Kanisa Katoliki lawatenga wanachama 400 wa CCM

kilimasera

JF-Expert Member
Dec 2, 2009
3,068
268
KATIKA kile kinachoonekana kuithibitishia jamii kuwa nyumba za ibada si mahala pa siasa, Kanisa Katoliki Jimbo la Sumbawanga limewafukuza na kuwazuia kushiriki shughuli za kanisa zaidi ya waumini wake 400 wanaotuhumiwa kuisaliti imani ya kanisa hilo kwa kukishabikia Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu uliofanyika hivi karibuni.

Miongoni mwa waumini wanaotajwa kuwa wamesimamishwa na kanisa hilo ni pamoja na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Rukwa, Hipolitus Matete na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Sumbawanga, Charles Kabanga.

Habari za uhakika ambazo HABARILEO Jumapili imezipata zinasema kwamba, uamuzi huo wa kanisa umelenga kujisafisha na 'kashfa’ ya kuegemea upande fulani wakati wa kampeni na baadaye uchaguzi mkuu wa Oktoba 31, mwaka huu.

Chanzo chetu cha habari kimepasha kwamba, wanaCCM hao wanaotuhumiwa na kanisa hilo wanahusika kufanya mikutano ya ndani, kuvaa sare za chama hicho na kumshabikia waziwazi aliyekuwa mgombea wa Ubunge kupitia CCM katika Jimbo la Sumbawanga Mjini,
Aeshi Hilaly.

Kwenye kinyang'anyiro cha uchaguzi mkuu huo mgombea ubunge wa CCM, Aeshi aliibuka kidedea kwa kutangazwa mshindi dhidi ya mgombea wa Chadema, Norbet Yamsebo ambaye kwa sasa amekata rufaa Mahakama Kuu mjini hapa kupinga matokeo hayo.

Inaelezwa kwamba, mgogoro wa kiimani baina ya Kanisa Katoliki Jimbo la Sumbawanga Mjini na waumini wake ambao ni wanaCCM, umetokana na waumini hao kupuuzia agizo la kanisa la kutomshabikia Aeshi kwa madai kwamba, alikufuru imani ya kanisa hilo kwa kujifananisha na Mwana wa Mungu, Yesu Kristu.

Baadhi ya viongozi wa kanisa jimboni humo wamekuwa wakimtuhumu mgombea huyo wa CCM pale alipodai katika moja ya mikutano yake ya kampeni kwa kufananisha mafiga matatu na Utatu Mtakatifu ambao mgombea huyo anadai kuwa alikufuru imani hiyo kwa kumfananisha mgombea Urais wa CCM, Rais Jakaya Kikwete kama Mungu Baba, mgombea ubunge kama Yesu Kristu mwana wa Mungu na wagombea Udiwani sawa na
Roho Mtakatifu.

Katibu wa CCM Mkoa wa Rukwa, Kapteni Fratern Kiwango amethibitisha kutengwa kwa wanachama wa chama hicho ambao ni waumini wa Kanisa Katoliki Jimbo la Sumbawanga.

“Ni kweli hadi sasa kanisa hilo limewafukuza na kuwazuia wanaCCM zaidi ya 400 kupokea sakramenti zozote kwenye Kanisa Katoliki la hapa,” alisema Kapteni Kiwango aliyewataja baadhi ya waliofukuzwa na kusimamishwa kuhudhuria ibada za misa takatifu kuwa ni pamoja na Matete, Kabanga, dereva wa Katibu wa CCM mkoa wa Rukwa aitwaye Vitalis Kalwangwa na mkewe na Katibu Mwenezi wa CCM Tawi la Majengo, Christina Tinde.

Inadaiwa kuwa waumini hao ni kutoka kanisa la Familia Takatifu lililopo Chanji mengine ni Kristu Mfalme , Katandala na Kanisa la Kiaskofu lililopo Mazwi mjini hapa ambapo kanisa lililopo kijiji cha Mlanda limefungwa na waumini wake wote wamezuiwa kupata
huduma yoyote ya kiroho kwenye kanisa hilo.

Inadaiwa kuwa pamoja na kuzuiwa kuingia makanisani na kuhudhuria ibada ya misa takatifu waumini hao wamezuiwa pia kupokea sakramenti zozote katika Kanisa Katoliki.

Pia wamezuiwa kupata huduma za kiroho kanisani zikiwemo kufunga ndoa, kubatizwa au kupata kipaimara na pia kufanyiwa ibada wakati wa maziko hadi hapo suala lao litakapopatiwa ufumbuzi ambapo itategemewa zaidi jitihada zao binafsi na huruma ya Mungu.

Mwandishi wa habari hizi alisoma baadhi ya nakala za barua za kuwasimamisha kupokea sakramenti kwenye kanisa hilo zilizosainiwa na Paroko wa Kanisa la Kristu Mfalme, Padri Pambo Mlongwa.

Sehemu ya barua hiyo inasema; "Kufuatia mwenendo mbovu wakati wa uchaguzi mkuu, huku ukiendekeza vitendo vya rushwa na usaliti wa imani Katoliki.

“Kwa heshima ya Mungu wetu na utatu mtakatifu wa kanisa, Mama kanisa Mtakatifu kwa nguvu ya Sheria ya kanisa CIC 13669, CIC1389,CIC 13712 na CIC 1391 naagiza usipokee sakramenti zozote katika Kanisa Katoliki… tekeleza amri hii mara umalizapo kuisoma barua hii.”

Padri Pambo alipohojiwa kwa njia ya simu ili kupata ufafanuzi zaidi wa suala hilo alisema kwamba, yuko mbali sana ambako hataki mtu yeyoye ajue aliko.

"Sawa mimi ni kiongozi wa kiroho kwa sasa sitaki kabisa mtu yeyote hata wewe ujue wapi nilipo, niko mbali sana kwa sasa nakushauri nenda ofisini ni suala la kiofisi hilo kwa sasa sina majibu yake,” alisema kiongozi huyo wa kiroho.

Lakini kabla ya mawasiliano ya siku hiyo, kwa nyakati tofauti Padri Pambo alipokuwa
akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu alikiri kuwa mgombea wa CCM, Aeshi alikuwa amekufuru imani na Kanisa Katoliki kwa kujifananisha na Yesu Kristu Mungu Mwana ambapo Kanisa liliwasilisha malalamiko yake kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alipokuja mjini hapa kumnadi mgombea huyo, lakini hawakuweza kufikia mwafaka.

Pia zimekuwa taarifa mjini hapa kwa Padri Pambo amekimbia kanisa lake la Kristu Mfalme kwa kile kinachodaiwa kuwa amekwenda kujificha kusikojulikana ili kukwepa hasira za waumini wa kanisa hilo wanaopinga kufukuzwa kwa wenzao kwa sababu ya itikadi zao za kisiasa.

Naye Paroko wa Kanisa la Kiaskofu mjini Sumbawanga, Padri Deo Simemba hivi karibuni alipohojiwa na gazeti hili alikiri kuwa kanisa limeanza kuwasimamisha baadhi ya waumini wake kwa kile alichodai kuisaliti imani ya Kanisa Katoliki.

Kutokana na tukio hilo, Katibu wa CCM wa Mkoa amelitahadharisha kanisa hilo kwa kujiingiza kwenye malumbano ya kisiasa.

Baadaye, gazeti hili liliwasiliana na Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Padri Anthony Makunde ili aweze kulizungumzia suala hilo na alipopatikana kwa njia ya simu alisema:

“Kwa nafasi yangu, naweza kusema sijui lolote kwa sababu sijapata taarifa rasmi na inawezekana kwa kuwa katika siku za hivi karibuni nilikuwa na vikao vingi pamoja na kuhudhuria mafahali pale Chuo Kikuu cha Madaktari Bugando (Mwanza).”
 
Kama imethibitishwa walikufuru imani ya kanisa hilo, kelele za nini?
Sidhani kama suala ni uanachama wa ccm, bali ni hiyo ya kujifananisha na Mungu.
 
Habari haijielezi inamaanisha nini!
Kama sababu ingekuwa ni kusimamishwa kwa sababu kanisa lilimtaka mtu flani na hao waumini wakakaidi sawa, lakini kama ni kwa kujifananisha na Kristo sioni tatizo kwa msimamo huo wa kanisa.
 
Kama kweli hao jamaa wa ccm walijiita Utatu Mtakatifu, basi ni kweli wamekufuru, tena sana tu. Na kosa la kufuru katika kanisa katoliki linaadhibiwa kwa kutengwa. Hapo hakuna cha siasa wala nini! Ni suala la imani. Wakubali kwamba walikosea na waombe msamaha. Kanisa litawasamehe. Lakini wakiingiza siasa katika mambo ya imani wajue kwamba wanapoteza muda, waanze labda kutafuta pa kwenda.
 
KATIKA kile kinachoonekana kuithibitishia jamii kuwa nyumba za ibada si mahala pa siasa, Kanisa Katoliki Jimbo la Sumbawanga limewafukuza na kuwazuia kushiriki shughuli za kanisa zaidi ya waumini wake 400 wanaotuhumiwa kuisaliti imani ya kanisa hilo kwa kukishabikia Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu uliofanyika hivi karibuni.

Miongoni mwa waumini wanaotajwa kuwa wamesimamishwa na kanisa hilo ni pamoja na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Rukwa, Hipolitus Matete na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Sumbawanga, Charles Kabanga.

Habari za uhakika ambazo HABARILEO Jumapili imezipata zinasema kwamba, uamuzi huo wa kanisa umelenga kujisafisha na 'kashfa' ya kuegemea upande fulani wakati wa kampeni na baadaye uchaguzi mkuu wa Oktoba 31, mwaka huu.

Chanzo chetu cha habari kimepasha kwamba, wanaCCM hao wanaotuhumiwa na kanisa hilo wanahusika kufanya mikutano ya ndani, kuvaa sare za chama hicho na kumshabikia waziwazi aliyekuwa mgombea wa Ubunge kupitia CCM katika Jimbo la Sumbawanga Mjini,
Aeshi Hilaly.

Kwenye kinyang'anyiro cha uchaguzi mkuu huo mgombea ubunge wa CCM, Aeshi aliibuka kidedea kwa kutangazwa mshindi dhidi ya mgombea wa Chadema, Norbet Yamsebo ambaye kwa sasa amekata rufaa Mahakama Kuu mjini hapa kupinga matokeo hayo.

Inaelezwa kwamba, mgogoro wa kiimani baina ya Kanisa Katoliki Jimbo la Sumbawanga Mjini na waumini wake ambao ni wanaCCM, umetokana na waumini hao kupuuzia agizo la kanisa la kutomshabikia Aeshi kwa madai kwamba, alikufuru imani ya kanisa hilo kwa kujifananisha na Mwana wa Mungu, Yesu Kristu.

Baadhi ya viongozi wa kanisa jimboni humo wamekuwa wakimtuhumu mgombea huyo wa CCM pale alipodai katika moja ya mikutano yake ya kampeni kwa kufananisha mafiga matatu na Utatu Mtakatifu ambao mgombea huyo anadai kuwa alikufuru imani hiyo kwa kumfananisha mgombea Urais wa CCM, Rais Jakaya Kikwete kama Mungu Baba, mgombea ubunge kama Yesu Kristu mwana wa Mungu na wagombea Udiwani sawa na
Roho Mtakatifu.

Katibu wa CCM Mkoa wa Rukwa, Kapteni Fratern Kiwango amethibitisha kutengwa kwa wanachama wa chama hicho ambao ni waumini wa Kanisa Katoliki Jimbo la Sumbawanga.

"Ni kweli hadi sasa kanisa hilo limewafukuza na kuwazuia wanaCCM zaidi ya 400 kupokea sakramenti zozote kwenye Kanisa Katoliki la hapa," alisema Kapteni Kiwango aliyewataja baadhi ya waliofukuzwa na kusimamishwa kuhudhuria ibada za misa takatifu kuwa ni pamoja na Matete, Kabanga, dereva wa Katibu wa CCM mkoa wa Rukwa aitwaye Vitalis Kalwangwa na mkewe na Katibu Mwenezi wa CCM Tawi la Majengo, Christina Tinde.

Inadaiwa kuwa waumini hao ni kutoka kanisa la Familia Takatifu lililopo Chanji mengine ni Kristu Mfalme , Katandala na Kanisa la Kiaskofu lililopo Mazwi mjini hapa ambapo kanisa lililopo kijiji cha Mlanda limefungwa na waumini wake wote wamezuiwa kupata
huduma yoyote ya kiroho kwenye kanisa hilo.

Inadaiwa kuwa pamoja na kuzuiwa kuingia makanisani na kuhudhuria ibada ya misa takatifu waumini hao wamezuiwa pia kupokea sakramenti zozote katika Kanisa Katoliki.

Pia wamezuiwa kupata huduma za kiroho kanisani zikiwemo kufunga ndoa, kubatizwa au kupata kipaimara na pia kufanyiwa ibada wakati wa maziko hadi hapo suala lao litakapopatiwa ufumbuzi ambapo itategemewa zaidi jitihada zao binafsi na huruma ya Mungu.

Mwandishi wa habari hizi alisoma baadhi ya nakala za barua za kuwasimamisha kupokea sakramenti kwenye kanisa hilo zilizosainiwa na Paroko wa Kanisa la Kristu Mfalme, Padri Pambo Mlongwa.

Sehemu ya barua hiyo inasema; "Kufuatia mwenendo mbovu wakati wa uchaguzi mkuu, huku ukiendekeza vitendo vya rushwa na usaliti wa imani Katoliki.

"Kwa heshima ya Mungu wetu na utatu mtakatifu wa kanisa, Mama kanisa Mtakatifu kwa nguvu ya Sheria ya kanisa CIC 13669, CIC1389,CIC 13712 na CIC 1391 naagiza usipokee sakramenti zozote katika Kanisa Katoliki… tekeleza amri hii mara umalizapo kuisoma barua hii."

Padri Pambo alipohojiwa kwa njia ya simu ili kupata ufafanuzi zaidi wa suala hilo alisema kwamba, yuko mbali sana ambako hataki mtu yeyoye ajue aliko.

"Sawa mimi ni kiongozi wa kiroho kwa sasa sitaki kabisa mtu yeyote hata wewe ujue wapi nilipo, niko mbali sana kwa sasa nakushauri nenda ofisini ni suala la kiofisi hilo kwa sasa sina majibu yake," alisema kiongozi huyo wa kiroho.

Lakini kabla ya mawasiliano ya siku hiyo, kwa nyakati tofauti Padri Pambo alipokuwa
akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu alikiri kuwa mgombea wa CCM, Aeshi alikuwa amekufuru imani na Kanisa Katoliki kwa kujifananisha na Yesu Kristu Mungu Mwana ambapo Kanisa liliwasilisha malalamiko yake kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alipokuja mjini hapa kumnadi mgombea huyo, lakini hawakuweza kufikia mwafaka.

Pia zimekuwa taarifa mjini hapa kwa Padri Pambo amekimbia kanisa lake la Kristu Mfalme kwa kile kinachodaiwa kuwa amekwenda kujificha kusikojulikana ili kukwepa hasira za waumini wa kanisa hilo wanaopinga kufukuzwa kwa wenzao kwa sababu ya itikadi zao za kisiasa.

Naye Paroko wa Kanisa la Kiaskofu mjini Sumbawanga, Padri Deo Simemba hivi karibuni alipohojiwa na gazeti hili alikiri kuwa kanisa limeanza kuwasimamisha baadhi ya waumini wake kwa kile alichodai kuisaliti imani ya Kanisa Katoliki.

Kutokana na tukio hilo, Katibu wa CCM wa Mkoa amelitahadharisha kanisa hilo kwa kujiingiza kwenye malumbano ya kisiasa.

Baadaye, gazeti hili liliwasiliana na Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Padri Anthony Makunde ili aweze kulizungumzia suala hilo na alipopatikana kwa njia ya simu alisema:

"Kwa nafasi yangu, naweza kusema sijui lolote kwa sababu sijapata taarifa rasmi na inawezekana kwa kuwa katika siku za hivi karibuni nilikuwa na vikao vingi pamoja na kuhudhuria mafahali pale Chuo Kikuu cha Madaktari Bugando (Mwanza)."

Kichwa cha habari kinaonekana kuwa na ujumbe kana kwamba 'waliotengwa', walifanyiwa hivyo simply kwa vile ni wana-CCM. Na nadhani editor aliyeweka kichwa hiki cha habari alitaka wasomaji wajenge imani kuwa Kanisa Katoliki linawatenga waumini wake kwa vile wamechagua CCM au kwa kuwa wana-CCM.
 
Sasa najiuliza kanisa lilikuwa wapi wakati huo wa kampeni
kuwazuia hao waumini mpaka lisubirie mshindi kupatikana

Kibinafsi kujifananisha na Mungu kiimani ni kosa kubwa
la kiimani na ni sawa kutengwa na kanisa.....tatizo
ni kwanini iwe sasa... wakati tayari madhara ya udini
yameanza kuonekana lingefanyika mapema..
walau tungeona mantiki
 
Wasingeweza kipindi cha kampeni maana ingeonekana kanisa linapigia kampeni wapinzani
 
Kujifananisha na Mungu, mwana wa mungu na roho mtakatifu!!!! hiyo adhabu inawafaa.
 
Dhambi zote zinasamehewa isipokuwa dhambi ya kumtukana Roho Mtakatifu ambayo huyo mbunge amefanya kwa mfananisha Roho Mtakatifu na Diwani ambaye labda haamini katika Roho.
Kanisa limfungie huyo Mbunge kama ni Mkatoliki lakini kuwafungia wote waliompigia kura ni ngumu.
 
kama ni kweli mtu kujifananisha na Mungu ni kosa kubwa sana.wapewe adhabu inayostahili!
 
Kwa mkatoliki yeyote kinachosemekana kimefanyika huko Sumbawanga ni utaratibu wa kawaida katika kanisa hilo, na wala hakina harufu yeyote ya kisiasa. Mimi ninayo mifano mingi inayothibitisha jambo hilo; kwa mfano kuna wakati ambapo paroko kwa amri yake yeye mwenyewe anatoa amri kwamba waumini walio chini yake hawaruhusiwi kuhudhuria sherehe ya harusi ya muumini mwenzao, ikiwa itafungwa bila ya kuzingatia matakwa ya kanisa hilo; amri kama hiyo ikisha tolewa, waumini wote wanaoipuuzia kwa kawaida utengwa na kanisa mpaka watakapotubu na kufanya adhabu husika. Inavyoelekea hali hiyo ndiyo iliyojitokeza huka Sumbawanga; baada ya mgombea huyo kufanya madai hayo, ambayo kulingana na imani ya kikatoliki ni kufuru, waumini wa kanisa hilo, bila shaka watakuwa wameamriwa kutenga na kampeni zake; nahivyo muumini yeyote aliyepuuzia jambo hilo hana budi atengwe na kanisa hilo mpaka atubu.
 
Waliofukuzwa tunawakarisha msikitini. Karibuni.

Naona mods ile post yangu ya mwanzo hawajaipenda ya kuwakaribsha kwenye uIslam.
 
Sasa najiuliza kanisa lilikuwa wapi wakati huo wa kampeni
kuwazuia hao waumini mpaka lisubirie mshindi kupatikana

Kibinafsi kujifananisha na Mungu kiimani ni kosa kubwa
la kiimani na ni sawa kutengwa na kanisa.....tatizo
ni kwanini iwe sasa... wakati tayari madhara ya udini
yameanza kuonekana lingefanyika mapema..
walau tungeona mantiki

Kwani mwandishi ameeleza wametengwa jana au leo? Si ndio maana kila mmoja anaona habari yenyewe haijaandikwa kiuandishi - maana haielezi issue yenyewe ni nini hasa!
 
Waliofukuzwa tunawakarisha msikitini. Karibuni.

Naona mods ile post yangu ya mwanzo hawajaipenda ya kuwakaribsha kwenye uIslam.

Nendeni huko Sumbawanga mkawachukue na mjue pia hamtakaa nao maana wakila nyama ya nguruwe mtaona ni kero kwenu pia au wasipopendelea kuwakata wezi mikono na kuwapiga mawe hadi kufa wanaofumaniwa!
 
funny!!! Kanisa lina takwimu za waumini wake ni wafuasi wa chama kipi cha siasa?

Nadhani hujajua stori yenyewe inaongelea nini! Haieleweki vizuri. Ila nadhani ilitokea kuwa baada ya huyo mbunge kutumia maneno ambayo yalionekana kufuru kwa Kanisa, Kanisa lilitoa onyo kwa wale wanaoshiriki kampeni za huyo 'mbunge aliyekufuru' na waliopuuza ndio wanaoongelewa na siyo wana-CCM wengine waliofanya kampeni zao kihalali.
 
SAFI SANA, DAWA YA WAUMINI WANAFIKI NI KUWA-BAN.....
PONGEZI KANISA KATOLIKI KWA UAMUZI HUU
.:lock1:
 
Lazima kanisa lifanye uamuzi mgumu. Naafiki kwa hatua hiyo iliyochukuliwa na Kanisa Katoliki. Hao wanaomkufuru Mungu anayetunyeshea mvua na kutuangazia jua hawafai, wasije wakatuletea laana.

Kwa dini zinazoona hilo si tatizo wanaweza kwenda kuwachukuwa na kuwafanya waumini wao, maana huenda wanafanana nao.
 
Kuna watu humu hawajalielewa Kanisa Katoliki likoje na linafanyaje kazi, and yet wanatalka sana kuliandika habari zake. Kanisa jamani haliwezi kufanya mambo kama halioni. Mwenye macho haambiwi tazama. Kama wamefungiwa basi kuna tatizo jingine siyo la kuchagua mtu.
 
Back
Top Bottom