Kampuni ya basi la Shabiby, hii ni hatari sana kwa abiria wenu

Ndio maana mama alitulia tuli wakati mumewe anadundwa yawezekana alishapata wa kumtuliza siti ya karibu akamwambia utakula utakunywa usiwe na hofu

Safari sio kitu cha ghafla inakuwaje aanze kutaka kumpa pesa last minute

mwanamke atakuwa alizira akaona ujinga kwa nini hukunipa mapema kwa hiyo hata wakati anadundwa mwanamke aweza kuwa alikuwa akiwapongeza kimoyo moyo wadundaji kuwa loo kidume gani huyu hadi mtu unaondoka hajakupa hela njiani anasubiri unaingia hadi kwwenye ndio anaanza kujifanya anaenda kuzitafuta wacha adundwe
Eti Hana kadi ya benki, watu wanatumia simbanking tu mie hata sijui kadi ipo wapi?.

Wife aliona huyu bwege wacha wamdunde akajikausha 😃😃😃 wanawake sio watu wazuri 😃😃😃😃😃
 
Haya maisha ya ajabu sana usikute wakati hayo yanatukia inawezekana mke wako alikuwa anafurahia huku akijisemea wacha wamkoneshe amezidi,Halafu unatembea na spika huwa unauza sumu za mende na panya?
 
Ndani ya basi wanatakiwa kuingia abiria tu waliokata tiketi na wafanyakazi wa basi tu sio mtu mwingine

Waliokukunja na kukuvuta miguu wamekuhurumia walitakiwa wakutandike mangumi na makofi juu

Ungempigia simu mkeo ashuke achukue hivyo vipesa vyako koko chini sio wewe upande basi

Ukome kabisa tabia hiyo ya kupanda ndani ya basi wakati wewe sio abiria
Daah!🙄
 
Kama ni kweli kwani nini hukwenda dirishani kumpatia hiyo pesa?
Kama ndivyo kuna Mpesa au Tigo pesa kwanini hukufikiria kumtumia Kwa njia hiyo?
Kwa nini usimpe Dereva ampelekee?au konda!
Kwanini usiache hiyo speaker nje ambayo ilikuweka kwenye mazingira ya kutafsiriwa vibaya?
Kwa kuja kwenye mitandao ya kijamii Ndio suluhisho?
Huna sababu ya kuhukumu wengine Kwa sababu ndogo ndogo hivyo
Jenga utulivu Fanya kazi Kibosho tunahitaji hela December
 
Nimekuwa mpenzi wa kutumia usafiri wa basi la Shabiby mimi na familia yangu kwa miaka zaidi ya mitano

Dar, Dodoma, Dodoma Arusha.

Ila leo kwa yaliyo nikuta kupitia dereva huyu, imeniuma sana

Tulikata tiketi siti namba 4 kwa ajili ya mke wangu kusafiri toka Arusha kuelekea Dodoma ni katika basi linalo wasili Arusha saa nne asubuhi ili kuelekea Dodoma.

Katika pilikapilika za safari nikajikuta nimesahau kadi yangu ya benki ambayo nilidhamiria kuitumia kutoa pesa ili kumpa mke wangu pesa ya matumizi njiani na hii ndio ikawa sababu kwa mimi kukutana na maumivu niliyoyapata kwa dereva nisiye mfahamu jina lake ila ndiye dereva wa basi tulilo kata tiketi hii,yaani basi la Shabiby.

Kutokana na kusahau kadi ya benki nililazimika kumuacha ndani ya gari mke wangu ambaye nilikuwa nikimsindikiza kutafuta namna nyingine ya kupata pesa ili nimpe ya kula njiani,

Baada ya kufanikiwa nikarejea ndani ya gari, kwa lengo la kumpa hiyo pesa mke wangu,ndipo dereva huyu wa shabiby baada ya kuona kuwa mkononi mwangu nimeshika speaker ndogo ambayo huwa naitumia kwa ujasiliamali ,yeye akahisi labda naingia kuuza bidhaa fulani

Hata hivyo kwa upole nilimweleza kuwa, mimi siingi kuuza ila lengo langu ni kumpa mke wangu pesa ya matumizi njiani.

Kilicho niumiza, bado aliendelea kuni zuia kibabe

Hakuishia hapo tu alinikunja huku kondakta wake akinivuta mguu kwa nje,mbele za mke wangu,abiria na watu wengine,kiukweli nimedhslilishwa,naamini kosa langu ni kuutumia usafiri wa shabiby kumsafirisha mke wangu,halafu kuamua kumletea pesa ya matumizi mke wangu.

Kweli nimejaribu kumwelezea mtu niliye fahamishwa kuwa ni kiongozi wake hata sijaridhishwa na namna alivyoshughulikia kudhalilishwa kwangu,kiukweli nimeamua,maana mimi huwa hakuna aina ya biashara mbayo huwa naifanya ndani ya mabasi,zaidi ya leo kumsindikiza mke wangu.

Kweli,kama kampuni ya mabasi ya shabiby haita muwajibisha huyu,aliye nikunja hata kunitishia kunipiga,kisa,nimemweleza kuwa nampa mke wangu pesa ya matumizi njiani, basi kwa mimi binafsi na familia yangu nitafikiria kuto penda kuutukimia usafiri huu kwa mara nyingine,maana nimeaibishwa sana.

Nimejaribu kutafuta mawasiliano ya kampuni ya basi la shabiby makao makuu ili kutoa taarifa ya kero hii, ila sijatambua namna ya kuwapata,ndio maana nimeandika hapa ili wahusika wapatapo ujumbe angalau walishughulikie hili kama wana upendo na wateja wao,tafadhali wasilifumbie macho

Muda huu basi hilo bado lipo njiani kuelekea dodoma, mke wangu niliye msafirisha anaitwa Silvero Mwacha ,yupo sit namba 4, tafadhali wahusika popote mlipo nimekereka, naomba msilifumbie macho hili.

Ni mimi Emmamuel.
Kwa hiyo mkuu unataka kusema hiyo safari ilikua ya ghafula kiasi cha kushindwa kujipanga kabla ya siku ya safari,halafu mke wako unampatia vijihela kwenye basi badala yeye ndio awe mtunza hazina,ili ikitokea dharula yoyote achukue pesa ila wewe upewe taarifa tu ya matumizi na jinsi pesa ilivyo tumika ua bado hujakomaa,au sio mke wako huyo.
 
Ndio maana mama alitulia tuli wakati mumewe anadundwa yawezekana alishapata wa kumtuliza siti ya karibu akamwambia utakula utakunywa usiwe na hofu

Safari sio kitu cha ghafla inakuwaje aanze kutaka kumpa pesa last minute

mwanamke atakuwa alizira akaona ujinga kwa nini hukunipa mapema kwa hiyo hata wakati anadundwa mwanamke aweza kuwa alikuwa akiwapongeza kimoyo moyo wadundaji kuwa loo kidume gani huyu hadi mtu unaondoka hajakupa hela njiani anasubiri unaingia hadi kwwenye BASI ndio anaanza kujifanya anaenda kuzitafuta wacha adundwe
Duh
 
Huyu Jamaa anadis shabiby sasa ata support kampuni gani wkt zilizobaki Karibu zote M*vi Tu.
Shabiby sio tatizo,ila huyu dereva,maana hata ushahidi wa sababu ya mimi kuingia ndani ya basi nilimwonyesha,ila hakutaka kunielewa

Hata hivyo mimi ndie nilikuwa namsafirisha mke wangu,

Shida ni huyu dereva,maana ni mteja ambaye nikitokea hapa jijini arusha ,hata wafanya kazi wa shabiby ofisini,wananitambua

Hata tangu nianze ku utumia usafiri wa shabiby,sijawahi na ubaya alio nifanyia

Wakati mwingine ninasafiri na shabiby toka dodoma mpaka tunduma,dodoma arusha,dodoma dar,

Sijawahi kutana na tatizo hili

Ndio maana naishauri shabiby,wamchunguze huyu dereva

Nadhani ana shida
 
Wewe utakuwa kanjanja tu usikute ulikuwa unataka kuwaibia abiria,ilishindikana vipi kumuachia mtu yoyote hilo lispika nje mpaka uingie nalo ndani ya basi hovyo sana wewe.
 
Shabiby sio tatizo,ila huyu dereva,maana hata ushahidi wa sababu ya mimi kuingia ndani ya basi nilimwonyesha,ila hakutaka kunielewa

Hata hivyo mimi ndie nilikuwa namsafirisha mke wangu,

Shida ni huyu dereva,maana ni mteja ambaye nikitokea hapa jijini arusha ,hata wafanya kazi wa shabiby ofisini,wananitambua

Hata tangu nianze ku utumia usafiri wa shabiby,sijawahi na ubaya alio nifanyia

Wakati mwingine ninasafiri na shabiby toka dodoma mpaka tunduma,dodoma arusha,dodoma dar,

Sijawahi kutana na tatizo hili

Ndio maana naishauri shabiby,wamchunguze huyu dereva

Nadhani ana shida
Yaani katka Hali ya kawaida umeenda kutaka kuingia ndani ya Basi, dereva akakukataza (maybe alishaanza kuondoka) Simply ilitakiwa umwite Wife umpe hiyo hela ya matumizi then ushuke story ingekuwa imeishia hapo, sasa inaonekana na wewe ulikomaa tu uingie kilazima huku umebeba mi speaker yako hiyo lazma angekukazia.
Halafu km tatizo ingekuwa dereva Tu na kondakta umesema wanakujua Basi wangekutetea lakini umesema na wao wamechangia kukukunja vizuri na kukudhibiti ili usilete jeuri hii inaonesha ulishaanza kuwa na kiburi na kuleta rabsha hapo kitu ambacho lazma wangekubananisha tu.

Mkuu sehemu Kama zile zingatia Sana "Appearance" ulikuwa ktk mwonekano gani mpk wakashindwa kukuelewa unachowaeleza na kuamua kukudhalilisha??? Kama ulikuwa rafu ktk namna ambayo hata abiria wanakutilia shaka hawatakusapoti kwa shida yako.

Lugha uliyokuwa unatumia kuelezea shida yako huenda haikua ya kistaarabu. Kumbuka ile haikua haki yako we kuingia mana si abiria hivyo ulikuwa ni ombi TU unaomba usaidiwe
Baada ya kushindikana ulitakiwa uangalie option ya pili kumwita wife aje umpe hiyo hela Au hata kumpa konda ampe hapo, hata hii ilishindikana?

Mkuu kwa hicho kilichotokea juu yako peke yake hakitoshi kuwalaumu shabiby na kuwaona hawafai .... kampuni hiyo naweza sema ndio pekee iliyokua serious zaidi katika kutoa huduma In a profeshno way sasa we tena unawadis kwa hiyo sababu ndogo TU. We kubali kwamba na wewe una makosa katka hicho kilichotokea na pole kwa inconvenience uliyoipata.
 
Haya maneno ya dharau na kebehi yanashangaza sana.
Kampuni inaweza ikawa nzuri lakini mtu mmoja tu akaichafua.
Kimsingi mleta hoja amedhalilika. Kwanini huyo dereva hakutumia busara kumsikiliza na kumsaidia?
Masala ya kusukumana ni ya kizamani. Kiukweli, baadhi ya wahudumu kwenye mabasi hawatambui wajibu wao kama watoa huduma.
Hali hii ipo na kwenye biashara nyingine. Angekuwa muhusika amevaa suti na Tai asingebughudhiwa. Tujenge tabia ya kuheshimu watu.
Pole sana
 
Back
Top Bottom