Kampuni ya Jamii Media inahitaji "Office Attendant" nafasi moja (1)

Jamii Opportunities

JF-Expert Member
Feb 10, 2014
4,422
1,384
Kampuni ya Jamii Media inahitaji mhudumu wa ofisi ambaye ataweza kusimamia na kufanya kazi zake za kila siku.

Majukumu ya mwombaji

Awe na uwezo wa kusimamia shughuli za kila siku za Kiofisi. Shughuli hizo ni Kufanya usafi wa ofisini, kufuatilia, kusimamia na kurekodi masuala ya chakula cha timu yote ya Jamii Media, Kununua na kusimamia mahitaji ya jikoni, kushiriki na kuhudumia katika Matukio yanayohusiana na Jamii Media, kujifunza majukumu na kuyatambua pamoja na uwezo wa kujisogeza katika majukumu.

Sifa za Mwombaji

Awe ni Mwanamke
Awe na umri kuanzia miaka 25 na kuendelea
Awe anajua kusoma na kuandika
Awe mkazi wa Dar es Salaam
Awe tayari kufanya kazi kwa mabadiliko na si kwa mazoea

Muda Wa Kazi


Jumatatu – Ijumaa: Saa 2 Asb mpk Saa 11 Jioni
Jumamosi na siku za Sikukuu: Saa 2 Asb hadi Saa 7 Mchana
Jinsi ya kutuma Maombi

Unaweza kutuma maombi kwa njia mbili tofauti

1. Tuma barua pepe (email) kwenda vacancies@jamiiforums.com ikiwa na kichwa cha habari “Office Attendant”, kisha eleza ni kwa nini tukuchague wewe kwa nafasi hiyo.

AU

2. Tuma ujumbe wa whatsapp kwenda namba 0745 200 717 (TAFADHALI USIPIGE), anza ujumbe wako kwa kichwa cha habari “Office Attendant”, kisha eleza ni kwa nini tukuchague wewe kwa nafasi hiyo. Hakikisha ujumbe huo unauandika kwa pamoja na usiutenganishe.

Mwisho wa kuomba 22, Julai 2016
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom