R.B
JF-Expert Member
- May 10, 2012
- 6,296
- 2,571
KAMPUNI ya China Merchant Holdings kutoka China, iliyoletwa na aliyekuwa Waziri wa Uchukuzi, Omary Nundu ili iwekeze kwenye mradi mkubwa wa ujenzi wa gati mbili kwenye Bandari ya Dar es Salaam na Bandari mpya ya Mwambani, imeibuka tena.
Kampuni hiyo, ambayo ilikumbana na vikwazo vingi, inadaiwa kurejeshwa kiaina safari hii kama mwekezaji mpya kupitia Ofisi ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji).
Awali kampuni hiyo iliyodaiwa kupigiwa chepuo na Nundu hadi kufikia hatua ya kutofautiana kwa kiasi kikubwa na menejimenti ya TPA, Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, ilisababisha Nundu kupoteza nafasi yake ya uwaziri, kutokana na kiwingu kilichoonekana kuwa kama Serikali ingekubali kuendelea na mwekezaji huyu kwa masharti aliyotaka, taifa lisingepata maslahi yoyote.
Mwekezaji huyo, alitaka ajenge kwa fedha zake na kuendesha mradi huo kwa miaka 43, kisha akabidhi bandari kwa TPA. Lakini itakumbukwa menejimenti ya TPA na bodi yake, walipendelea mradi huo ufanywe kwa mkopo, kutoka kwenye benki ya Exim ya China au kutoka kwa benki nyingine yoyote yenye masharti nafuu.
Benki ya Exim ya China, ilikubali kutoa mkopo na kupendekeza Kampuni ya China Construction Company (CCCC), ifanye upembuzi yakinifu, huku mkopo huo ungekuwa wa miaka 15, ikiwa ni pamoja na grace period ya miaka mitatu kabla ya kuanza kulipa.
Ilidaiwa Nundu, alidai Kampuni ya CCCC ilipendekezwa na mkopeshaji Exim Benki, bila kushindanishwa.
Cha kushangaza tumeona Waziri Nagu, akiueleza umma kuwa, kampuni ya China Merchant Holdings, inakuja kuwekeza kwenye ujenzi wa Bandari ya Mbegani..Bagamoyo bila kushindanishwa na kampuni nyingine yoyote na wala masharti ya uwekezaji huo hayajawekwa wazi, kilisema chanzo chetu.
Na kama ni Serikali inakopa kwa ajili ya mradi huu mkubwa ambao ni zaidi ya dola za Marekani bilioni 7, ni vema Waziri Nagu au waziri wa Uchukuzi, Dk. Mwakyembe akaliweka wazi zaidi.
Habari za kuaminika zilizopatikana jana kutoka ndani ya Wizara ya Uchukuzi, zinasema tayari makubaliano ya awali yamefikiwa kwa Kampuni ya China Merchant Holdings, kwa ajili ya mradi huo. MTANZANIA ilimtafuta Waziri Nagu kupitia simu yake ya kiganjani, lakini iliita bila kupokelewa
Kampuni hiyo, ambayo ilikumbana na vikwazo vingi, inadaiwa kurejeshwa kiaina safari hii kama mwekezaji mpya kupitia Ofisi ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji).
Awali kampuni hiyo iliyodaiwa kupigiwa chepuo na Nundu hadi kufikia hatua ya kutofautiana kwa kiasi kikubwa na menejimenti ya TPA, Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, ilisababisha Nundu kupoteza nafasi yake ya uwaziri, kutokana na kiwingu kilichoonekana kuwa kama Serikali ingekubali kuendelea na mwekezaji huyu kwa masharti aliyotaka, taifa lisingepata maslahi yoyote.
Mwekezaji huyo, alitaka ajenge kwa fedha zake na kuendesha mradi huo kwa miaka 43, kisha akabidhi bandari kwa TPA. Lakini itakumbukwa menejimenti ya TPA na bodi yake, walipendelea mradi huo ufanywe kwa mkopo, kutoka kwenye benki ya Exim ya China au kutoka kwa benki nyingine yoyote yenye masharti nafuu.
Benki ya Exim ya China, ilikubali kutoa mkopo na kupendekeza Kampuni ya China Construction Company (CCCC), ifanye upembuzi yakinifu, huku mkopo huo ungekuwa wa miaka 15, ikiwa ni pamoja na grace period ya miaka mitatu kabla ya kuanza kulipa.
Ilidaiwa Nundu, alidai Kampuni ya CCCC ilipendekezwa na mkopeshaji Exim Benki, bila kushindanishwa.
Cha kushangaza tumeona Waziri Nagu, akiueleza umma kuwa, kampuni ya China Merchant Holdings, inakuja kuwekeza kwenye ujenzi wa Bandari ya Mbegani..Bagamoyo bila kushindanishwa na kampuni nyingine yoyote na wala masharti ya uwekezaji huo hayajawekwa wazi, kilisema chanzo chetu.
Na kama ni Serikali inakopa kwa ajili ya mradi huu mkubwa ambao ni zaidi ya dola za Marekani bilioni 7, ni vema Waziri Nagu au waziri wa Uchukuzi, Dk. Mwakyembe akaliweka wazi zaidi.
Habari za kuaminika zilizopatikana jana kutoka ndani ya Wizara ya Uchukuzi, zinasema tayari makubaliano ya awali yamefikiwa kwa Kampuni ya China Merchant Holdings, kwa ajili ya mradi huo. MTANZANIA ilimtafuta Waziri Nagu kupitia simu yake ya kiganjani, lakini iliita bila kupokelewa