Uchaguzi 2020 Kampeni zinaenda kuisha. Sijasikia neno "haki" na "uhuru wa watu" likitamkwa na mgombea Urais CCM

kagoshima

JF-Expert Member
Dec 31, 2015
2,629
5,134
Ni jambo la kushangaza sana kwangu. Sijasikia popote akilaumu uvunjwaji wa haki za watu yanayofanywa na vikundi vya watu wasiojulikana.

Sijamsikia akikemea unambikiaji watu kesi kwa mashitaka ya uongo

Sijamsikia akikemea manyanyaso kwa waandishi wa habari hata kuonesha sympathy ya wandishi waliopotea wakiwa kazini au kuahidi kurudisha Uhuru halisi wa vyombo vya habari.

Ninachokisikia ni msipo nichagua sileti hiki sileti kile .

Sioni matumaini yoyote ya ustawi na Uhuru wa watu toka kwa mgombea wa CCM.
 
Kumetokea ajali Jana cjamsikia Lissu akitoa hata salamu za pole wakati wamepoteza maisha zaidi ya watu 15!

Wewe kujiunga jf nani alikushikia mtutu? Kuanzisha post hii nani kakulazimisha?

Endelea kungoja uongozi wa Lissu utakaokufanya uishi kama upo peponi!

Kuna wakati utajiuliza kwa nn Mwenyezi Mungu hakutuumba watu wote kuwa na upeo wa kung'amua kwa aina moja? Usinipe jibu!
 
umemsikia hashim rungwe na maganja wa nccr wakitoa pole au Shibuda wa ada tadea,
au unawashwa washwa na lissu?

pole inasaidia nini?

namna bora ya kuwafariji wafiwa ni kupeleka rambirambi na kuwa nao kipindi chote cha msiba mpaka kuzika,
namna bora ya kuwapa pole majeruhi ni kuwalipia gharama za matibabu mpaka wataporusiwa.
.je mgombea wako magu amefanya hayo???


kupost mtandaoni eti nimesikitishwa sana natoa pole hakusaidii chochote yeye akiwa kama mfariji wa taifa anapaswa kufanya zaidi.

Kumetokea ajali Jana cjamsikia Lissu akitoa hata salamu za pole wakati wamepoteza maisha zaidi ya watu 15!

Wewe kujiunga jf nani alikushikia mtutu? Kuanzisha post hii nani kakulazimisha?

Endelea kungoja uongozi wa Lissu utakaokufanya uishi kama upo peponi!

Kuna wakati utajiuliza kwa nn Mwenyezi Mungu hakutuumba watu wote kuwa na upeo wa kung'amua kwa aina moja? Usinipe jibu!
 
KURA ZA UBUNGE NA URAISI ZITASAFIRISHWA KWENDA KUHESABIWA JIMBONI, HAZITAHESABIWA KWENYE VITUO VYA KUPIGIA KURA

KURA ZA UDIWANI ZITASAFIRISHWA KWENDA KUHESABIWA MAKAO MAKUU YA KATA (KATANI)

WAPINZANI HAMPATI KITU.

KUWENI MAKINI
 
Magufuli anatumia nguvu kubwa kujenga taifa la waoga wasioweza kuhoji viongozi wao wanapokosea, rais wa namna hii hatufai kura zetu zote tunampa lissu
 
Haki gani unataka itamkwe?
-Haki ya kuishi
-Haki ya kupata maendeleo bila kubaguliwa.
-Haki ya kulipwa stahiki zangu za mafao kwa wakati, nyongeza ya mishahara nk.
-Haki ya kuona bunge live.
-Haki ya kufanya biashara bila kufuatwa fuatwa na TRA...
-Haki ya wanawake weusi kusikilizwa...
-Haki ya kuendelea na masomo kwa mtoto wa kike aliyepewa mimba..
-Haki ya kuuza mazao yangu popote ninapotaka....
-Haki ya kumchagua kiongozi ninayemtaka.
-Haki ya kuwa mfuasi wa chama cha upinzani bila kubughudhiwa.
-Haki ya kuandamana...
-Haki ya kuipinga na kuikosoa serikali iliyopo madarakani....
-Haki ya kupewa dhamana...
 
Ni jambo la kushangaza sana kwangu. Sijasikia popote akilaumu uvunjwaji wa haki za watu yanayofanywa na vikundi vya watu wasiojulikana.

Sijamsikia akikemea unambikiaji watu kesi kwa mashitaka ya uongo

Sijamsikia akikemea manyanyaso kwa waandishi wa habari hata kuonesha sympathy ya wandishi waliopotea wakiwa kazini au kuahidi kurudisha Uhuru halisi wa vyombo vya habari.

Ninachokisikia ni msipo nichagua sileti hiki sileti kile .

Sioni matumaini yoyote ya ustawi na Uhuru wa watu toka kwa mgombea wa CCM
Tuna kiongozi ambaye mambo ya haki si suala linalomgusa, tuachane naye ni mkatili sana.
 
Hilo lilishafanywa kabla ya 1961
Ni jambo la kushangaza sana kwangu. Sijasikia popote akilaumu uvunjwaji wa haki za watu yanayofanywa na vikundi vya watu wasiojulikana.

Sijamsikia akikemea unambikiaji watu kesi kwa mashitaka ya uongo

Sijamsikia akikemea manyanyaso kwa waandishi wa habari hata kuonesha sympathy ya wandishi waliopotea wakiwa kazini au kuahidi kurudisha Uhuru halisi wa vyombo vya habari.

Ninachokisikia ni msipo nichagua sileti hiki sileti kile .

Sioni matumaini yoyote ya ustawi na Uhuru wa watu toka kwa mgombea wa CCM
 
Back
Top Bottom