Elections 2010 Kanuni za Uchaguzi 2010 na mgogoro wa Sheria ya Gharama

Status
Not open for further replies.
Kikwete siyo maamuma asaini asichokijua.
anajua alichosaini ndo maana akasaini kwa mbwembwe. hiyo ishu ya kudanganywa naiweka pembeni. atakuwa anajua kilichoongezwa offtrack.
 
“(a) Kwa kesi ya urais watathibitishwa na Msajili, (b) Kwa kesi ya Mbunge watathibishwa na Katibu Tawala wa Wilaya na (c) Kwa kesi ya Diwani watathibitishwa na Katibu Tarafa...,” ilieleza sehemu ya sheria hiyo iliyosainiwa na Rais Kikwete ambayo nakala yake tunayo.
Kama sehemu hii haikujadiliwa na bunge kwa hiyo rais alisaini kwa mbwembwe kitu ambacho hana uhakika nacho kwa lugha nyepesi alisaini kanyaboya blank cheque
 
2: Hili lingine la kumsainisha Rais sheria ambayo haijapitishwa bungeni, ni la hatari sana. Kama vipengele fulani vya sheria vilichomekwa baada ya bunge kupitisha, ni wazi, alichosaini Rais sicho kilichopitishwa na Bunge; na hivyo alichosaini Rais ni batili!

Mambo mengi yanayofanywa na watendaji serikalini huwa ni kipimo cha jinsi mkuu wao anavyoheshimika. Madaraka aliyonayo Rais ni makubwa sana na adhabu anayoweza kumpa mtendaji mbovu ni kubwa au kali kiasi kwamba kila mtumishi alistahili kuogopa kucheza na madaraka yake.

Kwa hilo ulilotaja, kama mtu anadiriki kucheza na nguvu hiyo ya Rais maana yake ni kwamba huyo mtu kesha fahamu udhaifu wa Rais. Anajua hatafanya lolote kiasi cha kumpa taabu.
 
Somethings is seriously wrong, somewhere. Je dk Slaa hakuna reverse? Bunge haliwezi kuhoji uhuni wa watengeneza kanuni? Najua sheria hupitishwa na kanuni baadaye hili linakuwaje dk slaa au yeyote anayejua sheria tujuzeni hii ni kanuni au ndio sheria yenyewe?
 
Viongozi wetu tuliowapa madaraka ya kuamua mambo muhimu ya taifa hili kama wangekuwa wanaweka kipaumbele kusoma nyaraka zinazopita ndani ya in trays zao basi tusingekua na mikataba na makubaliona mabovu kama tuliyo nayo kwa sasa. Kutosoma kwao kumeelingiza taifa katika mikataba mibovu ambayo ni sawa na kuuza rasilimali zetu na mwishowe tutajeuzwa manamba kwenye mashamba na migodi yao kama ilivyo kwa Kisarawe na Rufiji (Jatropha), migodini kote ndiyo usiseme, kwenye vitalu vya uwindaji ndiyo nyara kebe wa kebe hatuna faida nazo. Nikiendelea kutaja nitazimia hapa!!!

Brazo Dr. Slaa kwa kutupa changamoto hata tulio mafisini na tuna dhamana tunahitaji kuwa na tabia ya kusoma between lines stricktly, tena kama huna muda just take some hours or day jifungie ikiwezekana hata hotelini soma na tafakari, usikurupuke. Unajua CEOs wengi na viongozi waandamizi serikalini huwa wana allowance inawaruhusu kuwa nje ya ofisi ili kupata muda muafaka wa kupitia mambo muhimu na inagharamiwa na ofisi husika. Nafikiri inafanyika but je ni kwa ajili ya kazi ya kiofisi reaaaaaaalllyyyyyy au ni kwa shughuli binafsi na bill zinaletwa maofisini. Tuwe serious!!! It pains!!! Ha.
 
The blue bolded statement from mzee wa vijisent worries me if he is real a lawyer if he knows the meaning of corruption.
That is why he wanted it to be part of the law so that cannot be construed as corruption!!! he is a clever chap!! But if people part of your campaign team they should be hospitalised or taken care by the campaign fund and not their own money as that will even be a dangerous situation as you have to find ways of paying back them after the elections!!!
 
