Karibu JamiiCheck ufanye uhakiki wa Taarifa mbalimbali zinazopatikana ndani na nje ya Mtandao

JamiiCheck

Senior Member
Nov 3, 2023
101
125
IMG_8977.jpeg

JamiiCheck ni Moja kati ya Majukwaa yanayopatikana ndani ya tovuti ya JamiiForums.com. Jukwaa hili limewekwa mahsusi kwa ajili ya kufanya uhakiki, kutafuta uthibitisho au uhalisia wa habari, taarifa, matukio, picha au video mbalimbali zinazojitokeza au kuibuka kutoka katika vyanzo mbalimbali ndani na nje ya mtandao.

Tofauti na Majukwaa na vyombo vingine vya kuhakiki ukweli wa habari, JamiiCheck ni Jukwaa pekee linalotoa fursa kwa watumiaji wake (Wanachama wa JamiiForums.com) kushiriki katika uhakiki kwa kuleta taarifa, picha au Video mbalimbali ambazo wanahitaji kuzichunguza kupata ukweli au chanzo chake pamoja na kuchangia/ kutoa maoni kwenye taarifa nyingine zilizohakikiwa.

Ikiwa utakutana na habari au taarifa yoyote inayokutatiza, ambayo hujui kama ni ya Kweli, Uzushi au Nadharia, tafadhari ilete JamiiCheck ili iweze kufanyiwa uhakiki.

 
Kuna post kwenye jukwaa la siasa kuhusu MBS wa Saudia na Palestine tupeni source.
 
Kuna hii changamoto ya upande mmoja kutoa taarifa lakini ikaonekana upande mwingine inaweza kuathiri maslahi ya pamoja
Sasa badala ya kukanusha kwa weledi wahusika hukimbilia kusema hiyo habari ni bandia.. Yaani habari husika ni halisi lakini kwa maslahi ya kundi fulani inaharamishwa
 
Nainjoyi tu kwataarifa tamu na zenye uhalisia hakika hata sijilamu kuwa member humu. Mpovizuri sana kwa upande wangu bg up sanaaa.
 
JamiiCheck unaweza kweli kuhakiki na kutupa ukweli kuhusu taarifa kuwa kuna siku mwendazake alimnyetia makamu wake usiku wa manane akiwa na lengo la kumla tunda hadi kupelekea makamu kutishia kujiuzuru kwenye nafasi yake?
 
Halafu kabla ya kufuta nyuzi muwe mnacheki tafaadhaal.....kama ule wa kuhoji kazi za KIKOSI CHA ZIMAMOTO NA UOKOAJI>...........yaani hapa mlikera mamia ya wadau......
 
JamiiCheck unaweza kweli kuhakiki na kutupa ukweli kuhusu taarifa kuwa kuna siku mwendazake alimnyetia makamu wake usiku wa manane akiwa na lengo la kumla tunda hadi kupelekea makamu kutishia kujiuzuru kwenye nafasi yake?
Hii haiitaji Jamii check, kwa akili za kawaida tu utabaini ni uongo mkuu
 
Back
Top Bottom