Kangi Lugola amwashia moto Waziri mkuu bungeni, anataka afukuzwe kazi

huyu mzee ni zaidi ya ccm! bora ahamie zake chadema, maana uhai wake........yasije yakawa mambo ya kolimba!
 
HUYU mzeee ni zaidi ya jembe sio mnafki wala hana ngonjera hata kidogo, sio mchumia tumbo kama zitto na boss wake Mwigulu...Lugola ni kiongoz shupavu asie ogopa lolote, ushauri wangu kwake ahamie chadema akaungane na wapambanaji wa kweli...
 
Kwakweli PM ni dhaifu mno lkn matatizo ya haya ya ufisadi yamekuzwa na mfumo uliopo wa kulindana na kupeana mamlaka kirafiki, mambo nyeti kuingiliwa na siasa na mapungufu ya kitaalam. Hili hata Mr. President anahusika.
 
Mh.Kangi lugola akiendelea kuchangia taarifa za kamati za oversite,amemshauri rais Jakaya Kikwete kumfukuza kazi waziri mkuu wa Tanzania kama anaitakia mema nchi hii.kasema Pinda ameshindwa kuwajibika mwanzo hadi mwisho.my op.Wabunge wa ccm sasa wanakumbuka shuka kumekucha.

CCM dhambi inawatafuna......
 
Afukizwe tu maaana hatuna namna, ni PM wa kwanza toka uhuru kupatwa na msukosuko isiyoisha
 
Mbunge wa Mwibara (CCM) Kangi Lugoda ameshauri Rais JK awatimue kazi mara moja Waziri Mkuu Pinda na Waziri wa TAMISEMI Hawa Ghasia kutokana na uzembe kazini ukiwemo wa kuachia sh. Bil. 644 za wafadhili zikiwa ni msaada kwa TAMISEMI kutafunwa kifisadi na hakuna hatua zimechuliwa! Amehoji udhaifu mwingi ulioko katika TAMISEMI ikiwemo kuendelea kulipwa mishahara kwa watumishi feki na wafu. Amehoji upole wa Pinda akisema upole hauna dawa wala tiba, na akahoji ni hadi lini Bunge litaendelea kushauri? Ametaka mtindo wa Timuatimua uwe adapted na JK mara moja ili kuweka mambo sawa!

Unajua kijana, sisi CCM ndiyo wenye nchi watoto wetu wanauza madawa ya kulevya hamtufanyi kitu huo utaratibu wa timuatimua hatunaga huku kwetu CCM, sisi ndiyo mafisadi OG na hiyo ni sera yetu huyo Kangi anachokoza tuvili tuonekane na sisi tunakemea ufisadi lkn kiukweli hatuwezi fukuza mtu
 
Binafsi,nimemsikia kuanzia mwanzo mpaka mwisho.Kwa kifupi nasema leo mh.Kangi Lugola ameandika historia.
 
Unajua kijana, sisi CCM ndiyo wenye nchi watoto wetu wanauza madawa ya kulevya hamtufanyi kitu huo utaratibu wa timuatimua hatunaga huku kwetu CCM, sisi ndiyo mafisadi OG na hiyo ni sera yetu huyo Kangi anachokoza tuvili tuonekane na sisi tunakemea ufisadi lkn kiukweli hatuwezi fukuza mtu

ImageUploadedByJamiiForums1386418670.236970.jpg
 
KANGI ni moja ya wabunge wachache wenye akiri timamu wanaopatikana CCM.Tatizo cyo MIZENGO tu ila ni SYSTEM yote ya Chama tawala ilishaoza miaka 25 Iliyopita.
 
Fedha za miradi kuliwa kupitia halmashauri ndio mtindo toka Pinda mwenyewe akiwa waziri wa TAMISEMi; hivyo wizi huo ni muendelezo wa tabia iliyokubuhu kwa wakubwa!! Kama mnakumbuka kulikuwa na wizi mkubwa sana wa fedha pale Bagamoyo wakati huo Celina Kombani akiwa waziri wa TAMISEMI; wezi huo uliwahusu mkurugenzi wa halmashauri na maofisa wachache ambapo uchunguzi ulibaini kuwa waziri Kombani na ndugu zake Kikwete kule bagamoyo pia walikuwa beneficiariees wa wizi wa zile pesa, matokeo yake ikawa yule waziri akahamishwa wizara na wahusika wengine wakafunguliwa kesi za kimagumashi ambazo mpaka leo hazijulikani zimeishia wapi!!!! Hii serikali ya magamba ni wachafu kupindukia na wala hawana aibu.
 
KANGI ni moja ya wabunge wachache wenye akiri timamu wanaopatikana CCM.Tatizo cyo MIZENGO tu ila ni SYSTEM yote ya Chama tawala ilishaoza miaka 25 Iliyopita.

Mtoto wa mkulima anaakiri kuliko mnavyofikiria,Kwanini avalie njuga jambo ambalo Boss wake na Chama wanalichekelea

Sent from my BlackBerry 9700 using Jamii Forums
 
Kauili ya mhe Kange Lugola Bungeni leo katika kuchangia Taarifa ya Mthibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za serikali kwamba mchawi aliyewafikisha watanzania hapa tulipo ni Wizara ya wa waziri Mkuu inayosimamiwa na Mhe Pinda kwa kumuomba mhe Raisi J.M.Kikwete kumfukuza kazi waziri mkuu kauli hii kwa maoni yangu sikubaliani nayo kwa kwamtizamo huu Bunge ndio chombo kinamamlaka ya kudhibitisha uteuzi wa waziri mkuu na kinamamlaka ya kumfukuza na kumuondao waziri mkuu kwahiyo mhe Lugola kumuomba mhe Kikwete kumfukuza kazi, ninamashaka na kauli hii nahofia kuamini ni ya kisiasa kwanini wasitumie mamlaka waliyonao kumfukuza na kuonyesha ushupavu na uimara wa bunge kufanya tofauti ni kudhihirisha udhaifu wa Bunge na mshauri mhe raisi asijali maombi ya Lugola, kwa upande wa pili nana amini mhe Lugola kwa kufahamu udhaifu wa muda mrefu wa wabunge wa chama cha mapinduzi na Chama chao(c.c.m) kutokuwa na mshikamano wa pamoja katika masuala ya Taifa ndio maana kaelekeza mzigo huu kwa mhe Kikwete kwa kutumia maamuzi yake ambayo hayajali wingi wakura kumuadabisha bwana huyu.Tufikiri nimadhara kiasi gani yamelikumba Taifa kwa Bunge kushindwa kumuondoa waziri Mkuu katika zoezi lililokuwa linasimamiwa na mhe Zitto Kambwe,watawala wameshindwa kusimamia kuiongoza Nchi kuelekea yaliko maendeleo.
 
pinda amepinda juzi amelidanganya bunge eti mshahara wake million sita bado amestutia hasara kubwa hawa waziri wa ccm ni kufukuza wote tatizo la ccm ukoo wote wezi wanalindana tamati ya ccm 2015 hataamini
 
Hakufafanua sana ni fungu lipi hasa, lakini alikuwa akiizungumzia Ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali. Alionyesha hasira zake dhidi ya 'usoft' wa Pinda kwa kusema hata hapo Bungeni kulikuwa na mawaziri wanne na manaibu mawaziri wawili tu leo asubuhi, ikiwa ni uthibitisho wa wazi kwamba mawaziri hawamheshimu wala hawamjali akiwa ndio kiongozi wa masuala ya serikali Bungeni!

Haya ni maneno ya kisiasa. Hivi kweli ukimwondoa Waziri Mkuu au hata Waziri yeyote basi unatatua tatizo na kuleta maendeleo? Swali dogo tu, mbona hatujaboresha au kujenga reli ambayo wote tunaamini ni uti wa mgongo wa miundo mbinu yetu ya usafirishaji wakati tunaamini pia Waziri aliyepo ni Waziri mchapa kazi? Nafikiri maendeleo ni zaidi ya hawa mawaziri.
 
Back
Top Bottom