UtuExchange
Member
- Oct 15, 2008
- 12
- 0
Karibu UtuExchange
Napenda kukukaribisha UtuEchange.
UtuExchange: Trading on the future!
UtuExchange ni mchezo ambao washiriki mnashindana katika kubashiri matukio ya baadaye. Jinsi ambavyo unabashiri sawasawa ndivyo jinsi unavyoshinda zaidi.
UtuExchange inaendeshwa kwa mfumo wa masoko ya mitaji. Madai ya matukio ya baadaye ni kama makampuni ambayo washiriki wanaweza kuwekeza kwa kununua hisa za matukio hayo.
Mfano wa Dai:
Ndio, kufungiwa kwa MwanaHALISI kutatanguliwa
Will the ban on MwanaHALISI be reversed?
Kama umenunua hisa za dai hilo na MwanaHALISI likafunguliwa kabla ya kifungo chake kuisha, unatengeneza faida, na lisipofunguliwa unakuwa umepata hasara.
Changamoto ni kukusanya faida nyingi zaidi kuliko wengine kwa kubashiri matukio kwa usahihi zaidi kuliko wengine.
Nnapata wapi fedha za kununulia?
Kwenye UtuExchange U ndio fedha yetu. Siyo fedha rasmi ya nchi yako.
Unapojiunga tu unapewa kama 2,000U kama mtaji wako. Unaweza ukatumia mtaji huu kununulia hisa kwenye matukio yajayo.
Na wakati ambapo faida ulizotengeneza hazifikii 25,000U, utakuwa unaongezewa mtaji kidogo kidogo ili uweze kujikwamua. Asiyenacho anaongezewa ... UtuExchange tunapenda haki ...
Thamani ya Hisa
Thamani ya hisa katika dai lolote ni kati ya 0U na 100U. Kabla matokeo ya dai hayajajulikana, thamani ya hisa inategemea na walionazo wakotayari kuuza kiasi gani, na wanaotaka kununua wako tayari kununua kwa kiasi gani. Utafanikiwa kununua hisa kama kuna mtu yuko tayari kuuza katika bei unayotaka. Na utafanikiwa kuuza hisa kama kuna mtu yupo tayari kununua hisa katika bei unayotaka.
Lakini baada ya matokeo ya dai kujulikana, thamin ya hisa ni kama hivi:
-Tukio la dai hilo likitokea, thamani ya hisa katika dai hilo inapanda kufikia 100U.
-Tukio lisipotokea, thamani ya hisa inashuka mpaka 0U.
Hisa zinatolewa vipi kwa mara ya kwanza?
Hisa za mdai mapya zinatolewa kwa mara ya kwanza kwa mnada (IPO).
Katika mnada huu, kila mshiriki anasema anataka hisa ngapi na yupo tayari kulipa kiasi gani kwa kila hisa. Huwezi kuona madau ya wengine kwenye mnada huu.
Baada ya mnada kufungwa, nusu ya washiriki watauziwa hisa. Na hawa ni wale walio weka madau ya juu zaidi. Lakini bei watakayouziwa ni bei ya yule aliyeweka bei ya chini kabisa.
Kwa mfano: kama kuna washiriki wanne waliweka madau ya 70U, 60U, 50U na 40U, hisa zitauzwa kwa aliyeweka 70U na 60U, lakini wote watauziwa kwa bei ya 60U.
Ninanunuaje/Ninauzaje hisa?
Baada ya IPO, na baada ya hisa kugawiwa, hisa zaweza kununuliwa na kuuzwa.
Mtindo wa kuuza na kununua hisa unafanana na unaotumika katika masoko ya mitaji.
Kununua hisa, unaweka oda yako ya kununua na kusema namba ya hisa unazotaka , na bei unayotaka kununulia. Kama kuna mtu ambaye yupo tayari kuuza katika bei hiyo, biashara itafanyika na utapata hisa na yeye atapat U zake. Kama hayupo, basi oda yako itasubiri mpaka atakapotokea mtu aliye tayari kuuza katika bei hiyo. Au mpaka utakapo amua kuifuta hiyo oda.