Wajuvi wanasikiliza pande mbili kabla ya kufikia conclusion, Silaha kasema hivyo sasa tusubiri upande mwingine lakini tukirejea historia na utaratibu mzima wa maaumizi hapa bongo hilo tayari limepita labda kama kuleta utata usio na tija kama kawaida yetu.

Ukisoma between lines kama mwaandishi ametia chumvi zaidi na kufanya watu wote kuwa makomongo (vichwa maji) isipokuwa Dr. Slaa. Kitu ambacho sio kweli labda kama mwandishi wa Tanzania Daima tutaelewa anamaanisha nini. Wadau wameitwa watoe maoni manake nia ya serikali ni nzuri na kama Dr. katoa maoni poa. Cheyo katoa maoni yake na Lipumba pia katoa.
 
Kikwete siyo maamuma asaini asichokijua.
anajua alichosaini ndo maana akasaini kwa mbwembwe. hiyo ishu ya kudanganywa naiweka pembeni. atakuwa anajua kilichoongezwa offtrack.

Mara baada ya muswada ule kupita bungeni bila mabadiliko ya msingi, Kikwete alijua kuwa alishapata alichokitaka kuufanya uchaguzi wa October uwe TAMBARARE!! Alitupiga dongo na ndio maana akasaini sheria hii kwa mbwembwe; DR. SLAA akaze buti aende mahakamani na kushitaki juu ya ughushaji uliofanyika juu ya sheria hii.
 
Kubwa ni kuhakikisha tunasimamia hili kwanza kwa kwenda mahakamani na kuzuia sheria hii kwanza na kuzuia uchaguzi wenyewe mpaka hapo marekebisho muhimu yatakapofanyika. Big Up Dr. Slaa.
 
umakini haupo
je hakuweza kufanya reference yoyote kabla ya kusaini???
kuna watu wengi hapo watakuwa wamehusika
rais mwenyewe lazima awe kahusika kwa namna moja au nyingine
Tunaangamia kwa kukosa maarifa Hosea 4:6
 
Wajuvi wanasikiliza pande mbili kabla ya kufikia conclusion, Silaha kasema hivyo sasa tusubiri upande mwingine lakini tukirejea historia na utaratibu mzima wa maaumizi hapa bongo hilo tayari limepita labda kama kuleta utata usio na tija kama kawaida yetu.

Ukisoma between lines kama mwaandishi ametia chumvi zaidi na kufanya watu wote kuwa makomongo (vichwa maji) isipokuwa Dr. Slaa. Kitu ambacho sio kweli labda kama mwandishi wa Tanzania Daima tutaelewa anamaanisha nini. Wadau wameitwa watoe maoni manake nia ya serikali ni nzuri na kama Dr. katoa maoni poa. Cheyo katoa maoni yake na Lipumba pia katoa.
Songambele kuna maoni ya kawaida hasa kwenye kanuni ambazo tunajua kila mtu anatoa ili kuboresha utekelezaji wa hiyo sheria hili la kuchomekwa kitu ambacho hakikuwepo sidhani kama liko kwenye sehemu ya maoni ni sehemu ya sheria mama ninachojua mimi sheria ilishapitishwa na bunge kwa hiyo hili la kuchomekwa vipengele haliwezi kutatuliwa na mkutano wa kujadili kanuni litatatuliwa na walioitunga hiyo sheria ambalo ni bunge zima
 
Tatizo kubwa ni watu wa chama tawala na kiongoozi wetu wanafanya vitu bila kutafakari athari zake za baadae (modeling). wamekurupuka sasa hata mwezi bado sheria mpya kabisa hata kuchapishwa na kuzambazwa bado ina utata. Serikali hii inaweza kufanya kitu gani kwa ukamilifu?

