lojificha,tamanisha siku zote
Nimeziona kashata,ya bububu ya pekee
Amani
Malenga wa jamii
Nna kipande cha kashata,nlichonunua Bububu
Kashata yenye utata,utamuwe wasulubu
Nimeziona kashata,ya bububu ni pekee
Kitaka kula najing'ata,kwa utamu so kifani
Nikimung'unya nadata,Sijui sababu gani
Tamu zaidi ya bata,Alopakwa Asumini
Nimemung'unya kashata,ya bububu ni pekee
Sikuinunua kwa shaka,nlipoiona bububu
Ulimi ulinitoka,nilitamani kutubu
Nilijiona kishoka,rudi bara nliona tabu
Nimezing'ata kashata,ya bububu ni pekee
Utamuwe wa milele,nnapoilamba ni tabu
Chachu kama uwele,hata sijui sababu
Ina sukari kichele,ni dawa tena tabibu
Nimeshaonja kashata,ya bububu ni pekee
Kashata yangu naficha,simpi mtu yeyote
Naila usiku kucha,wala sendi kokote
Utamu lojificha,tamanisha siku zote
Nimeziona kashata,ya bububu ya pekee
Amani
Malenga wa jamii