Vivyo hivyo, kuuza hisa, unaweka oda yako ya kuuza. Na oda yako itasubiri mtu aliyetayari kununua katika bei hiyo.
Ninatengenezaje faida?
Unatengeneza faida kwa kununua kwa bei ndogo na kuuza kwa bei ya juu zaidi.
Kuna jinsi mbili.
1. Unaweza kununua hisa na kusubiri mpaka dai litakapofungwa ili likitokea upate 100U. Kama ulinunua hisa kwa 60U, utatengeneza faida ya 40U.
2. Unaweza kununua hisa kwa bei ndogo pale unapodhani bei yake baadaye itaenda juu watu watakapogundua kwamba uwezekano wa tukio hilo kutokea umeongezeka. Bei itakapoenda juu, unaziuza na kutengeneza faida.
Mbona madai yanakuja "dabodabo"?
Kila dai linakuwa na dai lingine moja au zaidi yanayokinzana.
Kwa mfano: kwa swala la MwanaHALISI kuna dai linalosema: "Ndio, kufungiwa kwa MwanaHALISI kutatanguliwa". Lakini pia kuna dai kinzani linalosema "Hapana, kufungiwa kwa MwanaHALISI hakutatanguliwa".
Hii inamruhusu mtu asiyeamini kwenye dai la kwanza kuwekeza kwenye dai linigine ambalo yeye anadhani lina tija zaidi.
Na ni ruksa kufanya biashara kwenye madai yote mawili.
Tuzo
Ukishatengeneza U nyingi, unaweza kuzitumia kujinyakulia zawadi.
Zawadi zitakuwa zinwekwa kwenye orodha ya zawadi mara kwa mara. Na zitakuwa zinatolewa kwa mnada. Anayeweka dau la juu, ndiye anajichukulia. Kwa hiyo jinsi unavyobashiri kwa usahihi zaidi, ndio jinsi unakuwa na U nyingi, na ndivyo unavyojiweka katika nafasi nzuri ya kujinyakulia zawadi.
Na sasa ...
Karibu UtuExchange sasa, na utuonyeshe busara yako katika kubashiri yajayo!
UtuExchange: Trading on the future!
Napenda kukukaribisha UtuEchange.
UtuExchange: Trading on the future!
UtuExchange ni mchezo ambao washiriki mnashindana katika kubashiri matukio ya baadaye. Jinsi ambavyo unabashiri sawasawa ndivyo jinsi unavyoshinda zaidi.
UtuExchange inaendeshwa kwa mfumo wa masoko ya mitaji. Madai ya matukio ya baadaye ni kama makampuni ambayo washiriki wanaweza kuwekeza kwa kununua hisa za matukio hayo.
Mfano wa Dai:
Ndio, kufungiwa kwa MwanaHALISI kutatanguliwa
Will the ban on MwanaHALISI be reversed?
Kama umenunua hisa za dai hilo na MwanaHALISI likafunguliwa kabla ya kifungo chake kuisha, unatengeneza faida, na lisipofunguliwa unakuwa umepata hasara.
Changamoto ni kukusanya faida nyingi zaidi kuliko wengine kwa kubashiri matukio kwa usahihi zaidi kuliko wengine.
Nnapata wapi fedha za kununulia?
Kwenye UtuExchange U ndio fedha yetu. Siyo fedha rasmi ya nchi yako.
Unapojiunga tu unapewa kama 2,000U kama mtaji wako. Unaweza ukatumia mtaji huu kununulia hisa kwenye matukio yajayo.
Na wakati ambapo faida ulizotengeneza hazifikii 25,000U, utakuwa unaongezewa mtaji kidogo kidogo ili uweze kujikwamua. Asiyenacho anaongezewa ... UtuExchange tunapenda haki ...
Thamani ya Hisa
Thamani ya hisa katika dai lolote ni kati ya 0U na 100U. Kabla matokeo ya dai hayajajulikana, thamani ya hisa inategemea na walionazo wakotayari kuuza kiasi gani, na wanaotaka kununua wako tayari kununua kwa kiasi gani. Utafanikiwa kununua hisa kama kuna mtu yuko tayari kuuza katika bei unayotaka. Na utafanikiwa kuuza hisa kama kuna mtu yupo tayari kununua hisa katika bei unayotaka.
