Jana tar. 29 Januari, 2018 Kampeni za Mgombea Ubunge Jimbo la Siha kupitia Chama Cha Mapinduzi Dr. Godwin Mollel ziliendelea kushika kasi ambapo mgeni rasmi Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Mh. Humphrey Polepole amemnadi Mgombea Ubunge Jimbo la Siha na Mgombea Udiwani. Miongoni mwa changamoto ambazo Dr. Mollel ameahidi kuzifanyia kazi mara tu atakapochaguliwa kuwa Mbunge ni migogoro ya ardhi, ukosefu wa ardhi ya kilimo na mifugo na Ndg. Polepole ameahidi kumpatia ushirikiano wa kutosha katika kuwaletea Maendeleo wanaSiha na kutatua Changamoto mbalimbali zinazowakabili mara tu baada ya kuchaguliwa kuwa Mbunge. Wakati huohuo Mh. Polepole amewapokea wanachama wanachama wapya ambao wameikacha CHADEMA na kukabidhi kadi zao na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi kwa madai ya kuchoshwa na propaganda nyingi ndani ya CHADEMA na kuamua kuunga mkono Juhudi za Mh. Rais Magufuli za Kuwaletea Maendeleo Watanzania.
Kidumu Chama Cha Mapinduzi.
Robert PJN Kaseko
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Arusha.
Januari 30, 2018.
Kidumu Chama Cha Mapinduzi.
Robert PJN Kaseko
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Arusha.
Januari 30, 2018.