security guard
JF-Expert Member
- Sep 27, 2011
- 799
- 603
Miongoni mwa matunda ambayo yametokana na Ziara ya Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo nchini Algeria ni pamoja na Kampuni ya Umma ya Algeria, NAFTAL inayosindika na kusambaza gesi ya kupikia mijini na vijijini kukubali kuja kuwekeza nchini.
Nchi ya Algeria ambayo ina asili ya Jangwa na Nyika imeacha kabisa kutumia kuni pamoja na mkaa kwa mahitaji yao ya jikoni na badala yake wanatumia gesi ambayo inavunwa, kusindikwa na kusambazwa nchini mwao.
Kampuni Kubwa ya NAFTAL ambayo husindika gesi kiasi cha 2milion tons/year (LPG for domestic use) inasambaza LPG kutumia mabomba yenye urefu 2,886km, pamoja na magari na reli kuwafikia wanavijiji.
Kampuni hiyo sasa inajiandaa kuja nchini kufanya visibility study juu ya hatua muhimu za kuanza nazo katika uwekezaji huo mkubwa hapa nchini ambao utasaidia kuokoa maliasili nyingi zitokanazo na misitu. Tanzania imetoa ripoti ya maliasili na kubainisha hasara kubwa itokanayo na matumizi ya mkaa na kuni na uvunaji haramu wa mazao ya misitu ikiwemo mbao na magogo. Kuingia kwa Mradi huu hapa nchini kutapelekea Misitu yetu kubaki salama na hivyo kuchangia katika kudumisha hali ya hewa safi nchini.
Hongera Profesa Muhongo kwa hatua hii muhimu kwa maendeleo ya nchi na wananchi wa Tanzania.
Nchi ya Algeria ambayo ina asili ya Jangwa na Nyika imeacha kabisa kutumia kuni pamoja na mkaa kwa mahitaji yao ya jikoni na badala yake wanatumia gesi ambayo inavunwa, kusindikwa na kusambazwa nchini mwao.
Kampuni Kubwa ya NAFTAL ambayo husindika gesi kiasi cha 2milion tons/year (LPG for domestic use) inasambaza LPG kutumia mabomba yenye urefu 2,886km, pamoja na magari na reli kuwafikia wanavijiji.
Kampuni hiyo sasa inajiandaa kuja nchini kufanya visibility study juu ya hatua muhimu za kuanza nazo katika uwekezaji huo mkubwa hapa nchini ambao utasaidia kuokoa maliasili nyingi zitokanazo na misitu. Tanzania imetoa ripoti ya maliasili na kubainisha hasara kubwa itokanayo na matumizi ya mkaa na kuni na uvunaji haramu wa mazao ya misitu ikiwemo mbao na magogo. Kuingia kwa Mradi huu hapa nchini kutapelekea Misitu yetu kubaki salama na hivyo kuchangia katika kudumisha hali ya hewa safi nchini.
Hongera Profesa Muhongo kwa hatua hii muhimu kwa maendeleo ya nchi na wananchi wa Tanzania.