sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,408
- 19,026
Kuwa mkweli ni jambo la kheri nami nimeamua kuwa muwazi juu ya maisha yangu.
Mimi ni kijana ambae kwa sasa najitegemea, nimeoa na nina watoto wawili, kwa sasa naishi kwa mshahara wa serikalini na biashara yangu ndogo.
Tangu udogoni nilikuwa mdau mkubwa tu wa kwenda kanisani na wazazi walihakikisha na kusisitiza tuwe tunaenda kanisani, nilijifunza mengi ambayo yalisaidia tabia na mwenendo wangu wa maisha uwe mwema maana nilijifunza vitu kama nisiibe, nisiue, nisisingizie, nisiwe na dharau, nisake maarifa / elimu, nisaidie wasiojiweza, n.k.
IIla wakati nikizidi kukuwa nimiliyaona mengi katika matukio mbali mbali kwa watu niliowajua tunaoenda nao kanisani na wengine wanaoenda misikitini niliweza kuwashuhudia wanarudi katika tiba asili (tiba sio uchawi) walipopatwa matatizo hasa ya mda mredu yalienda kutatuliwa kwa mtaalam japo sio yote yalitatulika. Nkumbuka kuna mtoto alizaliwa vizuri tu hadi kafikia miaka minne hana tatizo ghafla akawa haongei wala kusikia, wazazi walizunguka mahospitalini na makanisani ila wapi, ikabidi tu waende kwa mtaalam tatizo likatatulika maana kuna wabaya walimteka mtoto kiroho.
Tatizo lengine ni kaka yangu alikuwa mbabe hivi sasa akazinguana enzi hizo sekondari na mwenzake wa darasani kwa kumuibia demu kwa ubabe, muda si muda kaka yangu akawa hawezi kukaa kwenye mwanga hata kidogo huko nje akawa anakaa ndani tu analalamika jua linamuumiza macho, kwenda kwa madaktari akapewa dawa nyingi za aina tofauti kwa miezi miwili ila hakuna dalili, kwenda kanisani nako hakuna kitu na mbaya zaidi kaka yangu niseme ukweli tu enzi hizo sijui kama aliujua hata mstari moja wa biblia, Basi ikabidi ifungwe safari aende kutibiwa kwa njia asili tulimpeleka akabaki huko wiki hivi akarudi yupo fresh, ikabaki stori.
Binafsi mimi kuna kipindi nilienda kusoma shule moja hivi (jina kapuni) nikiwa form 3 siku moja naenda chooni usiku nikakutana na kibwengo kijamaa kifupi kama kina kingora kichwani nilitoka nduki balaa kurudi bwenini, shule hio wengi walisumbuliwa na hivi viumbe, siku nyingine tena hivyo hivyo ikanitokea nikiwa form 4 tena mara mbili, ikabidi nipelekwe kwa mtaalam wa eneo hilo mwenye uzoefu na hivyo viumbe basi tullienda kama wanne hivi tukafukizwa mitishamba na tangu siku hio sijui habari za hivyo vibwengo.
Tukio lingine nilipanga huko uswazi nikiwa chuo kwasababu ya uhaba wa pesa basi kuna wiki flani ilikuwa ya mateso sana kwangu, siku za mwanzo nlikuwa nahisi kuna mtu anatembea juu ya dari, ikaendelea na siku ya pili, siku ya tatu ni kama mtu anamwaga mchanga juu ya bati nilikemea sana wakaondoka , baada ya siku mbili asubuhi naamka nina chale kwenye mkono wa kushoto, duuuh!!! nikaona nirudi tu kwetu siku hio hio nikaenda kutibiwa huko nakumbuka waliniambia tu kuna madhara ningepata.
Basi nikafutwa hizo chale na nikachanganiwa miti shamba flani na kinyesi cha nguruwe nikaambiwa nirudi na hico kitu nikiweke darini siku si nyingi ntapata matokeo na kikiyapata nihame, niliuliza matokeo yapi lakini nikaambiwa ntayaona tu, basi nimerudi huko geto nikafanya nlichoambiwa usiku ule nilila bila bugudha nlizozoea ila usiku wa siku ya pili kitu kizito sana kilidondoka kwenye bati usiku wa maanae "PUUUHH!!!
Aisee kila mpangaji alitoka ndani mwake kuangalia ni nini kimedondoka ila cha ajabu hatukuweza kuona, siku 3 mfululizo niligundua kitu tofauti maana mama mwenye nyumba hakuwa akitoka kuotea jua wala kufua nguo, sasa mi nikajua huyo ndio alikuwa jangiri, siku ya nne nilihama na kuchoma dawa nliyopewa, nliaga wapangaji wenzangu tu mama mwenye nyumba hata sikutaka kumuona.
Ni matukio mengi sana tu ambayo kiukweli wengine amam mimi nimeyatatua kwa njia za asili, naweza kuitwa mshirikina lakini kumbe si kweli, nachofanya ni kutatua matatizo kwa njia walizotumia babau zangu enzi toka enzi maana matatizo mengi yalianza hata kabla ya ukoloni na mpaka leo yapo.
Mwisho kabisa napenda tu niwaambie kuna waganga matapeli kibao sana, kwa ushauri nakuomba utafute chifu wa kabila lako au sehemu unayoishi, utaelekezwa kwa mtaalam ambae kizazi chake toka mababu ndio fani yao, usiende kwa wataalam hawa wanaojitangaza mitandaoni, utatapeliwa na wanaweza kukujengea chuki na ndugu zako au familia
Ni hayo tu ndugu zangu.
Mimi ni kijana ambae kwa sasa najitegemea, nimeoa na nina watoto wawili, kwa sasa naishi kwa mshahara wa serikalini na biashara yangu ndogo.
Tangu udogoni nilikuwa mdau mkubwa tu wa kwenda kanisani na wazazi walihakikisha na kusisitiza tuwe tunaenda kanisani, nilijifunza mengi ambayo yalisaidia tabia na mwenendo wangu wa maisha uwe mwema maana nilijifunza vitu kama nisiibe, nisiue, nisisingizie, nisiwe na dharau, nisake maarifa / elimu, nisaidie wasiojiweza, n.k.
IIla wakati nikizidi kukuwa nimiliyaona mengi katika matukio mbali mbali kwa watu niliowajua tunaoenda nao kanisani na wengine wanaoenda misikitini niliweza kuwashuhudia wanarudi katika tiba asili (tiba sio uchawi) walipopatwa matatizo hasa ya mda mredu yalienda kutatuliwa kwa mtaalam japo sio yote yalitatulika. Nkumbuka kuna mtoto alizaliwa vizuri tu hadi kafikia miaka minne hana tatizo ghafla akawa haongei wala kusikia, wazazi walizunguka mahospitalini na makanisani ila wapi, ikabidi tu waende kwa mtaalam tatizo likatatulika maana kuna wabaya walimteka mtoto kiroho.
Tatizo lengine ni kaka yangu alikuwa mbabe hivi sasa akazinguana enzi hizo sekondari na mwenzake wa darasani kwa kumuibia demu kwa ubabe, muda si muda kaka yangu akawa hawezi kukaa kwenye mwanga hata kidogo huko nje akawa anakaa ndani tu analalamika jua linamuumiza macho, kwenda kwa madaktari akapewa dawa nyingi za aina tofauti kwa miezi miwili ila hakuna dalili, kwenda kanisani nako hakuna kitu na mbaya zaidi kaka yangu niseme ukweli tu enzi hizo sijui kama aliujua hata mstari moja wa biblia, Basi ikabidi ifungwe safari aende kutibiwa kwa njia asili tulimpeleka akabaki huko wiki hivi akarudi yupo fresh, ikabaki stori.
Binafsi mimi kuna kipindi nilienda kusoma shule moja hivi (jina kapuni) nikiwa form 3 siku moja naenda chooni usiku nikakutana na kibwengo kijamaa kifupi kama kina kingora kichwani nilitoka nduki balaa kurudi bwenini, shule hio wengi walisumbuliwa na hivi viumbe, siku nyingine tena hivyo hivyo ikanitokea nikiwa form 4 tena mara mbili, ikabidi nipelekwe kwa mtaalam wa eneo hilo mwenye uzoefu na hivyo viumbe basi tullienda kama wanne hivi tukafukizwa mitishamba na tangu siku hio sijui habari za hivyo vibwengo.
Tukio lingine nilipanga huko uswazi nikiwa chuo kwasababu ya uhaba wa pesa basi kuna wiki flani ilikuwa ya mateso sana kwangu, siku za mwanzo nlikuwa nahisi kuna mtu anatembea juu ya dari, ikaendelea na siku ya pili, siku ya tatu ni kama mtu anamwaga mchanga juu ya bati nilikemea sana wakaondoka , baada ya siku mbili asubuhi naamka nina chale kwenye mkono wa kushoto, duuuh!!! nikaona nirudi tu kwetu siku hio hio nikaenda kutibiwa huko nakumbuka waliniambia tu kuna madhara ningepata.
Basi nikafutwa hizo chale na nikachanganiwa miti shamba flani na kinyesi cha nguruwe nikaambiwa nirudi na hico kitu nikiweke darini siku si nyingi ntapata matokeo na kikiyapata nihame, niliuliza matokeo yapi lakini nikaambiwa ntayaona tu, basi nimerudi huko geto nikafanya nlichoambiwa usiku ule nilila bila bugudha nlizozoea ila usiku wa siku ya pili kitu kizito sana kilidondoka kwenye bati usiku wa maanae "PUUUHH!!!
Aisee kila mpangaji alitoka ndani mwake kuangalia ni nini kimedondoka ila cha ajabu hatukuweza kuona, siku 3 mfululizo niligundua kitu tofauti maana mama mwenye nyumba hakuwa akitoka kuotea jua wala kufua nguo, sasa mi nikajua huyo ndio alikuwa jangiri, siku ya nne nilihama na kuchoma dawa nliyopewa, nliaga wapangaji wenzangu tu mama mwenye nyumba hata sikutaka kumuona.
Ni matukio mengi sana tu ambayo kiukweli wengine amam mimi nimeyatatua kwa njia za asili, naweza kuitwa mshirikina lakini kumbe si kweli, nachofanya ni kutatua matatizo kwa njia walizotumia babau zangu enzi toka enzi maana matatizo mengi yalianza hata kabla ya ukoloni na mpaka leo yapo.
Mwisho kabisa napenda tu niwaambie kuna waganga matapeli kibao sana, kwa ushauri nakuomba utafute chifu wa kabila lako au sehemu unayoishi, utaelekezwa kwa mtaalam ambae kizazi chake toka mababu ndio fani yao, usiende kwa wataalam hawa wanaojitangaza mitandaoni, utatapeliwa na wanaweza kukujengea chuki na ndugu zako au familia
Ni hayo tu ndugu zangu.