Je KILIMO KWANZA iko chini ya Sera na Sheria ipi? Ni Mkakati (strategy) au Tamko au nini katika sheria hiyo? MAANA NAONA KAMA IMEIBUKA NA KUTAFUTIWA MZAZI WAKE

NAOMBA WANAOIELEWA WANISAIDIE
 
Dr. Slaa akienda mahakamani na kuwashinda wanasema ni kipingamizi. Nidhani waandishi wa muswada huu walisahau haya alafu baada ya muswada kupita Bungeni wakakumbuka, wakachomekea na Rais kwa mbwebwe akasaini. Hii ni mara ya tatu Rais anachomekewa. Kule Arusha alifungua hotel kesho yake TanRoads wakabomoa ukuta. Hapa DAR Ambulance alikuja ofisa kutoka Wilaya nyingine. Kwa namna hii kuna hatari Rais wetu kumpongeza mwanafunzi bora na kesho yake tunaambiwa matokeo ya mtihani wa mwanafunzi huyo ni batili. Tutafika kwa kajanja hii?
 
8D6U0734.JPG


Ndiyo maana nilijiuliza kwa nini Mzee Kingunge Ngombale Mwiru ktk hii picha alikuwa ametoa tabasamu kubwa kuliko, kumbe tumeingizwa mjini.
 
Hata kabla ya kuchomekwa hivyo vipengele vinavyolalamikiwa, sidhani kama huu muswada ulikuwa wa kushangiliwa na wapinzani kama wanavyoonekana wamejipanga kwenye picha. Wangeweza ku-protest hata walau kwa kususia mwaliko wa kushuhudia utiaji saini muswada huo. Bado nashindwa kuamini kama hawahawa kina Slaa wanaolia leo ndio walimtuma Komu kuwakilisha chama kwenye utiaji saini muswada huo!
 
Hii kitu kama ni kweli, basi mtu anatakiwa ashitakiwe kwa UHAINI.

Kubadilisha maneno ya kwenye katiba ni sawa na kuvunja katiba tayari.

Namhurumia Kaka Sitta kwani asipoangalia, itaonekana ni yeye alifanya haya madudu.

Akiweza basi yeye mwenyewe ndiyo aende mahakamani haraka sana. Ofisi ya Rais wao wanaweza kujitetea kuwa walipokea hivyo kutoka bungeni. Sasa Sitta ni kazi yako wewe uonyesha haraka sana tofauti ya copy zako na copy alizoweka sahihi Rais. Vinginevyo utapandishwa kizimbani kwa kesi moja mbaya sana.

Hii kesi msione ni kesi kama EPA. Katika ya nchi si kitu cha kuchezea. Kama si leo, basi hata miaka ijayo, kuna watu watakuja kulia kwa madudu waliyoyafanya (kama ni kweli).
Tusubiri tuone.
 
huu ni mkuki kwa upinzani na uvunjaji wa sheria za nchi (kama hii ni kweli basi sasa ikulu inatunga sheria), sasa ngoja tusikie mweshimiwa six(6) mzee wa standard na speed anasemaje kuhusu hili? Na kama ni kweli nani awajibishwe? nashauri kama ni kweli basi wapinzani wakimbilie mahakamani haraka sana.

ndvyo ccm ilivyo,mahakamani haraka simamisha sheria hii kutumika mpaka hapo itakapowekwa sawa.
 
Hata kabla ya kuchomekwa hivyo vipengele vinavyolalamikiwa, sidhani kama huu muswada ulikuwa wa kushangiliwa na wapinzani kama wanavyoonekana wamejipanga kwenye picha. Wangeweza ku-protest hata walau kwa kususia mwaliko wa kushuhudia utiaji saini muswada huo. Bado nashindwa kuamini kama hawahawa kina Slaa wanaolia leo ndio walimtuma Komu kuwakilisha chama kwenye utiaji saini muswada huo!

Mkuu Gagnija,

Ni vipi ulitarajia Dr. Slaa ajue kwamba muswada huo tayari umechomekwa vitu ambavyo havikupitishwa na bunge kabla ya Rais kusaini na hivyo kuamua kutokumtuma mwakilishi (Komu) kwenye sherehe ya kuusaini? Kila mtu alitarajia alichosaini rais ni kile kilichopitishwa na bunge lakini wakali kama Dr. Slaa wamekuja kushtuka kwamba walichopitisha, sicho rais alichosaini. Huwezi jua bado kuna vipengele vingine vimeongezwa kinyemela lakini bado havijashtukiwa!!!

Tiba
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom