sepema
JF-Expert Member
- Jun 13, 2019
- 591
- 1,000
Salaam kwenu
Jana jioni nilitembelewa na mabinti wawili ambao ni wanafunzi wa shule ya msingi.
Ujio wa mabinti hawa ulitokana na kuagizwa na Kaka wa mmoja wabinti hawa waniletee bahasha iliyokuwa na documents flani ndani.Tuseme binti mmoja alikuwa kamsindikiza mwenzake.
Walipokuja nilikuwa nje nafanya shughuli flani hvy nikawasihi waingie sebuleni wanisubiri kwani nilitakiwa kuzikagua hizo nyaraka kabla hawajaondoka.
Kwenye TV nilikuwa nimeweka movie ambayo waliipenda hivyo wakazama Kwenye kuitazama.
Mimi nilipoingia nikawakuta wanaangalia movie sikutaka kuwasumbua badala yake nikachukua Ile bahasha iliyokuwa mezani nakujiridhisha.
Muda ulienda kagiza kakaanza kuingia so ikabidi watoto wale waage nakuondoka.Nilifunga mlango nikawasindikiza kdg ambapo nilipoachan nao niliamua kupitia mahali kubadilishana mawazo na jamaa zangu.
Niliporudi nilienda zangu kulala bila kukaa pale sebuleni.
Eebhanaeee, kumbe pale sebuleni binti mmoja alisahau kanga yake sehemu alipokuwa amekaa.Hili nimeligundua asubhi baada ya kutembelewa na mke wangu bila taarifa.Alikuwa kasafiri.
Hapa kimewaka kweli kweli, wife anadai nilikuwa namchepuko ndo umesahau kanga.Nimejaribu kumwelezea lakini haelewi kabisa. Njia pekee tuliyokubaliana nikuwaita wale watoto waje watoe ushahidi.Yule binti naye sijui imekuwaje kwani hadi saivi hajarudi kubeba kanga yake.
Nataman binti huyo atokee hata saivi japo lazima ajieleze vizuri kuwa ilikuaje akasahau kanga(nguo) sebuleni kwa watu.
Hili nalo mkaliangalie
Wasalaam!
Jana jioni nilitembelewa na mabinti wawili ambao ni wanafunzi wa shule ya msingi.
Ujio wa mabinti hawa ulitokana na kuagizwa na Kaka wa mmoja wabinti hawa waniletee bahasha iliyokuwa na documents flani ndani.Tuseme binti mmoja alikuwa kamsindikiza mwenzake.
Walipokuja nilikuwa nje nafanya shughuli flani hvy nikawasihi waingie sebuleni wanisubiri kwani nilitakiwa kuzikagua hizo nyaraka kabla hawajaondoka.
Kwenye TV nilikuwa nimeweka movie ambayo waliipenda hivyo wakazama Kwenye kuitazama.
Mimi nilipoingia nikawakuta wanaangalia movie sikutaka kuwasumbua badala yake nikachukua Ile bahasha iliyokuwa mezani nakujiridhisha.
Muda ulienda kagiza kakaanza kuingia so ikabidi watoto wale waage nakuondoka.Nilifunga mlango nikawasindikiza kdg ambapo nilipoachan nao niliamua kupitia mahali kubadilishana mawazo na jamaa zangu.
Niliporudi nilienda zangu kulala bila kukaa pale sebuleni.
Eebhanaeee, kumbe pale sebuleni binti mmoja alisahau kanga yake sehemu alipokuwa amekaa.Hili nimeligundua asubhi baada ya kutembelewa na mke wangu bila taarifa.Alikuwa kasafiri.
Hapa kimewaka kweli kweli, wife anadai nilikuwa namchepuko ndo umesahau kanga.Nimejaribu kumwelezea lakini haelewi kabisa. Njia pekee tuliyokubaliana nikuwaita wale watoto waje watoe ushahidi.Yule binti naye sijui imekuwaje kwani hadi saivi hajarudi kubeba kanga yake.
Nataman binti huyo atokee hata saivi japo lazima ajieleze vizuri kuwa ilikuaje akasahau kanga(nguo) sebuleni kwa watu.
Hili nalo mkaliangalie
Wasalaam!