Lupweko
JF-Expert Member
- Mar 26, 2009
- 20,680
- 20,432
Ndoa ni sakramenti, wizi, uzinzi na mengineyo ni dhambi. Kanisa linamtambua muumini kwa sakramenti anazopaswa kuwa nazo, na si kwa dhambi alizonazo. Si ndoa tu, hata angekuwa ni kijana mdogo wa sekondari amekufa bila sakramenti ya ubatizo, asingezikwa kwa imani ya Kanisa Katoliki. Kwa ufupi, kanisa Katoliki linawatambua waumini wake kwa sakramenti zao (rejea mgogoro wa sensa uliohusisha idadi ya wakatoliki nchini - hawa walihesabiwa kwa kutambuliwa through status yao ya ubatizo ambayo ndio sakramenti ya awali kabisa kumtambulisha Mkatoliki). Kama makanisa mengine yanawatambua waumini wao kwa kupitia mahudhurio ya kanisani, huo ni utaratibu wao, lakini imani ya Kanisa Katoliki inamtambua Mkatoliki pale anapobatizwa, na akifikia umri wa kuishi na mwenza wake basi awe ameshapata kipaimara kisha afunge ndoa. Usichanganye dhambi na sakramenti. Mtu anaweza akawa hatendi dhambi lakini kama hajabatizwa huyo si MkatolikiAaahn unaona sasa Kama ishu ni kufunga ndoa haya niambie ni wangapi wamefunga ndoa halafu wanamichepuko chungu nzima? Na kufanya Zambi nyingine nyingi Kama vile Wizi, kusema uongo, wivu, fitna, ushirikina n.k? Hao wanatishi bila ndoa wapendeni, waombeeni, wafundisheni Neno wapate kufahamu ipasavyo na siyo kuwahukumu! hiyo inaonesha namna gani mko mwilini zaidi!