Bahati furaha
JF-Expert Member
- Jul 11, 2012
- 3,030
- 1,384
Kinapatikana kwa majirani zetu Kenya kwa KSH 310Ntakitafuta nijisomee niongeze mbolea kwenye ubongo wangu make dilution imezidi kutokana na viongozi wa hii awam.
Kinapatikana kwa majirani zetu Kenya kwa KSH 310Ntakitafuta nijisomee niongeze mbolea kwenye ubongo wangu make dilution imezidi kutokana na viongozi wa hii awam.
Ha ha aha ! Pole ya nini tena?Pole
Hivi kwa zama hizi ambazo kumkosoa mh.rais ni kosa la jinai
Ingekuwa zama hizi, kisingefungiwa kitabu tu bali hata mtunzi angefungwa!eti zama hizi kumkosoa mheshimiwa ni kosa, ni lini ilikuwa sio kosa ?
umesoma kilichoandikwa humu kwamba hiki kitabu kilifungiwa?
halafu tunaambiwa Nyerere alikuwa hapigi mawazo makonzi...
wazee waongo kweli hawa
Mkuu zamani wabongo walikuwa wanaandika Fasihi bora sana. Sikuhizi ukikuta riwaya zinazouzwa hazivutii hata kusoma na macover yao ya marangirangi.
Nilibahatika kusoma Dunia uwanja wa fujo.Hicho Kaptula la Marx sijawahi soma. Ni wakati wa serikali na Baraza linalohusika wafungulie vitabu walivyofungia. Kuna kile shamba la wanyama/ Animal farm na kile the dark side of Nyerere. Hakuna haja ya kuendelea kuvifungia. Kuna kitabu kimoja cha zamani kinaitwa Bosi, umewahi kisoma?
Ila huyu Kezilahabi alikuwa na lugha kalikali. Kwenye Dunia uwanja wa fujo kuna kabinti kalibalehe na kakaanza ishu za wavulana vichakani. Basi dingi yake akakakamata na kuanza kukapa stiki huku akisema " vimatako vyenyewe vikavu halafu unataka kutuletea nyege"
Mkuu hujaelekezwa namna ya kuattac, uweke hicho cha Rosa mistikaJapo mimi si wa makamo sana ila husoma sana Vitabu vya hawa nguli wa fasihi.
E. Kezilahabi nimesoma vitabu vyake kadhaa. Nilipenda zaidi Rosa mistika. Aisee hicho hakiishi utamu. Kinaendana na mazingira ya kila namna. Ama kwa hakika kila nikikisoma hugundua jambo jipya katika mtoririko wa aya zake.
Vile vile Dunia uwanja wa fujo nakumbuka harakati za Tumaini na jinsi alivoishia hukumu ya kunyongwa.
Kiufupi, mimi hupendelea riwaya zenye Kunga na uficho fulani kifasihi ambao hauhitaji mtu uelewe moja kwa moja kinachozungumzwa.
Ndio maana Hussen Tuwa nae huwa ananikamata sana na mfululizo wa vitabu vyake.
Ben R. Mtobwa nae huwa sishibi bubujiko la lugha yake ya kifasihi.
Nina soft copy ya Rosa mistika na Nagona. Ila nashindwa kuviattach hapa. Nielekezeni
Mkuu hujaelekezwa namna ya kuattac, uweke hicho cha Rosa mistika
Kwa mind set yako hii unahitaji miaka hamsini kizazi cha nyuma yako kukusoma kwamba watu wa aina yako ndio mlichelewesha uhuru wa fikra!Aliona mbali mwandishi
Mfano leo hii kuna vyama vya upinzani hata haviwezi kujiongoza ati wanataka kuongoza Nchi!! Nchi gani waongoze sasa?
Waendelee kujifariji tu