Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,316
- 33,125
Ni kwanini ini ni muhimu?
Ini ni ogani ya pili kubwa zaidi katika mwili wako na inapatikana chini ya kizimba cha mbavu kwenye upande wa kulia. Ina uzani wa kama pauni tatu na umbo lake ni kama mpira wa soka ambao umelala upande mmoja.
Ini hufanya kazi nyingi katika mwili wako. Huwa inachakata kile unachokula na kunywa kuwa nguvu na virutubishi ambavyo mwili wako unaweza kutumia. Ini pia hutoa vitu vyinavyoweza kukudhuru kutoka kwa damu yako.
Saratani ya ini ni nini?
Saratani ya ini ni kukua na usambazaji wa seli zisizo na afya kwenye ini. Saratani ambayo huanza kwenye ini ni saratani ya kimsingi ya ini. Saratani ambayo inasambaa kwa ini kutoka kwa ogani nyingine ni saratani enezi ya ini.
Karibu Waamerika 21,000 wanapatikana na saratani ya kimsingi ya ini kila mwaka. Saratani ya kimsingi ya ini ni moja ya saratani chache zinazoongezeka huko Amerika. Saratani ya kimsingi ni kama mara mbili zaidi kwa wanaume kuliko wanawake.
Saratani ya ini inasababishwa na nini?
Kuna hatari kadhaa za saratani ya ini.
Cirrhosis (vidonda kwenye ini) inaweza kusababisha saratani ya ini. Huko Amerika, unywaji pombe kupindukia na Homa ya Virusi ndio chanzo kubwa za cirrhosis.
Uambukizaji wa muda mrefu wa Homa ya Maini na Homa ya Virusi unahusishwa na saratani ya ini kwa sababu mara nyingi husababisha ugonjwa wa cirrhosis. Homa ya Maini inaweza kusababisha saratani ya ini bila cirrhosis.
Ugonjwa wa kunona sana huongeza hatari ya kupata saratani ya ini.
Ugonjwa wa sukari unaweza kuongeza hatari ya saratani ya ini, haswa kwa wale ambao hunywa pombe sana au wanayo virusi vingi vya hepatisis.
Dalili za saratani ya ini ni nini?
Mara nyingi hakuna dalili za saratani ya ini hadi ugonjwa uwe katika kiwango cha juu zaidi. Wakati dalili zinatokea, zinaweza kuwa pamoja na, kufura tumbo, uchungu katika upande wa tumbo ya juu au mgongo na mabega, kichefuchefu, kupoteza hamu ya chakula, hisia za kushiba, upotezaji wa uzani, udhaifu, homa ya nyongo ya manjano (macho na ngozi kuwa manjano).
Je! saratani ya ini inagunduliwa vipi?
Saratani ya ini inagunduliwa kwa uchunguzi wa kimwili au kwa uchunguzi wa picha. Ili kudhibitisha uchunguzi wa saratani ya ini, madaktari hutumia upimaji damu, vipimo vya maabara, uchunguzi wa tomografia ya kompyuta (CT), uchunguzi wa picha za sumaku (MRI), na
andiogramu. Daktari wako pia anaweza kuhitaji uchunguzi wa giligili na tishu za kusababisha ugonjwa (biopsy). Wakati wa kuchunguza giligili, kipande kidogo cha tishu ya ini hutolewa na kuchunguzwa katika maabara.
Ini ni ogani ya pili kubwa zaidi katika mwili wako na inapatikana chini ya kizimba cha mbavu kwenye upande wa kulia. Ina uzani wa kama pauni tatu na umbo lake ni kama mpira wa soka ambao umelala upande mmoja.
Ini hufanya kazi nyingi katika mwili wako. Huwa inachakata kile unachokula na kunywa kuwa nguvu na virutubishi ambavyo mwili wako unaweza kutumia. Ini pia hutoa vitu vyinavyoweza kukudhuru kutoka kwa damu yako.
Saratani ya ini ni nini?
Saratani ya ini ni kukua na usambazaji wa seli zisizo na afya kwenye ini. Saratani ambayo huanza kwenye ini ni saratani ya kimsingi ya ini. Saratani ambayo inasambaa kwa ini kutoka kwa ogani nyingine ni saratani enezi ya ini.
Karibu Waamerika 21,000 wanapatikana na saratani ya kimsingi ya ini kila mwaka. Saratani ya kimsingi ya ini ni moja ya saratani chache zinazoongezeka huko Amerika. Saratani ya kimsingi ni kama mara mbili zaidi kwa wanaume kuliko wanawake.
Saratani ya ini inasababishwa na nini?
Kuna hatari kadhaa za saratani ya ini.
Cirrhosis (vidonda kwenye ini) inaweza kusababisha saratani ya ini. Huko Amerika, unywaji pombe kupindukia na Homa ya Virusi ndio chanzo kubwa za cirrhosis.
Uambukizaji wa muda mrefu wa Homa ya Maini na Homa ya Virusi unahusishwa na saratani ya ini kwa sababu mara nyingi husababisha ugonjwa wa cirrhosis. Homa ya Maini inaweza kusababisha saratani ya ini bila cirrhosis.
Ugonjwa wa kunona sana huongeza hatari ya kupata saratani ya ini.
Ugonjwa wa sukari unaweza kuongeza hatari ya saratani ya ini, haswa kwa wale ambao hunywa pombe sana au wanayo virusi vingi vya hepatisis.
Dalili za saratani ya ini ni nini?
Mara nyingi hakuna dalili za saratani ya ini hadi ugonjwa uwe katika kiwango cha juu zaidi. Wakati dalili zinatokea, zinaweza kuwa pamoja na, kufura tumbo, uchungu katika upande wa tumbo ya juu au mgongo na mabega, kichefuchefu, kupoteza hamu ya chakula, hisia za kushiba, upotezaji wa uzani, udhaifu, homa ya nyongo ya manjano (macho na ngozi kuwa manjano).
Je! saratani ya ini inagunduliwa vipi?
Saratani ya ini inagunduliwa kwa uchunguzi wa kimwili au kwa uchunguzi wa picha. Ili kudhibitisha uchunguzi wa saratani ya ini, madaktari hutumia upimaji damu, vipimo vya maabara, uchunguzi wa tomografia ya kompyuta (CT), uchunguzi wa picha za sumaku (MRI), na
andiogramu. Daktari wako pia anaweza kuhitaji uchunguzi wa giligili na tishu za kusababisha ugonjwa (biopsy). Wakati wa kuchunguza giligili, kipande kidogo cha tishu ya ini hutolewa na kuchunguzwa katika maabara.