Kampuni ya Israel yaiuzia Saudia teknolojia ya ujasusi

kimsboy

JF-Expert Member
Oct 17, 2016
8,991
17,887
Kampuni ya Israel yaiuzia Saudia teknolojia ya ujasusi

Jun 09, 2021 08:16 UTC

[https://media]

Shirika moja la ujasusi wa mitandaoni la utawala wa Kizayuni wa Israel limeuuzia utawala wa Aal-Saud wa Saudi Arabia teknoljia ya kisasa ya kufanya ujasusi na kudukua mawasiliano ya simu-erevu za rununu.

Hayo yameripotiwa na gazeti la Kizayuni la Haaretz ambalo limefichua kuwa, kampuni ya Quadream inayoongozwa na afisa wa zamani wa Idara ya Kijasusi ya Jeshi la Israel imeiuzia serikali ya Riyadh teknolojia hiyo kwa mamilioni ya fedha kwa miaka mingi sasa.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo iliyochapishwa jana Jumanne, Saudia inatumia teknolojia hiyo ya kijasusi ya kudukua kompyuta au simu za mkononi kuwafanyia ujasusi viongozi wa upinzani na wakosoaji wa Muhammad Bin Salman (MBS), Mrithi wa Ufalme wa Saudia.

Inaarifiwa kuwa, teknolojia hiyo inaweza kudukua mawasiliano ya simu za rununu hususan iPhones, inaweza kudhibiti kamera tokea mbali, kurekodi mazungumzo na kutambua sehemu aliko mtumiaji, pasi na mwenyewe kujua.

Kwa mujibu wa gazeti hilo la Kizayuni, Saudi Arabia, Bahrain na Imarati (UAE) zina mikataba mikubwa ya siri ya kununua vifaa vya kijasusi kutoka kwa utawala wa Kizayuni wa Israel.

[https://media]

Mwaka 2019, Saudi Arabia iliripotiwa kununua programu ya kufanya ujasusi yenye thamani ya dola milioni 300 kutoka utawala wa Kizayuni wa Israel.

Itakumbukwa kuwa, shirika moja la kijasusi la utawala wa Kizayuni wa Israel lilitoa msaada mkubwa kwa ufalme Saudi Arabia ili kufanikisha mauaji ya mwandishi habari Jamal Khashoggi ambaye alikuwa mkosoaji mkubwa wa ufalme huo wa kiimla.

4bpu41feb8433e1a47w_800C450.jpeg
 
Kwaiyo waarabu ni vichwa maji ? Hawawezi developed technology kama hiyo wao wenyewe ?
 
Kwaiyo waafrika ni vichwa maji ? Hawawezi developed technology kama hiyo wao wenyewe ?

Kweli nyani hajioni kundule


Ni bora hata waarabu pesa ipo...kuliko waafrika ambao neither technology nor money
Kwaiyo waarabu ni vichwa maji ? Hawawezi developed technology kama hiyo wao wenyewe ?
 
Kwaiyo waafrika ni vichwa maji ? Hawawezi developed technology kama hiyo wao wenyewe ?

Kweli nyani hajioni kundule


Ni bora hata waarabu pesa ipo...kuliko waafrika ambao neither technology nor money
Unaulizwa swali lingine unajibu jibu lingine....hii inadhihirisha akili yako ilivyo na shida mkuu
 
Kwa nini Saudia asiwaige wachina kurecruit wadukuzi wakubwa wa marekani nk kuja kuwapika vijana wake
 
Kwa nini Saudia asiwaige wachina kurecruit wadukuzi wakubwa wa marekani nk kuja kuwapika vijana wake
Mashirika makubwa yanatumia pesa nyingi ili kurubun kuuza bidhaa zao jambo hilo mchina haruhusu hata kidogo na ndicho kinachotokea kwa saudia husuusan kwa huyu Bin Salman shida yake ufalme wa saudia ili aupate inabid awe macho muda wote kwa sabab si halali yake kuna anaepaswa kushika hiyo nafas na hapo ndipo wajuz wa kurubun wanapotumia upenyo huo ili kupenyeza matakwa yao.
 
Kwaiyo waafrika ni vichwa maji ? Hawawezi developed technology kama hiyo wao wenyewe ?

Kweli nyani hajioni kundule


Ni bora hata waarabu pesa ipo...kuliko waafrika ambao neither technology nor money
Hajui huyo mwarabu, amejitengezea hela nyingi hahitaji kujisumbua akili, ni kununua tu, pesa iko! 🤣 Waafrika tuna shida sana, hatuna hata hiyo hela
 
Kwaiyo waafrika ni vichwa maji ? Hawawezi developed technology kama hiyo wao wenyewe ?

Kweli nyani hajioni kundule


Ni bora hata waarabu pesa ipo...kuliko waafrika ambao neither technology nor money
Oh kumbe ! Unalingalisha waarabu nasisi wafrika. Hapo sawa. Nilijua utawalinganisha na ma genius wa Islaeli
 
Mashirika makubwa yanatumia pesa nyingi ili kurubun kuuza bidhaa zao jambo hilo mchina haruhusu hata kidogo na ndicho kinachotokea kwa saudia husuusan kwa huyu Bin Salman shida yake ufalme wa saudia ili aupate inabid awe macho muda wote kwa sabab si halali yake kuna anaepaswa kushika hiyo nafas na hapo ndipo wajuz wa kurubun wanapotumia upenyo huo ili kupenyeza matakwa yao.
Yaan pale Riyadh nzima hakuna mwenye akili kama yako ya Kujua kuwa wanarubuniwa na mataifa ili wanunue Tech yao ila we muuza viatu wa uko Namtumbo unajua!!.

Hii " WHERE WE DARE TO TALK OPENLY" kuna watu mnaitafsiri vibaya.
 
Yaan pale Riyadh nzima hakuna mwenye akili kama yako ya Kujua kuwa wanarubuniwa na mataifa ili wanunue Tech yao ila we muuza viatu wa uko Namtumbo unajua!!.

Hii " WHERE WE DARE TO TALK OPENLY" kuna watu mnaitafsiri vibaya.
Labda kwa vile nimeandika kwa kiswahili ndio maana hujanielewa namaanisha kufanya lobbying na kuna mashirika kabisa ya kufanya mambo hayo.
 
Back
Top Bottom