Jana nilibahatika kukutana na kiongozi mmoja wa CCM wa eneo la Ilala National Housing /Msimbazi, nikawa namcharura kuhusu mikutano yao ya kubeba watu na mabasi zaidi ya 17 kuwapeleka kusikiliza kampeni za JK kama walivyofanya pale Mbagala Zakhem siku mgonjwa JK alipohutubia. Akanijibu mbona hata wapinzani wanafanya mbinu hiyo, any way sikubisha sana kwa sababu nilikuwa sina data hizo. Katika maongezi yetu mafupi pia nilimlaumu kuwavalisha boda-boda fulana za CCM halafu kuwalipa kwa kuwajazia vimafuta kidogo.
Jambo ambalo hasa lilinishangaza na hasa ndio sababu ya kuandika ujumbe huu, huyu mheshimiwa wa CCM alinionesha karatasi (ratiba ndefu) iliyochapishwa ya majina ya kaya alizonazo katika eneo lote la Ilala mchikichini mpaka kule buguruni yenye ratiba ya siri ya kuwapitia hawa watu Nyumba kwa Nyumba kufanya kampeni, ratiba ilionesha muda wa kuanzia saa moja usiku na wakati mwingine anasema wakiona kuwa huo muda kuna watu wengi ambao wanaweza kuwaona wanafanya saa saba au nane za usiku. Nilitamani nimuibie hiyo ripoti lakini naye akawa mjanja akaniambia angalia tu jinsi tunavyojidhatiti kuumaliza upinzani.
Sikujua kama CCM ina aina hii ya kampeni, swali: Je ratiba hii tume wanayo?
Jambo ambalo hasa lilinishangaza na hasa ndio sababu ya kuandika ujumbe huu, huyu mheshimiwa wa CCM alinionesha karatasi (ratiba ndefu) iliyochapishwa ya majina ya kaya alizonazo katika eneo lote la Ilala mchikichini mpaka kule buguruni yenye ratiba ya siri ya kuwapitia hawa watu Nyumba kwa Nyumba kufanya kampeni, ratiba ilionesha muda wa kuanzia saa moja usiku na wakati mwingine anasema wakiona kuwa huo muda kuna watu wengi ambao wanaweza kuwaona wanafanya saa saba au nane za usiku. Nilitamani nimuibie hiyo ripoti lakini naye akawa mjanja akaniambia angalia tu jinsi tunavyojidhatiti kuumaliza upinzani.
Sikujua kama CCM ina aina hii ya kampeni, swali: Je ratiba hii tume wanayo?