Kaniambia tuachane baada tu ya kumwambia nataka kumuoa

juvenile davis

JF-Expert Member
Apr 13, 2015
4,752
4,449
Sijamuelewa huyu mwanamke,ni mtoto mmoja wa kisukuma kutoka huko nyegezi mwanza,nimekuwa nae kwenye mahusiano takribani miezi minne sasa,kilichonishangaza ni kwamba nimemwambia nataka nipeleke posa kwao na wanijue maana nataka nimuoe,eti nilivomtamkia maneno hayo tu ni kosa kubwa sana maana kaniambia tuachane na hajibu simu wala msg zangu,sijaelewa tatizo ni nini?Maaana hajaolewa na kiukweli nimempenda sana kuliko hata wanawake zangu niliozaa nao.
 
Huenda huyo mwanamke anapenda dd tu hataki kuingia kwenye ndoa akawa anaishi kwa mipaka
 
Hapana.naongelea Huyu bwana juve kazaa hovyo kila mtoto na mamake..ni mwanamke gani atajiskia fahari kuolewa name mwanaume wa aina hii?
Post zake yaelekea ni kiwembe hatar sembuse umface!!!!!!! Kwa mwenye saikolojia hata matamshi / maongez yake tu yanakupa jibu tosha.
 
Kama humfikishi anapotaka atakubalije kufunga pingu za maisha?

Kuliko atoke nje ya ndoa ni bora aikatae ndoa.

Natania tu ila kama ni kweli samahani.
 
Kuna mdada nilikutananae pale arusha nikawa rafiki yake. Alikuwa anafanya kazi ktk ofisi moja ya contractors wa ujenzi. Akanihakikishia kuwa hana mtu. Nikamwachisha kazi hapo ili nimpatie kazi nzuri ktk ofisi za serikali. Tukaendelea na uchumba km kawaida lakini Swala la kufunga ndoa analikwepesha kiaina yeye anataka urafiki tu uendelee. Kuna siku nikagundua ktk cm yake km amechati na mtu km mume vile ambaye anaishi Moshi. Nikapeleleza kimyakimya nikagundua ni kweli anamume waliefunga nae ndoa km miaka miwili hivi. Yeye kila wkend anaenda moshi kwao kumbe Ndo anaenda kwa mume. Nilipokusanya data zote Nilianza kumwuliza ili nione atakiri ama la. Chakushangaza mdada akaona sasa namwumbua akaomba urafiki wetu umeshaingia unafiki hivo sasa tuachane. Akakusanya vilivovyake akaondoka
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom