Karamagi aanza kujitetea kwa wapigakura wake

Zee la shamba

Member
Oct 17, 2007
55
3
na Antidius Kalunde (Bukoba) na Salehe Mohamed



JINAMIZI la kashfa ya mkataba tata wa uzalishaji umeme wa Kampuni ya Richmond, bado linaendelea kuwasumbua baadhi ya viongozi, tangu lilipoibuka zaidi ya mwezi mmoja uliopita.
Hali hiyo inajidhihirisha kuwepo kwa tukio la aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi, kujitetea mbele ya wapigakura wake kuhusiana na sakata hilo, huku Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini, William Shelukindo akiishinikiza serikali kuvunja mapema mkataba huo ambazo umelisababishia taifa hasara ya mabilioni ya shilingi.

Karamagi ambaye ni Mbunge wa Bukoba Vijijini, akizungumza na wapigakura wake kwa nyakati tofauti juzi, alisema kuwa aliteuliwa na Rais Jakaya Kikwete kuwa Waziri wa Nishati na Madini Oktoba 16 mwaka 2006 na kwamba mkataba huo ulisainiwa miezi mitano kabla na kuwa alikuta ushauri wa bodi ya wakurugenzi ukiwa umesainiwa Machi 13 mwaka 2006 ukipendekeza Kampuni ya Richomod kupewa zabuni hiyo.

Alisema hata yeye alishangaa maoni ya Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza sakata hilo chini ya uenyekiti wa Dk. Harrison Mwakyembe kudai aliwalazimisha kusaini mkataba huo wakati kipindi hicho alikuwa Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko.

“Wananchi wangu niliingia kwenye nyumba niliyokuta imeanza kuungua na rais wangu aliniweka angalau niweze kuzima moto, nilijitahidi kumwagia maji ili ipoe, lakini ilishindikana, kwani na mimi nilihusishwa pia kwenye uunguzaji wa nyumba,” alisema Karamagi.

Aidha, aliwaeleza wapigakura wake kuwa, maoni ya kamati teule ya bunge iliyodai kuwa yeye alishabikia Kampuni ya Richmond kuuza mkataba kwa Kampuni ya Dowans ni kumsingizia.

Alisema kuwa wakati Richmond inataka kuuza mkataba kwa Dowans, Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania (TANESCO) lilikwishagundua kuwa gridi ya taifa ingezimika na kusababisha nchi kuingia gizani kwa kipindi cha wiki mbili kwa sababu ya upungufu wa kina cha maji.

Aliongeza kuwa kipindi hicho yeye alikuwa safarini nchini Canada akiwa ameambatana na aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa na kwamba akiwa huko alipokea taarifa kuwa Kampuni ya Richmond ilikuwa imepata mashine tatu zenye uwezo wa kuzalisha umeme wa megawatt 60 zikiwa Afrika Kusini na kwamba walitaka kuziuza kwa Kampuni ya Dowans.

Karamagi alieleza baada ya taarifa hizo aligundua kuwa Kampuni ya Richmond ilikuwa ni kampuni ya kitapeli iliyotaka kuiibia serikali, hivyo alimpigia simu Mwenyekiti wa Bodi ya TANESCO akimueleza kutokuwa na imani na kampuni hiyo na kumueleza waziwazi kuhusu utata wa mkataba huo.

Alisema alimuagiza mwenyekiti huyo kufanya uchunguzi wa kina kwa kutumia wataalam wa kuangalia uwezo wa mashine hizo, ili kuinusuru nchi kutapeliwa.

Alieleza kushangazwa na Kamati ya Bunge kutoa mapendekezo kuwa yeye (Karamagi) alishabikia Kampuni ya Dowans kuuziwa mkataba na Richmond.

Mbunge huyo alisema baada ya maoni hayo ya Kamati ya Bunge na yeye kujiuzulu, amewapelekea Spika wa Bunge, Samuel Sitta na Rais Kikwete nakala za barua zinazoonyesha wakati mkataba huo unasaniwa yeye alikuwa Waziri wa Viwanda Biashara na Masoko, hivyo kutohusika kabisa katika sakata hilo.

“Hivi sasa Bunge limeunda kamati ya kuchunguza madai yetu na ikibanika kuwa Kamati Teule ya Bunge ilinisingizia na kunivunjia heshima, watalazimika kuniomba radhi mbele ya umma.

“Wapigakura wangu inabidi muelewe kuwa mlinichagua kuwa mbunge wenu, hamkunichagua kuwa waziri, hivyo mimi ni mbunge halali mpaka mwaka 2010 na hili nalieleza kulinda heshima yangu na chama changu,” alisema Karamagi.

Karamagi, Lowassa na aliyekuwa Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Ibrahimu Msabaha, walitangaza kujiuzulu baada ya Kamati ya Bunge iliyochuguza sakata hilo kuwahusisha katika sakata hilo.

Wakizungumza na Tanzania Daima kwa nyakati tofauti, baadhi ya wananchi wa jimbo hilo, walisema wao kama wapigakura wanasubiri serikali itamke nini kuhusu mbunge wao na wala hawawezi kumhukumu kwa lolote kwa sababu mambo hayo yako nje ya uwezo wao, kwa sababu ndio waliomchagua na kama maelezo yake ni ya kweli, basi wataendelea kumpa nafasi ya kuwatetea bungeni.

Akizungumzia sakata hilo, Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini, William Shelukindo, alisema serikali kuchelewa kufuta mkataba huo hakuwafanyi wabunge wasahau suala hilo ambalo linaigharimu taifa sh milioni 152 kwa siku.

Alisema kamwe serikali isifikiri dawa ya kusahaulika kwa mkataba wa Dowans kwa wabunge ni kukawia kutoa majibu yake, bali itambue itafika muda mambo yatakuwa magumu zaidi pindi wabunge watakapochachamaa.

Alitoa kauli hiyo alipofunga majumuisho katika semina ya wabunge kuhusu muswada wa sheria za umeme na biashara ya mafuta ya petroli iliyofanyika juzi jijini Dar es Salaam.

“Huu mkataba wa Dowans uvunjwe, kuendelea kuvuta muda hakutatufanya tusahau mkataba huo unaoligharimu taifa fedha nyingi ambazo zingetumika kuboresha Tanesco,” alisema Shelukindo.

Alisema hakuna sababu ya kuendelea na mkataba ambao kwanza umeingiwa kimizengwe, pili uwezo wa kampuni husika kuzalisha umeme ni mdogo.

Shelukindo alisema mkataba huo na mingine ndiyo sababu kubwa ya Tanesco kutojiendesha kwa faida, kwani hutoa fedha nyingi kwa kampuni hizo ambazo uwezo wao wa kuzalisha umeme hauridhishi.

Kauli hiyo ya Shelukindo ni msumari mwingine kwa serikali, ambayo imekuja siku chache baada ya wafanyakazi wa Tanesco kuitaka serikali kusimamisha malipo kwa Kampuni ya Dowans kuanzia mwezi huu.

Wafanyakazi hao walisema hawaoni sababu ya kuendeleza malipo kwa kampuni ambayo imerithi mkataba kutoka kwa kampuni hewa ya Richmond.

Source: Tanzania Daima
 
Kama yeye anaamini kuwa alionewa, kudhalilishwa anasubiri nini kwenda Mahakamani ili wasafishe jina lake??????? Yeye ni FISADI tu hata kama akibaki Bukoba Vijijini still ni FISADI. Mlishaona watanzania ni watu tu wa kuwapigia deki nyie mnapita, subirini tu U Ain't seen nothing yet.
 
Kama yeye anaamini kuwa alionewa, kudhalilishwa anasubiri nini kwenda Mahakamani ili wasafishe jina lake??????? Yeye ni FISADI tu hata kama akibaki Bukoba Vijijini still ni FISADI. Mlishaona watanzania ni watu tu wa kuwapigia deki nyie mnapita, subirini tu U Ain't seen nothing yet.

Jamani Speaker mzee six alisema wanaongelea mambo ya bunge nje wanavunja sheria, Karamagi ameshau hilo? mmmhh haya watajitetea sana lakini nadhani wananchi wanajua kuchagua chuya na mchele...
 
na Antidius Kalunde (Bukoba) na Salehe Mohamed



JINAMIZI la kashfa ya mkataba tata wa uzalishaji umeme wa Kampuni ya Richmond, bado linaendelea kuwasumbua baadhi ya viongozi, tangu lilipoibuka zaidi ya mwezi mmoja uliopita.
Hali hiyo inajidhihirisha kuwepo kwa tukio la aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi, kujitetea mbele ya wapigakura wake kuhusiana na sakata hilo, huku Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini, William Shelukindo akiishinikiza serikali kuvunja mapema mkataba huo ambazo umelisababishia taifa hasara ya mabilioni ya shilingi.

Karamagi ambaye ni Mbunge wa Bukoba Vijijini, akizungumza na wapigakura wake kwa nyakati tofauti juzi, alisema kuwa aliteuliwa na Rais Jakaya Kikwete kuwa Waziri wa Nishati na Madini Oktoba 16 mwaka 2006 na kwamba mkataba huo ulisainiwa miezi mitano kabla na kuwa alikuta ushauri wa bodi ya wakurugenzi ukiwa umesainiwa Machi 13 mwaka 2006 ukipendekeza Kampuni ya Richomod kupewa zabuni hiyo.

Alisema hata yeye alishangaa maoni ya Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza sakata hilo chini ya uenyekiti wa Dk. Harrison Mwakyembe kudai aliwalazimisha kusaini mkataba huo wakati kipindi hicho alikuwa Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko.

“Wananchi wangu niliingia kwenye nyumba niliyokuta imeanza kuungua na rais wangu aliniweka angalau niweze kuzima moto, nilijitahidi kumwagia maji ili ipoe, lakini ilishindikana, kwani na mimi nilihusishwa pia kwenye uunguzaji wa nyumba,” alisema Karamagi.

Aidha, aliwaeleza wapigakura wake kuwa, maoni ya kamati teule ya bunge iliyodai kuwa yeye alishabikia Kampuni ya Richmond kuuza mkataba kwa Kampuni ya Dowans ni kumsingizia.

Alisema kuwa wakati Richmond inataka kuuza mkataba kwa Dowans, Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania (TANESCO) lilikwishagundua kuwa gridi ya taifa ingezimika na kusababisha nchi kuingia gizani kwa kipindi cha wiki mbili kwa sababu ya upungufu wa kina cha maji.

Aliongeza kuwa kipindi hicho yeye alikuwa safarini nchini Canada akiwa ameambatana na aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa na kwamba akiwa huko alipokea taarifa kuwa Kampuni ya Richmond ilikuwa imepata mashine tatu zenye uwezo wa kuzalisha umeme wa megawatt 60 zikiwa Afrika Kusini na kwamba walitaka kuziuza kwa Kampuni ya Dowans.

Karamagi alieleza baada ya taarifa hizo aligundua kuwa Kampuni ya Richmond ilikuwa ni kampuni ya kitapeli iliyotaka kuiibia serikali, hivyo alimpigia simu Mwenyekiti wa Bodi ya TANESCO akimueleza kutokuwa na imani na kampuni hiyo na kumueleza waziwazi kuhusu utata wa mkataba huo.

Alisema alimuagiza mwenyekiti huyo kufanya uchunguzi wa kina kwa kutumia wataalam wa kuangalia uwezo wa mashine hizo, ili kuinusuru nchi kutapeliwa.

Alieleza kushangazwa na Kamati ya Bunge kutoa mapendekezo kuwa yeye (Karamagi) alishabikia Kampuni ya Dowans kuuziwa mkataba na Richmond.

Mbunge huyo alisema baada ya maoni hayo ya Kamati ya Bunge na yeye kujiuzulu, amewapelekea Spika wa Bunge, Samuel Sitta na Rais Kikwete nakala za barua zinazoonyesha wakati mkataba huo unasaniwa yeye alikuwa Waziri wa Viwanda Biashara na Masoko, hivyo kutohusika kabisa katika sakata hilo.

“Hivi sasa Bunge limeunda kamati ya kuchunguza madai yetu na ikibanika kuwa Kamati Teule ya Bunge ilinisingizia na kunivunjia heshima, watalazimika kuniomba radhi mbele ya umma.

