Kampeni za marudio Jimbo la kinondoni,na siha zitumike kuelimisha wananchi kazi ya mbunge

lendila

JF-Expert Member
Sep 26, 2012
5,806
4,370
Kuna kampeni za chaguzi ndogo za Kinondoni,na siha zitumike kuelimisha wananchi kazi ya mbunge
Wananchi waambiwe kabisa kazi ya mbunge sio kumuunga mkono rais,kazi ya mbunge ni kutunga Sheria,kuisimamia serekali,na kuiwajibisha serekali,kupanga bajeti,sera,na kadhalika,wananchi waelimishe kuwa bunge ni muhimili unajitegemea,kati ya mihimili 3 ya dola,hiki ndio kipindi kizuri cha kuwaelimisha watu,kuhusu mihimili 3 ya dola,na jinsia Kila muhimil unatakiwa kutekeleza majukumu yake,haiwezeka jaji mkuu aache kazi yake,kwa hoja ya kumuunga mkono rais Kwa kazi nzuri,haiwezekani spika aache usipika Kwa hoja ya kazi nzuri ya mh,rais,hiki ni kituko,vyama vitumie jukwaa hili la kampeni kuelimisha wananchi Kwa ufasaa kazi za mbunge mmoja mmoja,na kazi za bunge kama taasisi,hii itakomesha watu wenye tabia za kishithole kutokutokea tena ndani ya bunge letu la jamhuri ya nyumbani
Ni maajabu ya Dunia padri kuacha kazi Kwa hoja ya kumuunga mkono askofu mkuu,au Mwl,kuacha kazi yake kwa hoja ya kumuunga mkono mwl,mkuu,huku ni kuwaona watanzania kama mazumbukuku yasiyo na akili
 
9abf0922d31847375641647639564ad5.jpg
 
Back
Top Bottom