KANGI LUGOLA kutolewa kafara!

Laiser James

Member
Dec 5, 2013
77
8
Mh Mbunge Kangi Lugola,ambae amekuwa mwiba mkali kwa Mawaziri huenda akatolewa kafara baada ya kutumiwa massege za kutishiwa kuuawa huku yeye akisema kuwa hataenda kutoa ripoti Polisi.
Hii ni baada ya mh Kangi Lugola kuwa miongoni mwa Wabunge waliotamka wazi bila kificho ndani ya Bunge kuwa mh Waziri Mkuu ni mzigo na anaetakiwa kujiuzulu.

Wiki mbili zilizopita wakati Wabunge wakijadili ripoti ya tume ya bunge iliyowasilishwa na mwenyekiti wake Mh James Lembeli, mh Kangi Lugola alimshambulia Waziri mkuu akimtuhumu kuwa Wamempa,Ndege,Helkopita na Magari ya Vingora lakini wakati Watanzania wanauawa yeye alikua amejikalia tu Ofisini. "ulikuwa wapi Mh Waziri mkuu" tumekupa magari na vingora,tumekupa Ndege,tumekupa na hata Helkopta?

Kwa habari zaidi soma gazeti la Jambo leo!
 
Nani sasa anamtisha? Si Pinda mwenyewe aliwapa ruhusa wabunge kumwajibisha kama wanaona hawajibiki?
 
Ulikuwa wapi mhe waziri mkuu? Utaponea wapi Kagasheki? Ulisema umenyang'anywa majukumu..we ni waziri wa namna gani..? Utaponea wapi? Utaponea wapi waziri wa mambo ya ndani! I like this guy
Lugola anasema kweli. Sema tu huwa anashinikizwa na kundi lake la Team Lowasa kuongea kwa jazba
 
Kaazi kweli kweli.
Nani sasa anamtisha? Si Pinda mwenyewe aliwapa ruhusa wabunge kumwajibisha kama wanaona hawajibiki?

Lugola anasema kweli. Sema tu huwa anashinikizwa na kundi lake la Team Lowasa kuongea kwa jazba. Kangi Lugola ni Mwana CCM ambaye anatimiza vema wajibu wake wa kuisimamia serikali iwajibike kwa wananchi. Hongera sana Lugola. Hizi propaganda za Jambo Leo zisikukatishe tamaa
.
 
Lugola kaona hamna anaemuongelea,anaamua kuanza kujipigia debe mwenyewe.
Mwambieni uwaziri haupati ng'oo.
 
Dah, Kunahawa Watu Wawili Nchimbi Na Pinda. Hawa Jamaa Ukiwaboa Sidhani Kama Utapona. Kama Huyu Mwingine Sijui Alimpeleka Wapi Mtoto Wa Marechela Na Yule Binti Amina Chifupa!
 
Kangi Lugola ni Mwana CCM ambaye anatimiza vema wajibu wake wa kuisimamia serikali iwajibike kwa wananchi. Hongera sana Lugola. Hizi propaganda za Jambo Leo zisikukatishe tamaa

Kwa hyo hao wabunge wengine waliobaki nao ni mamizigo tu ndani ya bunge.
 
Kangi Lugola ni Mwana CCM ambaye anatimiza vema wajibu wake wa kuisimamia serikali iwajibike kwa wananchi. Hongera sana Lugola. Hizi propaganda za Jambo Leo zisikukatishe tamaa
Leo hii wewe unasema jambo leo ni la propaganda...???
 
GENERAL
SalutationHonourableMember picture
C:\User1\AppData\Local\Temp\msohtmlclip1\01\clip_image002.jpg
First Name:Alphaxard
Middle Name:Kangi Ndege
Last Name:Lugola

EDUCATION
School Name/LocationCourse/Degree/AwardStart DateEnd DateLevel
University of Dar Es SalaamMasters19961997MASTERS DEGREE
University of Dar Es SalaamB.Com19881992GRADUATE
University of Leicester, UK-20082010CERTIFICATE
Tanzania Police AcademyCertificate19931994CERTIFICATE
Tanzania Police AcademyCertificate19991999CERTIFICATE
East African School of Aviation , NairobiCertificate20022002CERTIFICATE
International Civil Aviation Organisation, NairobiCertificate20022002CERTIFICATE
Songera Boys' Secondary SchoolA-Level Education19851987HIGH SCHOOL
Sengerema Secondary SchoolO-Level Education19811984SECONDARY
Nyamitwebili Primary SchoolPrimary Education19741977PRIMARY
Mugeta Primary SchoolPrimary Education19781978PRIMARY
Kafunjo Primary SchoolPrimary Education19791980PRIMARY

EMPLOYMENT HISTORY
Company NamePositionFromTo
The Parliament of TanzaniaMember - Mwibara Constituency20102015
East African CommunityChief Security Officer20022010
Tanzania Airports AuthorityHead of Security Section (Airports)20012002
Tanzania Police ForceHead of Police Post (Grade A)19992000
Tanzania Police ForceInvestigation Officer19981999
Tanzania Police ForceInspector19931998
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom