Kapata kazi ya 120,000/= afanyeje?

aende akafanye kaz,itamsaidia kupata experience pia ni mwanzo wa kupata chanel nyngne.
 
Wahindi walivyo akubali alafu akifika kule awaambie jamani hii hela kwa mazingira haya haitoshi nimeshindwa au nipeni 150. Huwa wanapandisha ilimradi isiwe too much. Wanataja viwngo duni watu wakiwagomea huwa wanapandisha ila uwe kazini na wamesha ku train lakini haujaanza kazi au fanya siku moja kwa bidii sana waone mchapa kazi alafu wakomalie wapandishe.
 
Aende kwa mentality ya kama internship tu, halafu awe mwangalifu kwenye mkataba terms and condition hususani kwenye termination.
 
Habarini ndugu zangu..nimeombwa ushauri na mimi pia nawaombeni ninyi ushauri...kuna binamu yangu aliyehitimu IFM 2010 fani ya accountancy...baada ya kula msoto wa muda mrefu amepata ajira atakayokuwa analipwa 120,000/- kwa mwezi kwenye kampuni moja ya kihindi..itambidi atoke dar aende morogoro kama eneo lake la kazi...anaomba ushauri wenu wazoefu wa maisha kama hiyo kazi itakuwa na maslahi kwake! asanteni...!
Akafundishe ale angalau laki tano, kazi bongo zipo nyingi n kitendo cha yeye kusota mwaka ni uzembe.
 
Habarini ndugu zangu..nimeombwa ushauri na mimi pia nawaombeni ninyi ushauri...kuna binamu yangu aliyehitimu IFM 2010 fani ya accountancy...baada ya kula msoto wa muda mrefu amepata ajira atakayokuwa analipwa 120,000/- kwa mwezi kwenye kampuni moja ya kihindi..itambidi atoke dar aende morogoro kama eneo lake la kazi...anaomba ushauri wenu wazoefu wa maisha kama hiyo kazi itakuwa na maslahi kwake! asanteni...!
Mkuu kwa ushauri wangu:- kijana akubali offer na aende popote afuate haya :- 1. ajitume 2. awemwaminifu 3. aheshimu wenye mali hayo yote yatazaa yafuatayo EXPERIENCE,PROMOTION,TRUST hapo baadaye kwa mantik zake kazini atapandishwa mshahara na bonus!! Good luck for him.....blessings
 
kwani kima cha chini ni bei gani? hiyo mbona kama analipwa ndogo zaidi ya kima cha chini au!

ila kufanya kazi na wahindi napo yataka moyo, ile tabia yao ya udosi huwa hawaachi
 
hiyo kazi asiende, bora atafute ka robo eka apande nyanya chungu na mabilinganya. hata we mwenyewe msaidie senti za kuanzia.
 
jamani mie naona hiyo pesa ni ndogo, nikifikiria hapa Dar dereva tu anayeendesha familia kwa masaa machache kwa siku anapokea elfu 7 na hapo anapewa nauli, anapewa mabonus extra incase akihitajika siku nzima au kwenda sherehe hadi usiku wa manane au hata karibu midnight.

Sasa huyo amesoma naoa hii ni kuonewa na hawa wahindi na wenzetu pia, i guess hapo atalipa rent, kula, kuvaa etc. amefuatilia kima cha chini kwa shahada yake ni shs ngapi? kwenye interview aliwaonyesha anajua kiwango cha kazi yake na shahada aliyopata?

hg mie anapata na elfu 6 kwa siku plus bonus kibao. na wote wanapata chai, chakula juu. wanasaidiwa pia kujiendeleza.

inasikitisha sana, ila kama ana pakukaa na anataka experience then labda ila asiache kutafuta kazi.

Mie naona wahindi wabairi sana.
 
halafu akiwa mwizi/mla rushwa mtamlaumu? afadhali angekuwa anakaa nyumbani kwao kila kitu kipo..mbaya zaidi anaenda mkoa mpya ambao hata network ya watu hana kwamba anaweza kupata support...huo ni upuuzi..there is more to life than just kuajiriwa...THINK BIG kama kweli we ni msomi..huo ni udhalilishaji..si bora uwe houseboy unapewa msosi bure na matibabu na kulala bure? You can do better than that..huu unyonge ndo unatufikisha hadi hapa na kwa kuwa cheap labor zipo nyingi hivi hata hao waajiri hawatapandisha mishahara hata siku moja maana wanajua hata wakisema mshahara 50,000 na uwe graduate watapata watu...kuna business kibao hapa mjini anaweza kufanya akatoka kuliko kwenda kukaa ofisini kwa mhindi ambae hathamini utu wala elimu yako...ingekuwa serikalini ningekushauri uende but si kwa mhindi tena mkoa mwingine..
 
Hapa sio kijiwe cha Saisa,hata kije chama gani kama kichwa buyu ni buyu tu.Msingi ni kujituma

Jamaa we nenda kafanye kazi.
Mshahara huo lazima nyumba atakuwa amepewa kama Staff house.

We nani kakuambia ukiwa msomi usifanye kazi ya kipato kidogo,kama wewe unajiona msomi basi hizo degree siku hizi kama darasa la saba tu zilivyo mjini.

Na ndio mana hawa wenye kujiona wana Elimu ya Chuo wanazurura mjini wakidharau kazi za wenzo,wakati muuza maji wa mjini anaingiza hesabu kuliko yeye.
We muuza maji tu aningiza si chini ya Tsh:5,000 kwa siku wewe ukipishananae tu na vyeti vyako.

-Kwanza Itakusaidi kupata uzoefu na kujuana na watu
-Uaminifu ndio kitu muhim,na pia ndio sehem ya kuonyesha taalum yako.
-Kaa na wafanyakazi wenzako wote vizur bila kubagua,huwezi kujua nani mwema na nani atakuwa kuwa msaada na chanzo cha channel nyingine,ukiiishi vizuri unaweza kukuta mwenzako alietoka hapo na kwenda kwingine akakutafuta ili upate kazi yenye maslahi mazuri.Mwanzo uwe na pakushika kwanza.Wewe mwanaume na muhim ni kujituma na kufanyakazi yoyote halali,hao unaowaona waliofanikiwa wamepitia safari ndefu ila leo tunaona kama wamepata pesa juzi ila siri yao ipo moyoni.

-Pia usijifanye wewe ni msomi au mjuaji,be cool and friendly one to all staffs,hapo utaona njia ya mafanikio.Usifanye tu tamaa ya kutaka utajiri wa mapema wa kupanga wizi,hapo ni kwamba mungu hatokuwa pamoja na wewe.

-Mwisho ni kwamba Mshirikishe mungu katika kila nyendo yako ya maisha ili akupe ustahamilivu,subra na njia.
acha anasa,na kama ni mlevi acha kabisa kitu hicho.
Ni Bora upate kidogo lakini ni chako na chenye Kheir na baraka za Mungu ili mwisho wa maisha pia uwe mwema kwako.

Well said Mkuu.
 
nisameheni ila me nisingeenda. Tena wahindi? Afadhali watu wengne. Mh kama hali ndo hii ngoja niendelee kugangamala na kasaluni kangu kuliko utumwa wa wazi hivi mh.
 
nisameheni ila me nisingeenda. Tena wahindi? Afadhali watu wengne. Mh kama hali ndo hii ngoja niendelee kugangamala na kasaluni kangu kuliko utumwa wa wazi hivi mh.

Una xperience nao nini hawa? Ebu nidokeze.. :car:
 
Nenda labda kuna mwanya wa kuiba.

Kuna jamaa yangu alinionyesha salary ya Mwandui ilikuaga ni ka 18000, lakini jamaa anamajumba na magari ya hatari.

Mshahara wa waziri mkuu ni mil 6, lakini akitengeneza semina au safari, hata mil 25, inaweza fika.
Kwa iyo cheki ka kuna allowances ka izo.
 
Duh japokuwa ajira ngumu but 120 jamani, huu ni ukiukwaji wa haki za binadamu, nyumba atalipa kodi bei gani, nauli bei gani, chakula bei gani na mavazi bei gani.

Hivi unajua kima cha chini kilichowekwa na serikali kwa sekta binafsi ni shilingi ngapi? Ukipata hilo jibu basi mengine utajaza mwenyewe.
 
Ukishangaa ya Musa utayaona ya Firauni. Hii ndiyo Tanzania iliyoshindwa kupanga viwango vya mishahara inayokidhi sifa na daraja la mtu kulingana na elimu yake. Tumeachia kila mnyama kula kwa ujanja wake wa porini, kwa urefu wa makucha yake na ukali wa meno yake. Soko huria kwa kila kitu. Kazi mbaya ni hiyo uliyonayo ila kama huna kazi hata ile mbaya yenye kipato kidogo inakuwa nzuri sana.
 
Back
Top Bottom