Mheikungu
JF-Expert Member
- Oct 15, 2018
- 214
- 448
Heshima na taadhima kwenu wakuu.
Nimekaa naangalia runinga hapa kwenye kituo cha Star Tvkipindi kinaitwa Agenda 2020. Anahojiwa Waitara hapa naona kichefuchefu:
1. Anaonekana amelewa chakari, kimaadili kwa kiongozi kama yeye alipaswa aheshimu maadili ya hadhira kwa ujumla.
2. Kwa kutumia kofia ya unaibu waziri ametangaza kuachana na jimbo la Ukonga. Ametangaza rasmi kuwa anaenda kugombea jimbo la Tarime vijijini.
Kwangu mimi hii naona ni kampeni ya wazi kabisa. Kwa sasa jambo ambalo linawanyima haki raia wengine wenye kutaka kutia nia lakini hawana uwezekano wa kuonekana runingani.
Naomba nijuzwe labda nipo nyuma ya wakati kama kampeni zimefunguliwa na mimi nikatangaze nia huko Mchambawima kwetu.
Nimekaa naangalia runinga hapa kwenye kituo cha Star Tvkipindi kinaitwa Agenda 2020. Anahojiwa Waitara hapa naona kichefuchefu:
1. Anaonekana amelewa chakari, kimaadili kwa kiongozi kama yeye alipaswa aheshimu maadili ya hadhira kwa ujumla.
2. Kwa kutumia kofia ya unaibu waziri ametangaza kuachana na jimbo la Ukonga. Ametangaza rasmi kuwa anaenda kugombea jimbo la Tarime vijijini.
Kwangu mimi hii naona ni kampeni ya wazi kabisa. Kwa sasa jambo ambalo linawanyima haki raia wengine wenye kutaka kutia nia lakini hawana uwezekano wa kuonekana runingani.
Naomba nijuzwe labda nipo nyuma ya wakati kama kampeni zimefunguliwa na mimi nikatangaze nia huko Mchambawima kwetu.