Karume apata kashifa nzito Z`bar

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,314
33,108
KarumeTulip(5).jpg

Rais mstaafu wa Zanzibar, Amani Abeid Karume


Rais mstaafu wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, amekumbwa na kashfa akidaiwa kutoa amri ya kukodishwa kwa majengo ya Mambo Msiige bila kufuata utaratibu na sheria.

Tume iliyoundwa na Baraza la Wawakilishi Zanzibar kuchunguza pamoja na mambo mengine, ukodishaji wa ardhi na majengo ya Serikali, imebaini Mambo Msiige ilikodishwa kwa miaka 99 thamani ya dola za Marekani milioni 1.5 kinyume cha sheria

Kwa mujibu wa Ripoti ya Uchunguzi wa kamati hiyo iliyoongozwa na Mwakilishi wa Chakechake, Omar Ali Shehe, majengo hayo yalikodishwa kwa Kampuni ya ASB Holdings Limited kupitia taratibu ambazo hazikuzingatia maslahi ya Taifa.

Ripoti ya kamati hiyo inaonyesha kuwa ukodishwaji huo ulifanyika baada ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Ikulu) Dk Mwinyihaji Makame Mwadini, kupewa agizo na Rais Karume (mstaafu) kwa maandishi.

“Dk Mwinyihaji aliiambia kamati kuwa yeye ndiye aliyepokea agizo kwa wino mwekundu kutoka kwa Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Amani Abeid Karume kuwa Serikali imepata mwekezaji kampuni ya ASB Holdings Ltd, “sehemu ya ripoti hiyo ilikariri maelezo ya Waziri Mwadini alipohojiwa na kamati hiyo.

Kwa mujibu ripoti hiyo, Dk Mwadini aliiambia kamati kuwa Rais aliagiza kampuni hiyo ikodishwe kwa mkataba wa malipo ya Dola milioni 1.5 na kulipa kiasi cha Dola 10,000 kwa mwaka.
Kwa agizo hilo, Dk Mwadini alimwandikia barua Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na uchumi Zanzibar akimwarifu kupokea fedha kutoka kwa mwekezaji huyo ili aweze kujenga hoteli ya nyota tano na kwamba baada ya kupokea malipo hayo afungue akaunti maalum ya kutunza fedha hizo.

Hata hivyo, kwa mujibu wa ripoti hiyo, Dk Mwadini alipotakiwa kutoa mbele ya kamati ushahidi wa agizo la rais alikataa na kusema kutoa dokezo la rais ambalo limeandikwa kwa wino mwekundu siyo sawa.
“Mpaka wakati huu tunawasilisha ripoti hii agizo la maandishi kutoka kwa rais halikutolewa na Dk Mwadini mbele ya kamati ya uchunguzi.” Kwa mujibu wa ripoti hiyo yenye kurasa 224.

Hata hivyo, ripoti hiyo imesema kwamba pamoja Kamati hiyo kumtaka Katibu wa Baraza kumwandikia Barua ya Desemba 8, mwaka 2011 ya kumtaka kuwasilisha ushahidi wa agizo la Rais mstaafu ameshindwa na kuendelea kutetea msimamo wake kuwa ni “Siri ya serikali.”

Kamati hiyo ya uchunguzi imebaini kuwa nyaraka za mpango wa ukodishwaji majengo na ufukwe wa Shangani zimepotea Wizara ya Ardhi, makazi, Maji, na nishati katika mazingira ya kutatanisha.
“ Katika mafaili ya Ofisi hakuna hata barua ya maombi ya ukodishwaji yaliyofanywa na mwekezaji mwenyewe, kwa ufupi hata faili lenye kumbukumbu za “Lease’ ya majengo ya Mambo Msiige na Starehe Club halipo.” Imeeleza Ripoti hiyo.



CHANZO: NIPASHE JUMAPILI

 
  1. Je Karume ana uhusiano wo wote hata wa kimazingira na kampuni ya ASB?
  2. Je fedha hizo USD 1.5 million zililipwa?
  3. Je kwa nini ziwe na akaunti maalum?
  4. Je hilo pango la USD 10,000/= kwa mwaka linaendelea kulipwa au la kwa kuwa nyaraka zimepotea?
 
Wazenji wanataka muungano ufe kila kukicha. Tutakapowavurumsha huku baada ya hiyo ki2 kufa rasmi ndo watajua ardhi maana yake nini.
 
Back
Top Bottom