Kamwe sitomsahau huyu mama aliyeninunulia chakula pale babati(HOTEL) nilipokuwa natoka Dodoma to Arusha

Saoka

JF-Expert Member
Oct 23, 2018
404
563
Wakuu habari zenu.

Napenda kumshukuru huyu mama aliyeninunulia chakula pale babati stand pamoja na kunijazia nauli ya bus la (machame) nilikuwa nimetoka kuchukua certificate yangu pale UDOM. nikapanda bus pale stand ya machame nikitegemea kujazia nauli mbeleni mana kuna rafiki yangu aliniahidi kunijazilishia ila baada ya kumwambia nimeshapanda bus akawa hapatikani tena ndipo mama mmoja mzuri pembeni ya siti yangu alipogundua na kukubali kunijazia hiyo pesa,(ubarikiwe sana mama ulikuwa unatumia iphone huku umeweka airphone maskioni) pia ulinipiga lunch ya nguvu pale babati

Mungu akubariki sana mama popote ulipo .nakumbuka ulishukia majengo,nakutafuta sana mama popote ulipo MUNGU akuzidishie

#kuna watu wana moyo mzuri sana hapa duniani

@samahanini kwa mwandiko wakuu nipo speed mno
 
Wewe ulimpenda na hali ya maisha imekubana na ajira hakuna ndio unamkumbuka ili akulee kama kiben10!Vijana hangaikeni bila kuchagua kazi!
Ulipotaja tu IPhone nikajua umemkumbuka kutokana na shida zako!
Mmmh.
 
Mapenzi yanauma na yanaua. Chukua tahadhari
Wakuu habari zenu.

Napenda kumshukuru huyu mama aliyeninunulia chakula pale babati stand pamoja na kunijazia nauli ya bus la (machame) nilikuwa nimetoka kuchukua certificate yangu pale UDOM. nikapanda bus pale stand ya machame nikitegemea kujazia nauli mbeleni mana kuna rafiki yangu aliniahidi kunijazilishia ila baada ya kumwambia nimeshapanda bus akawa hapatikani tena ndipo mama mmoja mzuri pembeni ya siti yangu alipogundua na kukubali kunijazia hiyo pesa,(ubarikiwe sana mama ulikuwa unatumia iphone huku umeweka airphone maskioni) pia ulinipiga lunch ya nguvu pale babati

Mungu akubariki sana mama popote ulipo .nakumbuka ulishukia majengo,nakutafuta sana mama popote ulipo MUNGU akuzidishie

#kuna watu wana moyo mzuri sana hapa duniani

@samahanini kwa mwandiko wakuu nipo speed mno

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimemuona wakati anashuka hapa Majengo anaishi mitaa ya Kitopeni Majengo ya Chini.
 
Wewe ulimpenda na hali ya maisha imekubana na ajira hakuna ndio unamkumbuka ili akulee kama kiben10!Vijana hangaikeni bila kuchagua kazi!
Ulipotaja tu IPhone nikajua umemkumbuka kutokana na shida zako!

alidata na iPhone
 
Wewe ulimpenda na hali ya maisha imekubana na ajira hakuna ndio unamkumbuka ili akulee kama kiben10!Vijana hangaikeni bila kuchagua kazi!
Ulipotaja tu IPhone nikajua umemkumbuka kutokana na shida zako!

Nimecheka sana mkuu tena kwa sauti😅😅
Nilichotaka kuandika,umeniwahi mkuu
Jamaa alishindwa kuomba namba ila leo kakumbuka baada ya kitaa kukosa ajira na maisha magumu,kaona amkumbuke yule mama na hajui atampataje
Anataka kulelewa kijana hahahahaha
Nimecheka sana,anajifanya kuja kushukuru jamii forum😅😅
Kweli maisha mqgumu jamani daah
Oyaaaa jiwe wape ajira vijana wataolewa bureee
 
Ujumbe mzuri kwa anaelewa
Wema ni wa kushukuru kwa baadhi


Sent from my iPhone using Tapatalk
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom