Uchaguzi 2020 Kanuni mpya CCM: Tumaini la pekee la Makonda, Mtulia, Mtolea, Nassari, Mwakyembe na Mwanri ni Kamati Kuu ya CCM chini ya Rais Magufuli

Ndugu yangu Peter upo kwenye jukwaa hili la siasa muda mrefu kwelii wewe wakusema "KANUNI MPYA" wakati hata 2010,2015 zilikuwepo, na mifano hai ipo wakina Kigwangala.
Mkuu, wakati ule majina matatu ya kupigiwa kura yalitokea Kamati Kuu halafu yakapigiwa kura na kurejea huko. Kwasasa, wote waliotia nia wamepigiwa kura kwanza kabla ya kupelekwa Kamati Kuu kwa maamuzi. Huo ndiyo upya. Tena, wakati ule wanachama wote wa CCM jimboni walipiga kura. Kwasasa ni Kamati ya Jimbo tu ndiyo iliyopiga kura. Kanuni zimebadilika.
 
Mkuu, wakati ule majina matatu ya kupigiwa kura yalitokea Kamati Kuu halafu yakapigiwa kura na kurejea huko. Kwasasa, wote waliotia nia wamepigiwa kura kwanza kabla ya kupelekwa Kamati Kuu kwa maamuzi. Huo ndiyo upya. Tena, wakati ule wanachama wote wa CCM jimboni walipiga kura. Kwasasa ni Kamati ya Jimbo tu ndiyo iliyopiga kura. Kanuni zimebadilika.
Nadhani kilichobadilika ni utaratibu tuu namna na upigaji kura lakini KANUNI YA KAMATI kuu kuwa mwamuzi wa Mwisho imebaki palepale.
 
Zako zinasemaje? Kwamba kura za maoni ndiyo mwisho?
Ndo mana nikakwambia acha uongo..hii kanuni sio ivo weeh ulivyoutafsiri ilihusu zaidi kama mgombea hakupatikana kwa misingi ya haki...its means labda kwa mipango ya Rushwa au vitisho ndo akamaanisha kutakua na panga la mwsh..asa unaleta uzi wa uongo tukuangalie tuu
 
Tatizo ni kwamba safari hii uchaguzi wameamua kuufanya wazi hakuna figusu wala rushwa so far, unamkata mtu kwa kigezo gani?

Labda kama alishahukumiwa kwa kosa kubwa kisheria huko nyuma au mgombea misimamo yake ina utata na mlengo wa CCM. Nje ya hapo kukata mtu inakuwa kama ni uporaji wa maamuzi ya kidemokrasia.
Nakuunga mkono
 
Sidhani Kama kamati kuu lengo lake Ni kuonesha "ubabe" wao kwa kuchagua yeyote wanayemtaka.Wenye "tumaini" kwa kamati Ni wale ambao pengine mchakato wa kupata mshindi wa kura za maoni uligubikwa na makandokando mengi au mshindi kuwa walakini.Amini,kwa Mambo yalivyokwenda,asilimia kubwa ya walioongoza Katika mchakato wa awali ndio watakaopitishwa.
Sasa umma wa Tanzania unafahamu kuwa watajwa hapo juu ambao walitia nia kugombea Ubunge kwenye majimbo mbalimbali hapa nchini. Katika kura za maoni zilizoendeshwa hapo jana ndani ya CCM, wote hao wamezidiwa kwenye kura za maoni kwenye Majimbo yao: wengine wameachwa mbali sana na wengine wamepitwa kiasi kidogo.

Kwa mujibu wa Kanuni 'mpya' za kiuchaguzi ndani ya CCM kadiri ninavyozifahamu, makabrasha ya waliopigiwa kura za maoni yatawasilishwa Kamati Kuu kwa ajili ya uamuzi kufanyika. Kamati Kuu ndiyo itakayoamua juu ya mgombea halisi wa Jimbo lolote la kiuchaguzi kwa tiketi ya CCM.

Naamini, bado akina Dr. Mwakyembe wana imani ya kuwa wagombea. Wana imani ya kuteuliwa na Kamati Kuu ya CCM itakayoketi kuamua chini ya Rais Magufuli. Kama ilivyowahi kushuhudiwa huko nyuma (kama ilivyotokea kwenye lililokuwa jimbo la NZEGA mwaka 2010 ambapo mshindi wa tatu Dr. Kingwangala ndiye aliyeteuliwa akiachwa Bashe na Selelii).

Kura za Maoni za jana na leo zinatoa tu sura na dalili za ushindi kwa wanaoongoza Majimboni. Si kura za kuhitimisha. Kamati Kuu bado yaweza kuteua kinyume na matarajio ya wengi. Kamati Kuu, hakika, inabaki kuwa tumaini pekee la washindwa wa jana na leo.
 
Nadhani kilichobadilika ni utaratibu tuu namna na upigaji kura lakini KANUNI YA KAMATI kuu kuwa mwamuzi wa Mwisho imebaki palepale.
Ili kutokuleta mgawanyiko, makonda apitishwe kugombea Buchosa, Dr tizeba aende sumve, na shigongo aende Kibamba. Mwanry apelekwe Kawe
 
Ndo mana nikakwambia acha uongo..hii kanuni sio ivo weeh ulivyoutafsiri ilihusu zaidi kama mgombea hakupatikana kwa misingi ya haki...its means labda kwa mipango ya Rushwa au vitisho ndo akamaanisha kutakua na panga la mwsh..asa unaleta uzi wa uongo tukuangalie tuu
Mkuu, nasikitika kukuambia kuwa hujui chochote kuhusu jambo hili nililolizungumzia. Tafuta Kanuni na uzifahamu. Usilazimishe kubisha wakati huna hoja ya maana.
 
Ili kutokuleta mgawanyiko, makonda apitishwe kugombea Buchosa, Dr tizeba aende sumve, na shigongo aende Kibamba. Mwanry apelekwe Kawe
Ili iweje sasa??CCM hawafanyi mambo ya hovyo to that extent, ulipogombea ndipo unanafasi ya kurudishwa na sio kuhamishwa ukagombee sehemu nyingine huko unapoenda kwengine utaenda kumuomba kura mwanaCCM gani wakati hawakutambui?
 
Ili iweje sasa??CCM hawafanyi mambo ya hovyo to that extent, ulipogombea ndipo unanafasi ya kurudishwa na sio kuhamishwa ukagombee sehemu nyingine huko unapoenda kwengine utaenda kumuomba kura mwanaCCM gani wakati hawakutambui?
Tusifanye Mambo kwa mazoea, mgombea akipewa bendera anakuwa wa chama ndio kitakacho mnadi, Sasa hivi kinachoendelea nimapendekezo tu
 
Kwenye hili la kamati kuu kupitisha wagombea watakaosimama kwenye majimbo, kuna watu watalia na kusaga meno


Inategemea nimeamkaje
 
Tusifanye Mambo kwa mazoea, mgombea akipewa bendera anakuwa wa chama ndio kitakacho mnadi, Sasa hivi kinachoendelea nimapendekezo tu
sasa utampeleka sehemu ambayo hakubaliki braza vipi??hajagombea hilo eneo kwasababu anajua hana ushawishi eneo husika.
 
Mkuu, wakati ule majina matatu ya kupigiwa kura yalitokea Kamati Kuu halafu yakapigiwa kura na kurejea huko. Kwasasa, wote waliotia nia wamepigiwa kura kwanza kabla ya kupelekwa Kamati Kuu kwa maamuzi. Huo ndiyo upya. Tena, wakati ule wanachama wote wa CCM jimboni walipiga kura. Kwasasa ni Kamati ya Jimbo tu ndiyo iliyopiga kura. Kanuni zimebadilika.
Well said uko vizuri mkuu
 
Kuna kipengele kimeongezwa kinasema "maamuzi ya nani atakua mgombea kupitia ccm yatategemea pia jinsi mwenyekiti wa chama taifa alivyoamka siku hiyo ya maamuzi"
Atakavyoamka siku hiyo hajasema kuwa atahamisha mtu kutoka kusini akagombee kaskazini. Na kanuni za chama zipo wazi kuwa majina matatu ndio yataenda kamati kuu kujadiliwa, washindi watatu wa mwanzo.
 
Watu mnakuwa wa ajabu,Magu angetaka apite angepita Kigamboni,huko kapigwa chini na kamati itampiga chini
Kigamboni angempitishaje wakati kila mjumbe anapiga kura ya siri? Una maana wajumbe karibia 400,angawalazimiza wampigie makonda kura?!! Huko kwenye kamati kuu inakuwa rahisi kama ataamua, kwakuwa atakuwa ndio kiongozi, na kule hawapigi kura, wanatumia vigezo vyao tu, kumbeba mgombea kulingana na matakwa yao! Na akilazimisha sana ndipo hutokea jimbo kupotea
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom