Uchaguzi 2020 Kanuni mpya CCM: Tumaini la pekee la Makonda, Mtulia, Mtolea, Nassari, Mwakyembe na Mwanri ni Kamati Kuu ya CCM chini ya Rais Magufuli

Atakavyoamka siku hiyo hajasema kuwa atahamisha mtu kutoka kusini akagombee kaskazini. Na kanuni za chama zipo wazi kuwa majina matatu ndio yataenda kamati kuu kujadiliwa, washindi watatu wa mwanzo.
Sio kanuni ni atakavyoamka
 
Watu mnakuwa wa ajabu,Magu angetaka apite angepita Kigamboni,huko kapigwa chini na kamati itampiga chini
Watu hawawi wa ajabu bali wasiwasi wao unatokana na tabia ya Chama Tawala kubadili gia angani wakati wowote. Kamati ina wajumbe wachache sana inakuwa rahisi zaidi kugawa bahasha nzito hata kubadili misimamo ya Chama kama ipo. Kikao cha Kamati kinaongozwa na Mwenyekiti ambaye maamuzi yake yanategemea alivyoamka siku hiyo ielewke kuwa wahusika waliotupwa na kura za maoni ni wapendwa wake. Mwenyewe kwa kauli yake amesema na amewahi kufanya kuwa wa kwanza anaweza kuwa wa mwisho na wa mwisho akawa wa kwanza ndo maana orodha yote ya wahusika wa kura za maoni inawakilishwa kwenye Kikao cha uteuzi cha Kamati. Waliotemwa na kura za maoni walikuwa na kazi za madaraka makubwa lakini kwa maagizo toka juu waliyaacha kwenda kugombea Ubunge na nafasi zao kujazwa mara mojà kukiwa na uhakika wa kupita kwenye kura za maoni lakini hata hivyo hakuna lililoharibika Mpendwa atarekabisha. CCM mpya na mapya!
 
Sasa umma wa Tanzania unafahamu kuwa watajwa hapo juu ambao walitia nia kugombea Ubunge kwenye majimbo mbalimbali hapa nchini. Katika kura za maoni zilizoendeshwa hapo jana ndani ya CCM, wote hao wamezidiwa kwenye kura za maoni kwenye Majimbo yao: wengine wameachwa mbali sana na wengine wamepitwa kiasi kidogo.

Kwa mujibu wa Kanuni 'mpya' za kiuchaguzi ndani ya CCM kadiri ninavyozifahamu, makabrasha ya waliopigiwa kura za maoni yatawasilishwa Kamati Kuu kwa ajili ya uamuzi kufanyika. Kamati Kuu ndiyo itakayoamua juu ya mgombea halisi wa Jimbo lolote la kiuchaguzi kwa tiketi ya CCM.

Naamini, bado akina Dr. Mwakyembe wana imani ya kuwa wagombea. Wana imani ya kuteuliwa na Kamati Kuu ya CCM itakayoketi kuamua chini ya Rais Magufuli. Kama ilivyowahi kushuhudiwa huko nyuma (kama ilivyotokea kwenye lililokuwa jimbo la NZEGA mwaka 2010 ambapo mshindi wa tatu Dr. Kingwangala ndiye aliyeteuliwa akiachwa Bashe na Selelii).

Kura za Maoni za jana na leo zinatoa tu sura na dalili za ushindi kwa wanaoongoza Majimboni. Si kura za kuhitimisha. Kamati Kuu bado yaweza kuteua kinyume na matarajio ya wengi. Kamati Kuu, hakika, inabaki kuwa tumaini pekee la washindwa wa jana na leo.
Kosa jingine la kiufundi litakalo izamisha ccm kwenye uchaguzi mkuu, haiwezekani kamati kuu ya watu 24 tu kuwa na maamuzi ya kibabe.
 
R
Tatizo ni kwamba safari hii uchaguzi wameamua kuufanya wazi hakuna figusu wala rushwa so far, unamkata mtu kwa kigezo gani?

Labda kama alishahukumiwa kwa kosa kubwa kisheria huko nyuma au mgombea misimamo yake ina utata na mlengo wa CCM. Nje ya hapo kukata mtu inakuwa kama ni uporaji wa maamuzi ya kidemokrasia.

Rushwa ipo aisee! Tena rushwa kubwa mno. Fanya restrospective investigation utapata ukweli.
 
Sasa umma wa Tanzania unafahamu kuwa watajwa hapo juu ambao walitia nia kugombea Ubunge kwenye majimbo mbalimbali hapa nchini. Katika kura za maoni zilizoendeshwa hapo jana ndani ya CCM, wote hao wamezidiwa kwenye kura za maoni kwenye Majimbo yao: wengine wameachwa mbali sana na wengine wamepitwa kiasi kidogo.

Kwa mujibu wa Kanuni 'mpya' za kiuchaguzi ndani ya CCM kadiri ninavyozifahamu, makabrasha ya waliopigiwa kura za maoni yatawasilishwa Kamati Kuu kwa ajili ya uamuzi kufanyika. Kamati Kuu ndiyo itakayoamua juu ya mgombea halisi wa Jimbo lolote la kiuchaguzi kwa tiketi ya CCM.

Naamini, bado akina Dr. Mwakyembe wana imani ya kuwa wagombea. Wana imani ya kuteuliwa na Kamati Kuu ya CCM itakayoketi kuamua chini ya Rais Magufuli. Kama ilivyowahi kushuhudiwa huko nyuma (kama ilivyotokea kwenye lililokuwa jimbo la NZEGA mwaka 2010 ambapo mshindi wa tatu Dr. Kingwangala ndiye aliyeteuliwa akiachwa Bashe na Selelii).

Kura za Maoni za jana na leo zinatoa tu sura na dalili za ushindi kwa wanaoongoza Majimboni. Si kura za kuhitimisha. Kamati Kuu bado yaweza kuteua kinyume na matarajio ya wengi. Kamati Kuu, hakika, inabaki kuwa tumaini pekee la washindwa wa jana na leo.

Iweje tuandikie mate na wino upo? July 27 sio mbali. Ukweli utataradadi.
 
Hilo ndiyo la msingi kuwa tumemuonyesha mteuzi wao kuwa hao watu hatuwahitaji.

Uchaguzi wa ndani wa wagombea ndiyo ilikuwa njia ya kutolea sauti za watawaliwa kwa mteuzi kuwa watu wake anao wateua kutuongoza hatuwataki.
Haya hayatuhusu muhimu ni hakubaliki...full stop!
hata akimbeba ampe unaibu waziri mkuu atajua mwenyewe
 
Swadakta
Aiseee. Muhimu zaidi wanaoitwa wanyonge huku chini wamesha amua. Hayo ya kamati kuuu hayata badili mtazamo mpana wa jamii husika juu ya hao walio kataliwa.

Wakipitishwa na kamati kuu ni sahihi na haki wakiitwa wagombea wa viti maalumu.
 
Sasa umma wa Tanzania unafahamu kuwa watajwa hapo juu ambao walitia nia kugombea Ubunge kwenye majimbo mbalimbali hapa nchini. Katika kura za maoni zilizoendeshwa hapo jana ndani ya CCM, wote hao wamezidiwa kwenye kura za maoni kwenye Majimbo yao: wengine wameachwa mbali sana na wengine wamepitwa kiasi kidogo.

Kwa mujibu wa Kanuni 'mpya' za kiuchaguzi ndani ya CCM kadiri ninavyozifahamu, makabrasha ya waliopigiwa kura za maoni yatawasilishwa Kamati Kuu kwa ajili ya uamuzi kufanyika. Kamati Kuu ndiyo itakayoamua juu ya mgombea halisi wa Jimbo lolote la kiuchaguzi kwa tiketi ya CCM.

Naamini, bado akina Dr. Mwakyembe wana imani ya kuwa wagombea. Wana imani ya kuteuliwa na Kamati Kuu ya CCM itakayoketi kuamua chini ya Rais Magufuli. Kama ilivyowahi kushuhudiwa huko nyuma (kama ilivyotokea kwenye lililokuwa jimbo la NZEGA mwaka 2010 ambapo mshindi wa tatu Dr. Kingwangala ndiye aliyeteuliwa akiachwa Bashe na Selelii).

Kura za Maoni za jana na leo zinatoa tu sura na dalili za ushindi kwa wanaoongoza Majimboni. Si kura za kuhitimisha. Kamati Kuu bado yaweza kuteua kinyume na matarajio ya wengi. Kamati Kuu, hakika, inabaki kuwa tumaini pekee la washindwa wa jana na leo.
Siyo rahisi kurudishwa mtu ambaye amepata kura 2 akaondolewa aliyepata kura 200
 
Back
Top Bottom