“Wapigakura wangu inabidi muelewe kuwa mlinichagua kuwa mbunge wenu, hamkunichagua kuwa waziri, hivyo mimi ni mbunge halali mpaka mwaka 2010 na hili nalieleza kulinda heshima yangu na chama changu,” alisema Karamagi.

Karamagi, Lowassa na aliyekuwa Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Ibrahimu Msabaha, walitangaza kujiuzulu baada ya Kamati ya Bunge iliyochuguza sakata hilo kuwahusisha katika sakata hilo.

Wakizungumza na Tanzania Daima kwa nyakati tofauti, baadhi ya wananchi wa jimbo hilo, walisema wao kama wapigakura wanasubiri serikali itamke nini kuhusu mbunge wao na wala hawawezi kumhukumu kwa lolote kwa sababu mambo hayo yako nje ya uwezo wao, kwa sababu ndio waliomchagua na kama maelezo yake ni ya kweli, basi wataendelea kumpa nafasi ya kuwatetea bungeni.

Akizungumzia sakata hilo, Mwenyekiti wa Kamati ya Nishati na Madini, William Shelukindo, alisema serikali kuchelewa kufuta mkataba huo hakuwafanyi wabunge wasahau suala hilo ambalo linaigharimu taifa sh milioni 152 kwa siku.

Alisema kamwe serikali isifikiri dawa ya kusahaulika kwa mkataba wa Dowans kwa wabunge ni kukawia kutoa majibu yake, bali itambue itafika muda mambo yatakuwa magumu zaidi pindi wabunge watakapochachamaa.

Alitoa kauli hiyo alipofunga majumuisho katika semina ya wabunge kuhusu muswada wa sheria za umeme na biashara ya mafuta ya petroli iliyofanyika juzi jijini Dar es Salaam.

“Huu mkataba wa Dowans uvunjwe, kuendelea kuvuta muda hakutatufanya tusahau mkataba huo unaoligharimu taifa fedha nyingi ambazo zingetumika kuboresha Tanesco,” alisema Shelukindo.

Alisema hakuna sababu ya kuendelea na mkataba ambao kwanza umeingiwa kimizengwe, pili uwezo wa kampuni husika kuzalisha umeme ni mdogo.

Shelukindo alisema mkataba huo na mingine ndiyo sababu kubwa ya Tanesco kutojiendesha kwa faida, kwani hutoa fedha nyingi kwa kampuni hizo ambazo uwezo wao wa kuzalisha umeme hauridhishi.

Kauli hiyo ya Shelukindo ni msumari mwingine kwa serikali, ambayo imekuja siku chache baada ya wafanyakazi wa Tanesco kuitaka serikali kusimamisha malipo kwa Kampuni ya Dowans kuanzia mwezi huu.

Wafanyakazi hao walisema hawaoni sababu ya kuendeleza malipo kwa kampuni ambayo imerithi mkataba kutoka kwa kampuni hewa ya Richmond.

Source: Tanzania Daima


Leo nimeamini CCM hawana mshipa wa noma kabisa .Yaani bado Karamagi anasemaje ?
 
Ktk suala zima la Richmond mtu kama ataniambia kwammba JK hausiki na sakata hili itakua ngumu kumuelewa.Nadhani JK alijua fika ubadhirifu wa Richmond na ndio ilikua sababu kubwa ya kumtoa Msabaha pale then wakamuuzia Kalamagi mbuzi kwenye gunia.Alichotakiwa kufanya Kalamagi ilikua ni kulifungua gunia na kuona ndani yake kuna nini.Yeye baada ya kukuta kuna uozo ndani ya gunia unanuka akaamua kuufumbia macho.Kalamagi baada ya kukuta uozo huo yeye alitakiwa kuukataa na kuutangazia umma kwamba jamani ndani ya gunia hili hakufai na nikutokana na uroho wa madaraka tu Karamagi aliamua kuuchubua na sasa yamemtokea puani na madaraka ameyakosa.

Kilichokuponza Kalamagi ni kutunza maiti isiyokuhusu na wanandugu wa marehemu walipokua wakiitafuta na kuikuta kwako lazima watajua wewe ndio muuaji wa ndugu yao.Ukiletewa maiti nyumbani kwako na haikuhusu hatua ya kwanza ni kutoa taarifa Police ili hatua zaidi ziweze kuchukuliwa lakini wewe hukufanya hivyo POLE KARAMAGI.Tunaomba uturudishie na TICS yetu maana na wewe ni FISADI MZURI TU.
 
Alisema hata yeye alishangaa maoni ya Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza sakata hilo chini ya uenyekiti wa Dk. Harrison Mwakyembe kudai aliwalazimisha kusaini mkataba huo wakati kipindi hicho alikuwa Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko.

“Wananchi wangu niliingia kwenye nyumba niliyokuta imeanza kuungua na rais wangu aliniweka angalau niweze kuzima moto, nilijitahidi kumwagia maji ili ipoe, lakini ilishindikana, kwani na mimi nilihusishwa pia kwenye uunguzaji wa nyumba,” alisema Karamagi.

Aidha, aliwaeleza wapiga kura wake kuwa, maoni ya kamati teule ya bunge iliyodai kuwa yeye alishabikia Kampuni ya Richmond kuuza mkataba kwa Kampuni ya Dowans ni kumsingizia.

Alisema kuwa wakati Richmond inataka kuuza mkataba kwa Dowans, Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania (TANESCO) lilikwishagundua kuwa gridi ya taifa ingezimika na kusababisha nchi kuingia gizani kwa kipindi cha wiki mbili kwa sababu ya upungufu wa kina cha maji.

Aliongeza kuwa kipindi hicho yeye alikuwa safarini nchini Canada akiwa ameambatana na aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa na kwamba akiwa huko alipokea taarifa kuwa Kampuni ya Richmond ilikuwa imepata mashine tatu zenye uwezo wa kuzalisha umeme wa megawatt 60 zikiwa Afrika Kusini na kwamba walitaka kuziuza kwa Kampuni ya Dowans.

Karamagi alieleza baada ya taarifa hizo aligundua kuwa Kampuni ya Richmond ilikuwa ni kampuni ya kitapeli iliyotaka kuiibia serikali, hivyo alimpigia simu Mwenyekiti wa Bodi ya TANESCO akimueleza kutokuwa na imani na kampuni hiyo na kumueleza waziwazi kuhusu utata wa mkataba huo.

Alisema alimuagiza mwenyekiti huyo kufanya uchunguzi wa kina kwa kutumia wataalam wa kuangalia uwezo wa mashine hizo, ili kuinusuru nchi kutapeliwa.

Alieleza kushangazwa na Kamati ya Bunge kutoa mapendekezo kuwa yeye (Karamagi) alishabikia Kampuni ya Dowans kuuziwa mkataba na Richmond.

Source: Tanzania Daima

Hivyo basi, kama yeye anakiri kuwa aligundua kampuni ni ya kitapeli, kwa nini aliruhusu mkataba uuzwe kwa Dowans? Kwa nini hakumshurtisha Waziri Mkuu na Rais wavunje mkataba wa Richmond pale ilipobainika ni kampuni ya kitapeli?

Ndiyo yeye hakuingia mkataba na Richmond, alikuwa wizara nyingine. Je katika usimamizi wake wa Wizara ya Viwanda na Biashara si alitumika kutoa kibali cha usajili na kuhakikisha kuwa wawekezaji hawa wanapewa huduma za VIP?

Kwa nini hawa jamaa wanaendelea kutufanya sisi mazobwe kama hatuwezi kufikiri na kung'amua uzembe wao?

It would have been easier for him to come out and acknowledge that due to uzembe, we have got Tanzania into a bad contract that has made lives of Watanzania more difficult. Wananchi ingekuwa ni rahisi kumsamehe, lakini si kiburi na vitisho vya kudai jina lisafishwe au kudai mamilioni!
 
Tangu mara ya kwanza kumuona public nilitokea kumchukia huyu baba hasa kwa namna anavyoongea bila kufikiria. Sasa napiga hatua moja mbele kwamba labda ana matata ktk ubongo wake hivyo labda akachunguzwe na wataalam kama yupo sawa.
 
Karamagi,

Kelele zako hazitusumbui........You are a dead case................mind you however we are not yet done with you.........na mkataba wako wa TICTS kule bandarini.......tutakula sahani moja na wewe.......we there!!.......tik tak tik tak tik tak
 
Back
Top Bottom