HISIA KALI
JF-Expert Member
- Oct 26, 2010
- 694
- 108
Nimesoma habari kwenye gazeti la Mwananchi yenye kichwa ``Kampuni saba zaomba kuingiza mafuta nchini``. mimi hili linanisumbua kwa kiasi fulani.
Kati ya hizo kampuni saba ni moja tu ambayo ni ya ndani ya nchi. Kampuni mbili zinatoka Bahamas, tatu zinatoka Singapore na moja Geneva Uswisi.
Nina wasiwasi na hizi kampuni kutokana nchi zilikotoka. Bahamas na Uswisi ni tax haven countries. Kwa kifupi watu ambao wanasajili kampuni zao kwenye tax haven countries ni wale ambao hawapendi kulipa kodi na wanafanya biashara za kuficha ficha. Sasa Tanzania ina imani gani na watu kama hawa mpaka itake kuwakabidhi biashara nyeti ya mafuta.
Tukiachana na hilo naoni ni vyema tukajiuliza hivi serikali imeshindwa kuitumia TPDC kuagiza mafuta? Mafuta ni bidhaa nyeti kwa uchumi na usalama wa Taifa kwa ujumla. Hivyo basi sio vyema hata kidogo kuipa kampuni moja au hata tatu za binafsi kufanya biashara ya kuagiza mafuta kutoka nje ya nchi. Tulishuhudia hivi karibu wafanyabiashara wa mafuta walipogoma kuuza mafuta jinsi nchi ilivyoadhirika. Hawa waliogoma walikuwa wengi sasa je tukimpa mmoja au wachache itakuwaje? Si ndio itakuwa rahisi kwa wao kuamua kufanya chochote kwa sababu watakuwa na nguvu sana kwenye biashara ya mafuta.
Kwa hitimisho nasema biashara ya mafuta ni suala nyeti kwa uchumi na usalama wa taifa hivyo sio vyema kuwategemea watu binafsi kwa asilimia mia moja kuagiza mafuta nje. Nashauri serikali iitumie TPDC kufanya kazi ya kuagiza mafuta nchi. Kama serikali inaona ni kazi kubwa basi hiyo kazi igawenywe nusu kwa nusu. Nusu TPDC na nusu kampuni binafsi.
Tukumbuke tu suala la mafuta ni nyeti kupita hata suala la umeme. Mafuta yanatumika hata sehemu ambayo umeme haupo. Pia mafuta ndio yanatumika kuzalisha umeme kwa kiasi fulani.
Kati ya hizo kampuni saba ni moja tu ambayo ni ya ndani ya nchi. Kampuni mbili zinatoka Bahamas, tatu zinatoka Singapore na moja Geneva Uswisi.
Nina wasiwasi na hizi kampuni kutokana nchi zilikotoka. Bahamas na Uswisi ni tax haven countries. Kwa kifupi watu ambao wanasajili kampuni zao kwenye tax haven countries ni wale ambao hawapendi kulipa kodi na wanafanya biashara za kuficha ficha. Sasa Tanzania ina imani gani na watu kama hawa mpaka itake kuwakabidhi biashara nyeti ya mafuta.
Tukiachana na hilo naoni ni vyema tukajiuliza hivi serikali imeshindwa kuitumia TPDC kuagiza mafuta? Mafuta ni bidhaa nyeti kwa uchumi na usalama wa Taifa kwa ujumla. Hivyo basi sio vyema hata kidogo kuipa kampuni moja au hata tatu za binafsi kufanya biashara ya kuagiza mafuta kutoka nje ya nchi. Tulishuhudia hivi karibu wafanyabiashara wa mafuta walipogoma kuuza mafuta jinsi nchi ilivyoadhirika. Hawa waliogoma walikuwa wengi sasa je tukimpa mmoja au wachache itakuwaje? Si ndio itakuwa rahisi kwa wao kuamua kufanya chochote kwa sababu watakuwa na nguvu sana kwenye biashara ya mafuta.
Kwa hitimisho nasema biashara ya mafuta ni suala nyeti kwa uchumi na usalama wa taifa hivyo sio vyema kuwategemea watu binafsi kwa asilimia mia moja kuagiza mafuta nje. Nashauri serikali iitumie TPDC kufanya kazi ya kuagiza mafuta nchi. Kama serikali inaona ni kazi kubwa basi hiyo kazi igawenywe nusu kwa nusu. Nusu TPDC na nusu kampuni binafsi.
Tukumbuke tu suala la mafuta ni nyeti kupita hata suala la umeme. Mafuta yanatumika hata sehemu ambayo umeme haupo. Pia mafuta ndio yanatumika kuzalisha umeme kwa kiasi fulani.