Kampuni ya madini yafanya unyama wa kutisha

Lunyungu

JF-Expert Member
Aug 7, 2006
8,873
1,894
Wananchi wapigwa risasi, walawitiwa na walinzi
*Mwekezaji ajinasibu ni rafiki wa Rais Kikwete
*Wananchi sasa waja juu, wataka tamko la Rais

Na Mwandishi Wetu, Korogwe

MIGOGORO kati ya wawekezaji kwenye sekta ya madini na wachimbaji wadogo wadogo wiki hii imechukua sura ya kutisha zaidi baada ya kubainika kuwa wananchi wapatao 20 wa kijiji cha Kalalani na Kigwase Kata ya Mashewa wilayani Korogwe wamefanyiwa vitendo vya kikatili na kinyama ikiwemo kulawitiwa na walinzi wa kampuni ya Amazon Trading Co. (T) Ltd.

Wakati wananchi hao wakikumbana na unyama huo, Majira Jumapili lilipotembelea eneo hilo jana limeelezwa kuwa katikati ya mateso na unyama huo, licha ya baadhi yao pia kupigwa risasi, wamekuwa wakikerwa zaidi na majigambo ya mmiliki wa mgodi huo anayejinasibu kuwa ni rafiki wa karibu wa Rais Jakaya Kikwete na kwamba hakuna mtu anayeweza kumsumbua.

Baadhi ya wananchi wakiwa na risasi miilini wamelazimika kukimbilia kwa waganga wa jadi kupata tiba wakiogopa kwenda hospitali ambako wanahofu watakamatwa na polisi waliokuwa wakiendesha msako.

Vita ya raslimali

Chanzo cha tafrani hiyo imeelezwa kuwa ni kitendo cha wananchi hao kukosa maeneo ya kujipatia riziki yao kufuatia eneo la madini kupewa mwekezaji huyo na hivyo wengi wao kulazimika kuingia katika baadhi ya maeneo yanayomilikiwa na mwekezaji huyo na kuchimba madini.

Katika kukabiliana na uvamizi huo imeelezwa kuwa mwekezaji huyo amejenga 'mahabusu' ndani ya mgodi huo ambapo wananchi mbalimbali wanapokamatwa huwekwa humo na ndipo mkasa wa unyama wa kulawitiwa unapojitokeza.

'Kambi ya mateso'

Uchunguzi wa gazeti hili ulibaini kuwa zaidi ya wanakijijini 15 waliowahi kushikiliwa katika 'mahabusu' ya mgodi huo walilawitiwa na baadhi ya walinzi wa mgodi huo kabla ya kuachiwa huru na wengi wameshindwa kueleza unyama huo wakiona aibu.

Mmoja wa wafugaji wa kijijini hapo ambaye ni mmasai, Bw. Maziwa Telikia alisema kuwa wamiliki wa mgodi huo pindi wanapowakamata wachimbaji wadogo wanaoingia kwenye maeneo yao huwafungia katika 'mahabusu' yao na kuwasimamia walizni wao wakiwalawiti raia.

"Kuna mwenzetu mmoja wa Kimasai ana umri wa miaka 70, alikuwa akichunga ng'ombe wake, akakamatwa na kupelekwa mahabusu, akalawitiwa na hivi sasa anatokwa na damu kila anapokaa,'' alisema mkazi mwingine Bw. Oloronyo.

Mkazi wa kijijini hapo Bw. Mohamed Saidi (30) akizungumza mbele ya Katibu wa CCM tawi la Kigwase, Bw. David Swai alionesha jeraha la risasi na kueleza kuwa amekuwa akiishi na maumivu makali kutokana na kuogopa kwenda hospitali kwa kuwahofia polisi.

Akisimulia mkasa huo alisema Aprili 12 mwaka huu akiwa anafua nguo mtoni alisikia watu wanakimbizana na askari wa FFU wakiwa na mgambo wa kampuni hiyo ya Amazon, alipohoji kulikoni alistukia anapigwa risasi kwenye makalio na kutishwa na askari hao asiende hospitali kwani watamfungulia kesi ya wizi wa madini.

'Rais, ni sisi au mwekezaji?'

