habari ya hapa
JF-Expert Member
- Dec 20, 2012
- 12,791
- 8,739
Nipo nae yapata 2yrs na miez kadhaa, huyu binadamu ameoa na anawatoto wa 2, tumefanya vitu vingi vya maendeleo ikiwa ni pamoja na kufungua kampuni na baadhi ya miradi mingine midogo midogo, aliamua kushirikiana nami baada ya kuona mkewe kila akimfungulia biashara inakufa na akitafutiwa kazi miezi 2 tu anashindwa na kurudi nyumbani.
Kuna baadhi ya miradi tumeshare na mingine kila mtu kasajili kwa jina lake hakuna siku tumegombana ila kuna kupishana kauli tu mara moja moja. Jana kuna document nilimpelekea ofisi kwake nilipofika nikaongea na secretary km anaweza kuniruhusu niingea ndani akanambia anawatu, baadae secretary alioona wageni wake wametoka akaniruhusu nikaingia.
Nilipoingia kule ndani ghafla simu yangu ikaita, nilipokea na kuaza kusema na aliyenipigia ghafla mwenzangu akanipokonya ile simu na kupigiza chini na kuivunja vunja, akaninyang'anya mkoba wangu akachukua na simu nyingine akaibonda bonda, kibaya zaidi na laini akaziharibu kabisa, kulitokea ugomvi bahati yangu kulikuwa na watu wengine, me ikabidi nitoke na kuondoka, sikulala nyumbani kwangu kuogopa angeweza kuja usiku.
Nimeumia sana kwa hili tukio kwani angehoji kwanza hata angetaka nimpe namba ya niliyekuwa naongea nae ningempa kuliko hiv alivyofanya, sjaelewa hadi sasa nini hiki!!
Mawazo yenu tafadhali
Kuna baadhi ya miradi tumeshare na mingine kila mtu kasajili kwa jina lake hakuna siku tumegombana ila kuna kupishana kauli tu mara moja moja. Jana kuna document nilimpelekea ofisi kwake nilipofika nikaongea na secretary km anaweza kuniruhusu niingea ndani akanambia anawatu, baadae secretary alioona wageni wake wametoka akaniruhusu nikaingia.
Nilipoingia kule ndani ghafla simu yangu ikaita, nilipokea na kuaza kusema na aliyenipigia ghafla mwenzangu akanipokonya ile simu na kupigiza chini na kuivunja vunja, akaninyang'anya mkoba wangu akachukua na simu nyingine akaibonda bonda, kibaya zaidi na laini akaziharibu kabisa, kulitokea ugomvi bahati yangu kulikuwa na watu wengine, me ikabidi nitoke na kuondoka, sikulala nyumbani kwangu kuogopa angeweza kuja usiku.
Nimeumia sana kwa hili tukio kwani angehoji kwanza hata angetaka nimpe namba ya niliyekuwa naongea nae ningempa kuliko hiv alivyofanya, sjaelewa hadi sasa nini hiki!!
Mawazo yenu tafadhali