Kampeni za mwisho za Monduli na Lowassa

Nicksixyo

JF-Expert Member
Jan 11, 2011
944
263
Hii ndio kampeni ya mwamba wa kaskazini akiwa kwenye himaya yake katika kampeni za uchaguzi wa serikali za mitaa ndani ya mji wa Monduli. Idadi wa wananchi ndio kama uonavyo, wengi wakiwa wameletwa na malori na landrover kutoka mto wa mbu na makuyuni. Watu wanazomea kama kawa. Sare ya chama inaendelea kugawanywa kwa wasio na t-shirt za kubadilisha wanajisevia. Bodaboda zikizurura na bendera katika viunga vya mji wakijipatia kipato cha siku. Nawasilisha. ImageUploadedByJamiiForums1418472200.161916.jpg ImageUploadedByJamiiForums1418472223.654468.jpg ImageUploadedByJamiiForums1418472241.637416.jpg ImageUploadedByJamiiForums1418472264.400468.jpg
 
Hali ni tete kwa kweli. Nasikitikia chama cha Escrow kinakufa taratibu. Rais mtarajiwa amesimama na kunadi wagombea waliopatikana kwa uchakachuaji ndani ya chama, watu wanazomea balaaa.
 
Hali ni tete kwa kweli. Nasikitikia chama cha Escrow kinakufa taratibu. Rais mtarajiwa amesimama na kunadi wagombea waliopatikana kwa uchakachuaji ndani ya chama, watu wanazomea balaaa.
Sasa kama wanazomea walifuata nini hapo? Hawana kazi za kufanya?
 
Hizi kampeni ni hasira tupu,
Jana pale kijijini kwetu walihitimisha kwa shamra shamra na nderemo,
vyakula vilipikwa, nguo, kanga ziligawanywa.

Risala za kashfa zilisikika ili mradi ni hasira tu.

.................. by the way ....... umekuja kwa ajili ya kupiga kura?
 
Sasa kama wanazomea walifuata nini hapo? Hawana kazi za kufanya?

kama wamonduli wanaamini monduli ni ngome yao ccm kama anavyoamini mtakatifu wao wasingekuwa wanafanya hujuma kwa wagombea wa vyama vya upinzani kama ilivyokuwa kwa uchaguzi huu. hajawahi tokea mh. anahudhuria kampeni serikali za vijiji, ni kweli wamatambua UKAWA ipo...!! Wapo kazini maana hapo idadi kubwa ni wafanya biashara wa sokoni, na mkutano umefanyikia eneo la soko na pamezungukwa na hotel na bar kwa jirani. So usidhani wamekuja kwa sababu ya mkutano, la hasha ni mkutano umeingilia eneo la shughuli zao kutafuta idadi. Kumbe idadi badala ya kushangilia kampeni inazomea kampeni. Mia.
 
Hizi kampeni ni hasira tupu,
Jana pale kijijini kwetu walihitimisha kwa shamra shamra na nderemo,
vyakula vilipikwa, nguo, kanga ziligawanywa.

Risala za kashfa zilisikika ili mradi ni hasira tu.

.................. by the way ....... umekuja kwa ajili ya kupiga kura?

Hapana nipo kwa likizo, nilikuwa napita zangu kwenda tafuta nyama choma na moja mbili bariiidi nikajikuta nipo katikati ya zomea zomea.
............. By the way ........ Haujambo?
 
Ok fine,
............ just fine ...... malaria.........
Hapana nipo kwa likizo, nilikuwa napita zangu kwenda tafuta nyama choma na moja mbili bariiidi nikajikuta nipo katikati ya zomea zomea.
............. By the way ........ Haujambo?
 
Wengi wawaliosema ccm hoyeeee hoyeee hawajapiga hata kura leo na makofia yao wapo mtaani wanazurura. Nilitembelea vituo kadhaa watu daah wachache mnoo.
 
Back
Top Bottom