Wanakijiji hao wakionesha kukerwa na ukatili huo na pia majigambo ya mwekezaji wa mgodi huo, sasa wanamtaka Rais Kikwete atoe tamko iwapo ni kweli yeye ndiye anampa nguvu mwekezaji huyo na wakasema wanaamini kuwa walimchagua Rais Kikwete ili awaletee maisha bora na si ukatili unaofanywa na watu wanaodai kuwa ni marafiki zake.

Mwenyekiti wa kijiji cha Kilalani, Bw Agustino Yustino Hassani alisema wananchi waliopigwa risasi wanazidi 20 na wengine inadaiwa wamefia porini na kuzikwa kwa siri na ndugu zao kwa kuogopa kutoa taarifa polisi.

Polisi: tunachunguza

Kamanda wa Polisi mkoani Tanga, Bw Simoni Sirro amethibitisha kuwepo tafrani eneo hilo ambapo alisema kuwa ilianza wiki iliyopita kwa kuwahusisha ambapo askari wa FFU walilazimika kuingilia kati kuwatawannya wananchi waliokuwa wakipambana na walinzi wa mgodi.

Huku akionya kuwa uchunguzi utakapokamilika kuhusu tukio hilo askari au walinzi waliohusika watachukuliwa hatua, aliwataka wananchi nao waache kuvamia mgodi huo na kuwakaripia wamiliki wa mgodi kwa 'kujenga mahabusu.'

"Hakuna kampuni inayoruhusiwa kuwa na mahabusu yake…hakuna kampuni inayoruhusiwa kuwalawiti wahalifu hata kama wamewakosea, inayotoa hukumu ni mahakama pekee, naomba wananchi wanipe ushirikiano tukomeshe vitendo hivi na wao kama wanavamia migodi ya watu waache tukibaini watafikishwa mahakamani," alisema Bw. Sirro.

DC:Ndio nasikia, ngoja nifuatilie

Akizungumza kwa simu na gazeti hili jana Mkuu wa Wilaya ya Korogwe, Bi. Betty Mkwasa amesema hakuwa na taarifa na tukio hilo na kuahidi kulifuatilia.

"Nimekuwa naangalia matukio ya polisi hapa sijaliona tukio hilo.Nashukuru kunijulisha, ngoja sasa nifuatilie," alisema.

Mmoja wa maofisa wa mgodi huo aliyekataa kuwekwa bayana gazetini alidai wanakijiji hao wamekuwa na tabia ya kuvamia mgodi huo mara kwa mara hali ambayo aliwalazimu kutoa taarifa polisi kwa msada zaidi.

Tangu kampuni ya Amazon iuchukue mgodi huo wa madini ya ruby na saphire mwaka 2005 kutoka kampuni ya AAPS iliyokuwa ikiumiliki mgodi huo tangu mwaka 1988, kumekuwepo na migogoro ya mara kwa mara kati ya uongozi wa mgodi huo na wananchi.
 
inasikitisha sana kwa kweli nchi wanavyopewa watu wa nje na wazawa wanaachwa kufa njaa tu! JK kazi yake ni kusafiri tu, najua hili ni jambo dogo sana kwake yeye JK, lakini wanakijiji hao hao ndio waliompigia kura na kumpa hicho cheo, basi na awaangalie aache hiyo siasa ya kusema kuwa hana habari za migogoro kati ya wananchi na wamiliki wa migodi kwenye maeneo yote Tz yenye madini.
Na hawa mapolisi wetu ni GESTAPO au ni mapolisi wa kulinda wananchi jamani?
Kazi iko !!!
 
This is Seroius.

Hivi serikali kwa nini isimnyang'anye huyo mwenye kampuni hiyo leseni ya biashara/kuchimba madini????

Hivi Tanzania hii nani mwenye nchi raia au mwekezaji??????

Kwa nini mkuu wa pOlisi wilaya hiyo asifukuzwe kazi maana hajatoa taarifa kokote kwa unyama ulifanyika hadi magazeti kuanza kufuatilia????

Ni Lini Raia wa Tanzania wataanza kuthaminiwa?

MTIZAMO WANGU

Mimi naona Vita kubwa inanukia Tanzania ambayo itasababishwa na madini maana kila kukicha vurugu vurugu kwenye maeneo ya madini
 
inasikitisha sana kwa kweli nchi wanavyopewa watu wa nje na wazawa wanaachwa kufa njaa tu! JK kazi yake ni kusafiri tu, najua hili ni jambo dogo sana kwake yeye JK, lakini wanakijiji hao hao ndio waliompigia kura na kumpa hicho cheo, basi na awaangalie aache hiyo siasa ya kusema kuwa hana habari za migogoro kati ya wananchi na wamiliki wa migodi kwenye maeneo yote Tz yenye madini.
Na hawa mapolisi wetu ni GESTAPO au ni mapolisi wa kulinda wananchi jamani?
Kazi iko !!!


Polisi wa CCM.Kuhakiki maslahi ya CCM na wakubwa ndani ya CCM wako salama na kutuibia vilivyo .Mkuu wa Wilaya hakuwa na habari wanaleta mchezo .Hilo ni tukio kubwa sana kwa Mkuu wa Wilaya kuto kujua maana wana vikao vya usalama vya Wilaya OCD na Mkuu wa Wilaya wako wote muda wote .Mkuu wa Wilaye ni Mwenyekiti wa vikao hivyo .
 
This is Seroius.

Hivi serikali kwa nini isimnyang'anye huyo mwenye kampuni hiyo leseni ya biashara/kuchimba madini????

haiwezi kumnyang'anya mwekezaji kwa sababu hii nchi inarudishwa kwa wakoloni na huo ni mwanzo tu.

Hivi Tanzania hii nani mwenye nchi raia au mwekezaji??????
kwa sasa tanzania ni ya viongozi na ndo wanaoitafuna na kuuza kila kitu.

Kwa nini mkuu wa pOlisi wilaya hiyo asifukuzwe kazi maana hajatoa taarifa kokote kwa unyama ulifanyika hadi magazeti kuanza kufuatilia????
hawezi kufukuzwa kazi kwa sababu yeye pale amewekwa na viongozi wanaokula na huyo mwenye mgodi.

Ni Lini Raia wa Tanzania wataanza kuthaminiwa?
mpaka watakapokata shauri na kuachana na shetani CCM.
MTIZAMO WANGU

Mimi naona Vita kubwa inanukia Tanzania ambayo itasababishwa na madini maana kila kukicha vurugu vurugu kwenye maeneo ya madini

hili la mwisho uliloliongea ndo litaifikisha tanzania katika nchi ya ahadi, na bila hilo la mwisho uliloligusia ni wazi kuwa mtauzwa na kunyanyasika mpaka mkimbie nchi.
 
Sina haja ya kumaliza story nzima tunapoelekea itabidi ifike wakati viongozi awajibike. Hivi yule Mkuu wa wilaya(Bety) anafanya kazi gani?. Au anasubiri JK atoke madarakani hili tumfikishe Rumande?

Inatakiwa afanye kazi yake mapema sana kabla sheria haijamfikia. Tanzania ni nchi yenye sheria zinazo eleweka na yeye anatakiwa asaidie viongozi ktk kutekeleza sheria hizo. Asisubiri yakamkuta, maana Jk hatamsaidia ktk hilo.
 
this is too much:mad:

na inpokasirisha zaidi ni kwamba haya matendo yote haya, polisi, mkuu wa wilaya, mkuu wa mkoa, wote wanajua, lakini wanakula pesa ya mwekezaji, kwa hiyo wanakhiari watu wafanyiwe unyama wa namna hii.

tume ya haki za binaadam iko wapi?
 
Hawa si wawekezaji ni hayawani na tena hawana akili kabisa kufanya vitendo hivi vya uzalilishaji kwa wananchi.

Haya ni baadhi tu ya matokeo ya mikataba mibovu inayowabeba hawa hayawani.Hakuna sheria ya kuwabana hawa wageni?Mara utasikia wachina wamewapiga watu kung-fu Arusha na Kagera,na tena wale makaburu wa AFGEM waliwahi kumlima makofi afande mkubwa sana pale Arusha na ikaishia jamaa kurudishwa Afrika kusini.

Huo ujasiri wa kusema kikwete rafiki yao wanapata wapi?Au huo mgodi ni wa kigogo na makaburu?
 
Iko siku mambo haya yatakuwa mabaya zaidi... watu ambao wamepoteza kila kitu, ambao wanajiona hawana cha kupoteza zaidi, hawatasita kuchukua silaha na kupigania haki yao.

Tunachotakiwa ni kuhakikisha kwamba HATUFIKI HUKO! Vita ni mbaya ndugu zangu! Mbaya sana! Hatujayaona ya Burundi, Rwanda, DRC na Kenya?

./Mwana wa Haki!
 
Hivi mbona huyo mmliki wa Amazon huwa hatajwi? Nimepitia vyombo vingi vya habari, havimtaji kabisa!
 
na sasa watakachofanya ni kushika mahakama zote ili wakifanya madhambi wasipelekwe sega dansi, sie JF tutapiga kelele weeee lakini wao watakuwa wanatung'ong'a...ndio faida ya uwekezaji hiyo
 
kuna wakati wananchi wetu hutumia vijisababu kuhalalisha uhalifu wao.

na hili tuwe makini nalo.
 
Hii mbona ndiyo strategy yao. Usishangae alichofanya Mukandala pale mlimani dhidi ya wanafunzi wasomi. Kama yeye ndiye mshauri wa Kikwete basi unategemea atafanya nini dhidi ya wananchi wale wanaoweka usiku kwenye migodi ya "wenye nchi"
 
tuwaachie nchi tu yaishe!!

Nchi mbona walishachuka kitambo? Lakini kama wanaanza kuchukua na makalio yetu- this is another issue, something needs to be done.Halafu bila aibu kabisa, jambo kubwa kama hili limetokea wilayani kwake lakini Mkuu wa wilaya hana hata habari!
 
Mmmmm!!!! , mimi nawasifu sana wale watu wa Mara, wawekezaji wanawajua hawataki mchezo, siku wakisikia aaaaa!!! hao!!! mpaka mgodini wanachukua kilichochao wanatoweka, na hii ndiyo dawa.
 
Mmmmm!!!! , mimi nawasifu sana wale watu wa Mara, wawekezaji wanawajua hawataki mchezo, siku wakisikia aaaaa!!! hao!!! mpaka mgodini wanachukua kilichochao wanatoweka, na hii ndiyo dawa.

Kweli mara hawachomi chumvi .Lakini haya mambo kidogo kidogo ya kutumia FFU na kuwaziba midomo yana athari sana .Kesho tusije shangaa kuuana nk .Jamani CCM nasiki mlipata 80% mbona hamuonyeshi kuwajali wapiga kura wenu wa vijijini ?
 
Huo mgodi unafaa uvamiwe kijeshi kama kule kijijini ambapo watu walivamia kituo cha polisi na kuteketeza kila kitu ,nafikiri ilikuwa Tabora au Bukoba sina ukakika lakini kuna kituo kilivamiwa baada ya polisi kumhifadhi jamaa anaeshukiwa kubaka katoto kadogo.
sasa hapo panafaa pavamiwe kikweli kweli sio masihala yaani hapa tulipofikia inafaa kabisa kuungana na majambazi ,ni bora ieleweke wazi polisi waachiwe washirikiane na mafisadi na wananchi washirikiane na majambazi halafu tuone ,kwa kweli ni bora majambazi wanaweza kuchagua katika kufanya kazi yao kuliko hawa polisi wa kuzuia fujo ,inakuwaje raia alie huru anaogopa kwenda hospitali ,bila ya shaka polisi watambambikia likesi la wizi wa madini,lakini sasa baada ya kugombana katika siasa watu watagombana katika rasilimali kwa ujinga wa wachache tu,ni tatizo kama hilo ndilo linalosababisha matatizo kule Nigeria ndio maana hata wazungu inawabidi wasaini kwa dau kubwa kabla ya kuamua kuelekea Nigeria naona umefika wakati kwa wawekezaji wakati wa kuuliwa japo kwa nshale.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom