Zanzibar 2020 Kampeni, 2020 Zanzibar. Tunamtaka Dkt. Mwinyi aje hapa uwanjani

KISHADA

JF-Expert Member
Oct 18, 2012
2,224
3,290
Naam hiki ni kipindi mujarabu sana.

Kampeni zinaendelea kwa kasi kote Bara na Zanzibar.

Leo Tunamwita Dkt. Mwinyi ama timu yake aje hapa ama waje uwanjani.

Tunahitaji tujibiwe baadhi ya masuali yetu muhimu kuhusu Mwelekeo wa sera za CCM na msimamo wa Dkt Mwinyi.

Dkt Kule Zanzibar unaitwa uwajibu haya maswali na nadhani yatakuongezea murua wako na kutathminiwa ili upate kuungwa mkono.

MASWALI

1. Wazanzibari wengi wanataka kujua msimamo wako juu ya Muungano wa serikali tatu au Mkataba ili Zanzibar ipate hadhi, uwezo na nguvu za kujiletea Maendeleo yake baada ya miaka zaidi ya 50 ya Muungano wa serikali mbili bila mafanikio yaliyokusudiwa. Nini msimamo wako kuhusu hili? .

2. Umezungumzia sera ya Uchumi ya Blue na kuahidi Wazanzibari kunufaika na Mafuta. Kwanza Rasilimali za Mafuta na Bahari Kuu ni mali ya Muungano hili unalijuwa. Wazanzibari wanahitaji kuyamiliki mafuta yao na Bahari yao jee uko tayari kuhakikisha Zanzibar inamiliki rasilimali ya Mafuta na bahari kwa kuondoa sheria zinazotoa umiliki kwa Jamuhuri ya Muungano badala ya Zanzibar kama nchi?

3. Tunajuwa kwa sasa CCM na chama chako kinatambua uwepo wa serikali mbili kuelekea moja. Jee utakuwa tayari kusikiliza maoni ya wazanzibari wengi kuhusu Muungano wautakao au utasimamia msimamo wa CCM ?

4. Katiba ya Zanzibar inatambua Zanzibar kama nchi yenye mipaka yake ile iliyokuwepo kabla ya Mapinduzi na inatambuwa muundo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa pamoja Rais wa Zanzibar kuwa na uwezo wa kuigawa Mipaka ya Mikoa na Wilaya. Unawahakikishia vipi Wazanzibari juu ya uwepo wa Zanzibar yao bila kugawanywa au kuwa nchi moja wakati CCM inatambuwa Serikali mbili kuelekea moja?

5. Huoni kampeni zako zina lengo la kuwahadaa wazanzibari wakati unajuwa fika aina ya Muungano uliopo hautoi fursa za Zanzibar kufunguka kiuchumi kutokana na kubanwa na ilani , katiba ya CCM na Sheria kadhaa za JMT? Uko tayari kupingana na CCM kwa maslahi ya Zanzibar?

6. Unawahikishia vipi Wazanzibari kuhusu Ubaguzi wa kiitikadi na ubaguzi wa ajira kwenye Serikali wakati unajuwa tatizo ni uhafidhina wa CCM. Uko tayari kupambana na wahafidhina kuhakikisha unaleta usawa Zanzibar?

MWISHO KWA LEO.

Tunaomba uje hapa uwanjani useme kinaga ubaga Wazanzibari wakusikie.


Kishada.
 
Zingatia kiapo, ni kuulinda Muungano ulioasisiwa..... kwa mujibu wa katiba!
 
Akishajibu hayo Maswali ajiandae tutapata walau kwa mbali kumpima kama kweli anastahiki kuchahuliwa.

Zanzibar tatizo ni CCM na sio mgombea. Hata aje nani ndani ya CCM basi kwenye Sanduku la Kura anagonga mwamba kitakachobaki ni Dola kuamua wampe nani. Hili hata Dkt Hussein analijua .
 
Naam hiki ni kipindi mujarabu sana.

Kampeni zinaendelea kwa kasi kote Bara na Zanzibar.

Leo Tunamwita Dkt. Mwinyi ama timu yake aje hapa ama waje uwanjani.

Tunahitaji tujibiwe baadhi ya masuali yetu muhimu kuhusu Mwelekeo wa sera za CCM na msimamo wa Dkt Mwinyi.

Dkt Kule Zanzibar unaitwa uwajibu haya maswali na nadhani yatakuongezea murua wako na kutathminiwa ili upate kuungwa mkono.

MASWALI

1. Wazanzibari wengi wanataka kujua msimamo wako juu ya Muungano wa serikali tatu au Mkataba ili Zanzibar ipate hadhi, uwezo na nguvu za kujiletea Maendeleo yake baada ya miaka zaidi ya 50 ya Muungano wa serikali mbili bila mafanikio yaliyokusudiwa. Nini msimamo wako kuhusu hili? .

2. Umezungumzia sera ya Uchumi ya Blue na kuahidi Wazanzibari kunufaika na Mafuta. Kwanza Rasilimali za Mafuta na Bahari Kuu ni mali ya Muungano hili unalijuwa. Wazanzibari wanahitaji kuyamiliki mafuta yao na Bahari yao jee uko tayari kuhakikisha Zanzibar inamiliki rasilimali ya Mafuta na bahari kwa kuondoa sheria zinazotoa umiliki kwa Jamuhuri ya Muungano badala ya Zanzibar kama nchi?

3. Tunajuwa kwa sasa CCM na chama chako kinatambua uwepo wa serikali mbili kuelekea moja. Jee utakuwa tayari kusikiliza maoni ya wazanzibari wengi kuhusu Muungano wautakao au utasimamia msimamo wa CCM ?

4. Katiba ya Zanzibar inatambua Zanzibar kama nchi yenye mipaka yake ile iliyokuwepo kabla ya Mapinduzi na inatambuwa muundo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa pamoja Rais wa Zanzibar kuwa na uwezo wa kuigawa Mipaka ya Mikoa na Wilaya. Unawahakikishia vipi Wazanzibari juu ya uwepo wa Zanzibar yao bila kugawanywa au kuwa nchi moja wakati CCM inatambuwa Serikali mbili kuelekea moja?

5. Huoni kampeni zako zina lengo la kuwahadaa wazanzibari wakati unajuwa fika aina ya Muungano uliopo hautoi fursa za Zanzibar kufunguka kiuchumi kutokana na kubanwa na ilani , katiba ya CCM na Sheria kadhaa za JMT? Uko tayari kupingana na CCM kwa maslahi ya Zanzibar?

6. Unawahikishia vipi Wazanzibari kuhusu Ubaguzi wa kiitikadi na ubaguzi wa ajira kwenye Serikali wakati unajuwa tatizo ni uhafidhina wa CCM. Uko tayari kupambana na wahafidhina kuhakikisha unaleta usawa Zanzibar?

MWISHO KWA LEO.

Tunaomba uje hapa uwanjani useme kinaga ubaga Wazanzibari wakusikie.


Kishada.

Maelezo yako yana kasoro na mapungufu kadhaa.

1. Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inamtaka Rais wa JMT na wabunge wake wote watakaochaguliwa, Kuapa kuutambua na kuulinda Muungano huo. Ndio maana moja ya Ahadi za Wagombea ni kuahidi kuulinda (KWA NGUVU ZAKE ZOTE)

2. Kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar, Mali asili za Mafuta na Gesi ndani ya visiwa hivyo ni mali ya Wananchi wa Zanzibar na JMT inatambua hilo. soma taarifa hii ya Balaza la Wawakili nimeambatanisha.


3. Suala la muundo wa Serikali ya Muungano ni la Kikatiba. Katiba haibadilishwi kisiasa na Rais au maamuzi ya upande mmoja wa Muungano. |Bali kwa mchakato na taratibu za kisheria za kubadili katiba.

4. Katiba ya Zanzibar inatambua uwepo wa Muungano na kuwa Zanzibar ni sehemu ya Muungano juo. Rais ni mtekelezaji wa Katiba ya Katiba.

5. Si mambo yote ya uendeshaji wa Serikali hizi mbili, ni mambo ya muungano. Rais wa Zanzibar ana mamlaka kwa mambo yote yasiyo ya Muungano.
 

Attachments

  • Pages from Baraza.pdf
    147.9 KB · Views: 12
Maelezo yako yana kasoro na mapungufu kadhaa.

1. Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inamtaka Rais wa JMT na wabunge wake wote watakaochaguliwa, Kuapa kuutambua na kuulinda Muungano huo. Ndio maana moja ya Ahadi za Wagombea ni kuahidi kuulinda (KWA NGUVU ZAKE ZOTE)

2. Kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar, Mali asili za Mafuta na Gesi ndani ya visiwa hivyo ni mali ya Wananchi wa Zanzibar na JMT inatambua hilo. soma taarifa hii ya Balaza la Wawakili nimeambatanisha.


3. Suala la muundo wa Serikali ya Muungano ni la Kikatiba. Katiba haibadilishwi kisiasa na Rais au maamuzi ya upande mmoja wa Muungano. |Bali kwa mchakato na taratibu za kisheria za kubadili katiba.

4. Katiba ya Zanzibar inatambua uwepo wa Muungano na kuwa Zanzibar ni sehemu ya Muungano juo. Rais ni mtekelezaji wa Katiba ya Katiba.

5. Si mambo yote ya uendeshaji wa Serikali hizi mbili, ni mambo ya muungano. Rais wa Zanzibar ana mamlaka kwa mambo yote yasiyo ya Muungano.
Mbona hakuna mnasaba wa majibu na maswali yaliyoulizwa. Wazanzibari wengi wanahitaji majibu. Huo Ni utetezi.
 
Mbona hakuna mnasaba wa majibu na maswali yaliyoulizwa. Wazanzibari wengi wanahitaji majibu. Huo Ni utetezi.
Majibu ndiyo hayo, ni uongo kusema Mafuta na Gesi ni suala la Muungano nimekuonyesha document.
Lakini pia Mgombea wa Urais wa Visiwani hawezi kuwa na majibu kwa maswala yanayohusu au yanayosimamiwa na serikali ya J/Muungano na ukiona mtu anajinasibu kufikiri anaweza kutengua suala kirahisi tu swala lolote linalohusu Muungano, anajifurahisha kwa sababu kuna taratibu zake kwa mujibu wa makubaliano na ulinzi wake uko mikononi mwa Rais wa Jamhuri ya Muungano. (KWA NGUVU ZOTE ALIZONAZO)
 
Majibu ndiyo hayo, ni uongo kusema Mafuta na Gesi ni suala la Muungano nimekuonyesha document.
Lakini pia Mgombea wa Urais wa Visiwani hawezi kuwa na majibu kwa maswala yanayohusu au yanayosimamiwa na serikali ya J/Muungano na ukiona mtu anajinasibu kufikiri anaweza kutengua suala kirahisi tu swala lolote linalohusu Muungano, anajifurahisha kwa sababu kuna taratibu zake kwa mujibu wa makubaliano na ulinzi wake uko mikononi mwa Rais wa Jamhuri ya Muungano. (KWA NGUVU ZOTE ALIZONAZO)
Haya masuala Ni magumu kwako ndugu Kifaurongo.

Kwa mfano hats kumjibia hilo suala LA tatu huwezi.

Jee mh atakuwa tayari kuunga mkono mawazo ya wazanzibari wengi kuhusu muungano wautakao au ataendelea ataunga mkono msimamo wa ccm mbili kuelekea moja?

Ikiwa huyamudu tafadhali yaache kama wenzako wanavyokuja kuchungulia na kuondoka kimya kimya.
 
Haya masuala Ni magumu kwako ndugu Kifaurongo.

Kwa mfano hats kumjibia hilo suala LA tatu huwezi.

Jee mh atakuwa tayari kuunga mkono mawazo ya wazanzibari wengi kuhusu muungano wautakao au ataendelea ataunga mkono msimamo wa ccm mbili kuelekea moja?

Ikiwa huyamudu tafadhali yaache kama wenzako wanavyokuja kuchungulia na kuondoka kimya kimya.
Uliza wenzio Rais Jumbe alitaka kuunga mkono mawazo ya wenye msimamo huo alipatwa na nini
 
Wazanzibari wanataka majibu ya hayo maswali.

Nje ya hapo Ni porojo zilizoboreshwa.
Watu walishaamka kitambo.

Maneno yoyote na ahadi zozote kwa mgombea wa ccm Ni bure. Miaka yote ndio hivyo. Wazanzibari wanataka mabadiliko ya kweli. Ccm imeshindwa kuitetea Zanzivar
 
Uliza wenzio Rais Jumbe alitaka kuunga mkono mawazo ya wenye msimamo huo alipatwa na nini
Sawa bas Ni wazi hawezi kuungwa mkono.

Aweke plan basi vipi ataondowa hivyo vikwazo.

Haya masuali hata Pole pole hapiti hapa
 
Uliza wenzio Rais Jumbe alitaka kuunga mkono mawazo ya wenye msimamo huo alipatwa na nini
Aliitwa Dodoma na kuvuliwa urais na akasimikwa mwengine... Mwinyi (alihongwa urais huyu hakuchaguliwa na wazanzibar)
Hivyo hata Mwinyi Jr akijaribu kuunga mkono mawazo ya wazanzibar ataitwa Dodoma na kuvuliwa uanachama mara moja. Suluhisho ni Maalim Seif pekee ndie anaweza kuwatetea wazanzibar maana Dodoma haitakuwa na uwezo wa kumvua uanachama na kumkosesha sifa za kuwa Rais.
Upinzani pekee ndio suluhisho la kutatua kero za Muungano either kwa kukubali serikali tatu au kuuvunja kabisa.
 
Naam hiki ni kipindi mujarabu sana.

Kampeni zinaendelea kwa kasi kote Bara na Zanzibar.

Leo Tunamwita Dkt. Mwinyi ama timu yake aje hapa ama waje uwanjani.

Tunahitaji tujibiwe baadhi ya masuali yetu muhimu kuhusu Mwelekeo wa sera za CCM na msimamo wa Dkt Mwinyi.

Dkt Kule Zanzibar unaitwa uwajibu haya maswali na nadhani yatakuongezea murua wako na kutathminiwa ili upate kuungwa mkono.

MASWALI

1. Wazanzibari wengi wanataka kujua msimamo wako juu ya Muungano wa serikali tatu au Mkataba ili Zanzibar ipate hadhi, uwezo na nguvu za kujiletea Maendeleo yake baada ya miaka zaidi ya 50 ya Muungano wa serikali mbili bila mafanikio yaliyokusudiwa. Nini msimamo wako kuhusu hili? .

2. Umezungumzia sera ya Uchumi ya Blue na kuahidi Wazanzibari kunufaika na Mafuta. Kwanza Rasilimali za Mafuta na Bahari Kuu ni mali ya Muungano hili unalijuwa. Wazanzibari wanahitaji kuyamiliki mafuta yao na Bahari yao jee uko tayari kuhakikisha Zanzibar inamiliki rasilimali ya Mafuta na bahari kwa kuondoa sheria zinazotoa umiliki kwa Jamuhuri ya Muungano badala ya Zanzibar kama nchi?

3. Tunajuwa kwa sasa CCM na chama chako kinatambua uwepo wa serikali mbili kuelekea moja. Jee utakuwa tayari kusikiliza maoni ya wazanzibari wengi kuhusu Muungano wautakao au utasimamia msimamo wa CCM ?

4. Katiba ya Zanzibar inatambua Zanzibar kama nchi yenye mipaka yake ile iliyokuwepo kabla ya Mapinduzi na inatambuwa muundo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa pamoja Rais wa Zanzibar kuwa na uwezo wa kuigawa Mipaka ya Mikoa na Wilaya. Unawahakikishia vipi Wazanzibari juu ya uwepo wa Zanzibar yao bila kugawanywa au kuwa nchi moja wakati CCM inatambuwa Serikali mbili kuelekea moja?

5. Huoni kampeni zako zina lengo la kuwahadaa wazanzibari wakati unajuwa fika aina ya Muungano uliopo hautoi fursa za Zanzibar kufunguka kiuchumi kutokana na kubanwa na ilani , katiba ya CCM na Sheria kadhaa za JMT? Uko tayari kupingana na CCM kwa maslahi ya Zanzibar?

6. Unawahikishia vipi Wazanzibari kuhusu Ubaguzi wa kiitikadi na ubaguzi wa ajira kwenye Serikali wakati unajuwa tatizo ni uhafidhina wa CCM. Uko tayari kupambana na wahafidhina kuhakikisha unaleta usawa Zanzibar?

MWISHO KWA LEO.

Tunaomba uje hapa uwanjani useme kinaga ubaga Wazanzibari wakusikie.


Kishada.

Hilo swali na.1 usipoteze kabisa muda wako. Sera ya CCM kuhusu Muungano iko wazi kabisa! Inasimamia mfumo wa Serikali mbili.
Hiyo sera ya mfumo wa serikali tatu ni ya CUF/UKAWA na sasa ACT-Wazalendo!
 
Hilo swali na.1 usipoteze kabisa muda wako. Sera ya CCM kuhusu Muungano iko wazi kabisa! Inasimamia mfumo wa Serikali mbili.
Hiyo sera ya mfumo wa serikali tatu ni ya CUF/UKAWA na sasa ACT-Wazalendo!
Wewe Ni Dkt Mwinyi mwenyewe au Ni mwanakampeni?

Zanzibar inaathiriwa na mfumo wa Muungano ili kufikia maendeleo yake ya kweli. Hizo zengine Ni advanced propaganda.

Hakuna political freedom, hakuna economical freedom, hakuna legal freedom ambapo wataweza kujiamulia mambo yao. Mfumo wote Ni controlled in favour na nini Tanganyika INA taka kwa jina LA Muungano.

Utopolo wowote bila kwanza kuwa wazi kwa hili jambo Ni bure. Sera zozote vile bila kugusa hili na kulitolea mwelekeo wake na kuwa na msimamo wa wazi Ni kuwahadaa wazanzibari.

Hapa tunafundisha uraia na political science bure.
 
Back
Top Bottom