Timm Wu
JF-Expert Member
- Dec 16, 2018
- 505
- 1,360
Wakenya wanamfahamu Brian Mutembei kama mtu mjanja mjanja tu wa mjini - mithili ya akina Jerry Murro au Le Mutuz au Cyprian Musiba hivi - yan ni kama umchukue Le Mutuz umvalishe suti halaf ukusanye serikali nzima ya Kenya on live TV uwasainishe Mkataba Feki wa kununua mavuno yote ya zao la Chai ya Kenya kwa mwaka 2018.
Sasa ndo narudi kwenye swali langu, kwanini huyu Waziri mjanja mjanja Palamaganda Kabudi na wenzake Kakunda na Hasunga hawajawajibishwa mpaka sasa pamoja na kumdhalilisha Rais kwa kiwango hiki? Au hii kampuni ya INDO WHO? kama wanavyoiita Wakenya ni jipu la Ikulu moja kwa moja na kwa hiyo kuwawajibisha akina Kabudi itakuwa ni kuwaonea?