CR wa PROB
Senior Member
- Sep 21, 2011
- 170
- 29
Awali ya yote nipende kuwapongeza kampuni ya tiGO kwa kuwa kampuni mama ya Tanzania!!
Tatizo kubwa linaloniumiza mimi kama mteja wenu ni pale mnapotudanganya kupitia matangazo yenu ya biashara kuwa dakika moja sh, 60 za kitanzania kisha robo shilingi ambayo ni sawa na sh 15 kwa dakika ila sio hivyo, kwa mtanzania yeyeote mwenye uelewa mdogo tu kama wa kwangu amabao hauhitaji elimu ya chuo kikuu ameashagundua utapeli wenu na mpo hatiani kuwapoteza wateja wenu wengi. Hivyo basi msipende kutudangaya sisi wateja wenu kama watoto wadogo.
Nilidhani labda ni laini yangu tu ambayo inanikata hela kwa fujo hivyo, ila kwa utafiti wangu mdogo nlioufanya nimedhihirisha ya kwamba sio mimi bali tupo wengi mno ambao mnatuibia kupitia matangazo yenu ya biashara, Swala kama hili halihitaji maandamano ni kulifanyai tu marekebisho.
Vilele kuna mfumo ambao mmeuanzisha wa kumwekea mtu nyimbo ambazo hazina maadili huku hajaziomba na mkiendelea kumkata hela kila siku ya Mungu na akiwapigia ili muondoe simu hazipokelewi, Mkiona biashara imewashinda ni bora mfungashe virago muondoke hata kabla mda wenu wa kulipa kodi haujafika, kwani nimesikia hata kodi hamlipi!!!!!!
Tatizo kubwa linaloniumiza mimi kama mteja wenu ni pale mnapotudanganya kupitia matangazo yenu ya biashara kuwa dakika moja sh, 60 za kitanzania kisha robo shilingi ambayo ni sawa na sh 15 kwa dakika ila sio hivyo, kwa mtanzania yeyeote mwenye uelewa mdogo tu kama wa kwangu amabao hauhitaji elimu ya chuo kikuu ameashagundua utapeli wenu na mpo hatiani kuwapoteza wateja wenu wengi. Hivyo basi msipende kutudangaya sisi wateja wenu kama watoto wadogo.
Nilidhani labda ni laini yangu tu ambayo inanikata hela kwa fujo hivyo, ila kwa utafiti wangu mdogo nlioufanya nimedhihirisha ya kwamba sio mimi bali tupo wengi mno ambao mnatuibia kupitia matangazo yenu ya biashara, Swala kama hili halihitaji maandamano ni kulifanyai tu marekebisho.
Vilele kuna mfumo ambao mmeuanzisha wa kumwekea mtu nyimbo ambazo hazina maadili huku hajaziomba na mkiendelea kumkata hela kila siku ya Mungu na akiwapigia ili muondoe simu hazipokelewi, Mkiona biashara imewashinda ni bora mfungashe virago muondoke hata kabla mda wenu wa kulipa kodi haujafika, kwani nimesikia hata kodi hamlipi!!!!!!