Karibuni ADC kwa wote waliochoshwa na ufisadi wa CCM na CCM 'B' na ubabe wa CHADEMA

Tatizo sio rangi Christina na mwenzio tatizo ni ubunifu hakuna mmecopy kila kitu bado sera tu

Sehemu ya Katiba yetu inasemaje haya yafuatayo:

1. Ukomo WA Uongozi: Vipindi viwili vya miaka mi5 mi5 kwa uongozi WA Kitaifa.
2. Kiongozi kutangaza Mali zake ndani ya KIPINDI cha MIEZI MITATU mara baada ya kuchaguliwa.

3. Kufukuzana: Kutakua na CHOMBO cha Kutatua migogoro ya chama nje ya chama kitakachokuwa CHINI ya Uongozi WA Mwanasheria AMA jopo la wanasheria ili kukwepa personal interest ie: makundi hivyo suala la kutimuana kiholela halitokuwepo katika chama Chetu.
4. KATIBA pia itatambua Uwepo WA MwenyeziMungu, Itasaidia kupata viongozi waadilifu, wachamungu hivyo kupunguza matendo yote maovu ie: Ufisadi, Wizi WA Mali za Umma, Udikteka etc.
5. Walemavu wasipungue asilimia TANO (5%) katika ngazi zote za Uongozi. Hii ni kutokana na ukweli kwamba kuna zaidi ya walemavu millioni NNE (4mil.) NCHINI Tanzania.
6. Asilimia hamsini ya wanawake katika ngazi zote za Uongozi.

Vp kuna eneo tumewaingilia mpaka hapo? Tazama kwenye blue utajua tumejipanga kwa KIASI gani. Punguza kuropoka pia.

KARIBUNI ADC - DIRA ya mabadiliko.
 
Hapo kwny 4. Mtaanzisha dhehebu au dini?Maana wanachama wa vyama vyote vya siasa wana imani zao na hakuna katiba isiyotambua uwepo wa Mungu maana watekelezaji wake wanamuabudu Mungu
 
Ndugu zangu wa CUF ni watu safi ni mfano mzuri waliwaita jamaa wakataka kusulihisha hawakueleweka,Chadema pia kwa kina David,ninachoshangaa ni wewe kutotambua hivyo vyombo,tatizo ni UBUNIFU
 
Mna walemavu wangapi?

Sikiliza Kipimbwe, Hatujaanzisha chama ili kujua idadi ya walemavu wanaotuunga MKONO, Tumeanzisha chama cha ADC tumkomboe Mtanzania. Atakayevutiwa na sera zetu anakaribishwa kujiunga bila kujali jinsia AMA uzima, ulemavu wake.....Jambo la Msingi ni kwamba lazima awe na akili zake timamu na awe Mtanzania baaaasi, Si Zaidi ya hapo.
Tumetazama maeneo ambayo yana mapungufu hasa katika vyama vinginevyo vya kisiasa kikiwemo CCM na tukayafanyia kazi.
Vyama vingi vya Siasa NCHINI vinaendeshwa Kama kikundi flani cha watu AMA kidikteta zaidi kuliko kidemokrasia, Mfano hai ni kwa chama cha wananchi CUF ambapo tangu mwaka 1995,2000,2005,2010 na sasa tunaelekea 2015 general election wagombea ni hao hao na viongozi wakuu ni hao hao Sultani na Profesa wake.
Katika kuonyesha Usultani AMA Udikteta wao ni pale MHE. HAMAD Rashid Mohamed alipotangaza nia ya kugombea Ukatibu Mkuu WA Chama ambapo walipitisha maazimio ya kumshughulikia na mwishowe tukaona yaliyotokea. Wakamfukuza.
Tumeliona hili na ndio tukapitisha maazimio ya Ukomo WA Madaraka baada ya vipindi viwili vya miaka mi5 mi5.
 
Natafuta chama kitakachokuwa na sera ya UPANDAJI MITI ISIYO HARIBIFU/UTUNZAJI WA MAZINGIRA
 
Natafuta chama kitakachokuwa na sera ya UPANDAJI MITI ISIYO HARIBIFU/UTUNZAJI WA MAZINGIRA

ADC ni chama chenye sera ya upandaji wa miti kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi, sera ambayo imo ndani ya katiba ya chama na itafanyiwa kazi katika matawi ya ADC nchi nzima.
Karibu ADC.
 
Sehemu ya Katiba yetu inasemaje haya yafuatayo:

1. Ukomo WA Uongozi: Vipindi viwili vya miaka mi5 mi5 kwa uongozi WA Kitaifa.
2. Kiongozi kutangaza Mali zake ndani ya KIPINDI cha MIEZI MITATU mara baada ya kuchaguliwa.

3. Kufukuzana: Kutakua na CHOMBO cha Kutatua migogoro ya chama nje ya chama kitakachokuwa CHINI ya Uongozi WA Mwanasheria AMA jopo la wanasheria ili kukwepa personal interest ie: makundi hivyo suala la kutimuana kiholela halitokuwepo katika chama Chetu.
4. KATIBA pia itatambua Uwepo WA MwenyeziMungu, Itasaidia kupata viongozi waadilifu, wachamungu hivyo kupunguza matendo yote maovu ie: Ufisadi, Wizi WA Mali za Umma, Udikteka etc.
5. Walemavu wasipungue asilimia TANO (5%) katika ngazi zote za Uongozi. Hii ni kutokana na ukweli kwamba kuna zaidi ya walemavu millioni NNE (4mil.) NCHINI Tanzania.
6. Asilimia hamsini ya wanawake katika ngazi zote za Uongozi.

Vp kuna eneo tumewaingilia mpaka hapo? Tazama kwenye blue utajua tumejipanga kwa KIASI gani. Punguza kuropoka pia.

KARIBUNI ADC - DIRA ya mabadiliko.
Mkuu wangu hili swala la kuwa na walemavu asilimia 4 na wanakwake asilimia 50 mnatumia vigezo gani maana Equal opportunity haina maana hiyo isipokuwa affirmative action..Binafsi yangu kinachotakiwa ni kuwapa nafasi sawa wanawake na walemavu kugombani nafasi za uongozi na isitokee mtu kubaguliwa kwa sababu hizo..

nadhani mnachanganya sana maana ya kuweka uuwiano pale ambapo kundi moja lilibaguliwa. Zamani ktk nchi za magharibi ilikuwa sheria kutowaruhusuwanawake na walemavu kushiriki ktk ujenzi wa Taifa na walinyimwa nafasi hata za kugombea. Hivyo ndio ikawekwa haki yao na nguvu kubwa ikatumika kuhamasisha wanawake na walemavu kushiriki..Sio kuwapa zawadi kama kwamba wao ni walemavu kweli hivyo wanatakiwa kusaidiwa kuingia ktk uongozi..

Binafis yangu nadhani haya ni matusi kwa kmakundi haya lakini kwa sababu ni misheni town (mbinu za kuishi mjini) yawezekana kuna maana na ukweli kutoana!.
 
Back
Top Bottom