Lakini baada ya matokeo ya dai kujulikana, thamin ya hisa ni kama hivi:
-Tukio la dai hilo likitokea, thamani ya hisa katika dai hilo inapanda kufikia 100U.
-Tukio lisipotokea, thamani ya hisa inashuka mpaka 0U.
Hisa zinatolewa vipi kwa mara ya kwanza?
Hisa za mdai mapya zinatolewa kwa mara ya kwanza kwa mnada (IPO).
Katika mnada huu, kila mshiriki anasema anataka hisa ngapi na yupo tayari kulipa kiasi gani kwa kila hisa. Huwezi kuona madau ya wengine kwenye mnada huu.
Baada ya mnada kufungwa, nusu ya washiriki watauziwa hisa. Na hawa ni wale walio weka madau ya juu zaidi. Lakini bei watakayouziwa ni bei ya yule aliyeweka bei ya chini kabisa.
Kwa mfano: kama kuna washiriki wanne waliweka madau ya 70U, 60U, 50U na 40U, hisa zitauzwa kwa aliyeweka 70U na 60U, lakini wote watauziwa kwa bei ya 60U.
Ninanunuaje/Ninauzaje hisa?
Baada ya IPO, na baada ya hisa kugawiwa, hisa zaweza kununuliwa na kuuzwa.
Mtindo wa kuuza na kununua hisa unafanana na unaotumika katika masoko ya mitaji.
Kununua hisa, unaweka oda yako ya kununua na kusema namba ya hisa unazotaka , na bei unayotaka kununulia. Kama kuna mtu ambaye yupo tayari kuuza katika bei hiyo, biashara itafanyika na utapata hisa na yeye atapat U zake. Kama hayupo, basi oda yako itasubiri mpaka atakapotokea mtu aliye tayari kuuza katika bei hiyo. Au mpaka utakapo amua kuifuta hiyo oda.
Vivyo hivyo, kuuza hisa, unaweka oda yako ya kuuza. Na oda yako itasubiri mtu aliyetayari kununua katika bei hiyo.
Ninatengenezaje faida?
Unatengeneza faida kwa kununua kwa bei ndogo na kuuza kwa bei ya juu zaidi.
Kuna jinsi mbili.
1. Unaweza kununua hisa na kusubiri mpaka dai litakapofungwa ili likitokea upate 100U. Kama ulinunua hisa kwa 60U, utatengeneza faida ya 40U.
2. Unaweza kununua hisa kwa bei ndogo pale unapodhani bei yake baadaye itaenda juu watu watakapogundua kwamba uwezekano wa tukio hilo kutokea umeongezeka. Bei itakapoenda juu, unaziuza na kutengeneza faida.
Mbona madai yanakuja "dabodabo"?
Kila dai linakuwa na dai lingine moja au zaidi yanayokinzana.
Kwa mfano: kwa swala la MwanaHALISI kuna dai linalosema: "Ndio, kufungiwa kwa MwanaHALISI kutatanguliwa". Lakini pia kuna dai kinzani linalosema "Hapana, kufungiwa kwa MwanaHALISI hakutatanguliwa".
Hii inamruhusu mtu asiyeamini kwenye dai la kwanza kuwekeza kwenye dai linigine ambalo yeye anadhani lina tija zaidi.
Na ni ruksa kufanya biashara kwenye madai yote mawili.
Tuzo
Ukishatengeneza U nyingi, unaweza kuzitumia kujinyakulia zawadi.
Zawadi zitakuwa zinwekwa kwenye orodha ya zawadi mara kwa mara. Na zitakuwa zinatolewa kwa mnada. Anayeweka dau la juu, ndiye anajichukulia. Kwa hiyo jinsi unavyobashiri kwa usahihi zaidi, ndio jinsi unakuwa na U nyingi, na ndivyo unavyojiweka katika nafasi nzuri ya kujinyakulia zawadi.
Na sasa ...
Karibu UtuExchange sasa, na utuonyeshe busara yako katika kubashiri yajayo!
UtuExchange: Trading on the future!
Last edited by a moderator: