kampeni ni leo ya washia ya kuchangaia benki ya damu salama ni ya kujenga umoja wa kitaifa

KAZIMOTO

JF-Expert Member
Aug 19, 2010
1,073
324
Leo ni simu ya waislamu wa madhehebu ya washia wakimkumbuka mjukuu wa mtume Mohammed (S.A.W).

Washia wametumia siku ya leo kutoa damu salama kwa benki ya damu ya taifa. Damu hii itazambazwa kuokoa watanzania wote bila kujali dini zao na hata wale wasio na dini.

Benki ya damu salama inahitaji damu lita laki sita kwa mwaka kwa matumizi ya nchi nzima.

Tukumbuke damu ya washia itapelekwa hadi kwenye hospitali za kanisa, hospitali binafsi na serikali zikiwatibu watanzania wote.

My take: Wanaharakati akina Ponda wanatakiwa kujifunza kitu.Kulalamika tu kila siku bila angalau kujitokeza kufanya jambo jema kwa watu wote bila kujali dini zao ni kumpendeza mwenyezi Mungu pia.

Washia hao wameonyesha kwamba vazi haliwezi kuwatenganisha na dunia ingine wengi wameandamana wakiwa wamevaa suti nyingi kuliko kanzu. Hii inaonyesha kuwa mavazi hayawezi kutufarakanisha.

source: ITV na Star TV taarifa ya habari saa 2 usiku huu.
 
mods kichwa cha habari kisomeke.

kampeni ya leo ya washia ya kuchangia benki ya damu salama ni ya kujenga umoja wa kitaifa
 
Back
Top Bottom