Kamlete - akibisha...

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,463
39,929
Tarehe 6 Disemba mwaka 2007 Helikopta ya Jeshi la Wananchi ilianguka kwenye ziwa Natron huku na kujeruhi watu kadhaa wakiwemo wale ambao walidaiwa kuwa ni "Wageni wa serikali" ambao walikuwa na vifaa vya kupigia picha za filamu katika ziwa hilo na taarifa za awali zilisema pia kupiga picha mlima wa Oldonyo Lengai.

Na jana Helikopta nyingine imeanguka mkoani Arusha na kuua watu wote sita waliokuwemo kwenye chopa hiyo ambayo ilikuwa inatoka Arusha kuelekea Dodoma.

Ndege zote hizo mbili zinaunganishwa na yule dalali maarufu Bw. Shaileth Pragji Vithlani ambaye ndiye aliyeshughulikia mchakato wa kuzipata ndege hizo na kuwaunganisha JWTZ huku yeye mwenyewe akiwa mabilioni ya shilingi mfukoni kama gharama yake ya udalali. Bw. Vithlani ndiye dalali huyo huyo aliyeshiriki katika ununuzi wa rada ambako inadaiwa kuwa alikatiwa karibu Shs. Bilioni 21 kama malipo yake ya udalali wa kazi yake.

vithlani2.JPG

Kwa vile sasa inaonekana helikopta zake hizo zote zina matatizo, jambo la kwanza ambalo tunapenda kutoa wito.

a. Kusitisha kuruka kwa helikopta zote za Jeshi hadi uchunguzi huru wa kitaalamu wa airworthness ufanywe na kuona kama zinafaa kuendelea na huduma.

b. Endapo helikopta hizo zilizoanguka na zile zilizopo bado zilionekana zina defects zozote za msingi basi Bw. Vithlani pia afunguliwe mashtaka ya manslaughter au criminal negligence kutokana na kuchangia vifo vya watanzania hao na pia kulisababisha Taifa hasara.

c. Maafisa waliohusika na ununuzi wa helikopta hizi wachukuliwe hatua mara moja ikiwemo kufunguliwa mashtaka ya kijeshi.

d. Serikali imtafute huyo dalali kabla na yeye hajafa na kuzikwa huko huko Uswisi siku chache zijazo na mwili wake kuteketezwa kwa moto kwa desturi za kwao!!

Vinginevyo kama kina Rashid Othman wanauwezo wa kukifanya kile Waisrael walikifanya baada ya mauaji ya Munich ya 1972 ambapo maafisa wake wa Usalama waliwafanyizia wale wote waliohusika na mauaji hayo bila kujali nchi walizopo. Ni wakati wa kutuma kikosi chetu (kama hakipo kianzishwe) cha kuwashughulikia watu kama hawa ambao wanafanya uhalifu Tanzania halafu wanakimbilia nje ya nchi.

Tuwatume waende "wakamlete.. akibisha... "
 
Hivi si tuliambiwa serikali ina mkono mrefu inakuwaje huo mkono hauwezi kumfikia huyu bwana??????? Au ni mkono wa nguo nguo hivyo ukipigwa upepo kidogo unapinda na kushindwa kufika unapotakiwa!!!!!!!!!!!!
 
Off topic for a min, as BRAZAMENI would have it, a commercial break.

Kamlete... akibisha...

Unakumbusha mambo ya Hammie Rajab Mzee na Musiba, what you youngunz know about Hammie and Musiba?

And don't even mention Aristablus Elvis Musiba's acrobatics in some ANC shenanigans, or soe Sierra Leonean diamond deals, the Elvis Presley of Bongo espionage dramatics! And all this was way back in 85-86.

Huku jumamosi watu wanasubiri Mfanyakazi kumsoma Muccadam Lakha katika majibizano ya kesi ya uhaini, kujua Hatibu McGhee Ghandi anatoa mpya zipi!

Way before Katabalo and Loliondo, way befiore Family Mirror and The Express, let alone This Day!

Enzi za pen pals na poetry kwenye Sunday News!

Youngunz wanadumaa na Playstation 3, enzi hizo kuona Indiana Jones and The Temple of doom ilikuwa mnakusanyana mtaa mzima kwenda kwa mzee mmoja tu mwenye TV mtaa mzima, lol!

Kununua Benzi shurti kwa kibali cha Juliasi Kaizari dikteta mwenyewe!

By the way the correct ending of akibisha.... is mlipue
Tuendelee
 
Pundit.. nilikuwa naangalia kama vijana wanaweza kukumbuka mambo ya "Tutarudi na Roho zetu", "Kamlete Akibisha Mlipue" au "Kikosi cha Kisasi". Mambo ya "Roho Mkononi" na "Malaika wa Shetani" ya kija Joram Kiango... ..
 
Pundit.. nilikuwa naangalia kama vijana wanaweza kukumbuka mambo ya "Tutarudi na Roho zetu", "Kamlete Akibisha Mlipue" au "Kikosi cha Kisasi". Mambo ya "Roho Mkononi" na "Malaika wa Shetani" ya kija Joram Kiango... ..

Playstation3 na Shigongo wa Shigongo washaharibu mambo.

Unafikiri Youngunz wanamjua hata Agoro Anduru na "This is Living"? Au Ben Mtobwa?
 
Hivi si tuliambiwa serikali ina mkono mrefu inakuwaje huo mkono hauwezi kumfikia huyu bwana??????? Au ni mkono wa nguo nguo hivyo ukipigwa upepo kidogo unapinda na kushindwa kufika unapotakiwa!!!!!!!!!!!!

Methali
Ana mkono mrefu = ni mwizi
Bandugu naona serikali yetu ilipo sema ina mkono mrefu ilikuwa sahihi kwa maana kwamba ni wezi wa mali za wadanganyika.
 
Mwanakijiji,
Sikuwa nimejumlisha moja na moja. Shukrani kwa kutuhabarisha kuhusu uhusiano wa ajali hizi mbili na manunuzi yaliyofanywa na Vithlani.
Cha kushangaza, hakuna anayesema chochote. Wote wako Bungeni kusikiliza porojo.
 
Agoro Anduru umenikumbusha nadhani ndiyo alikuwa na ile "Rosa Mystica" siyo?

Agoro Anduru

Temptation and Other Stories. (Short Story) 1981.

This Is Living and Other Stories. (Short Story) 1982.

A Bed of Roses and Other Writings. (Autobiography) 1989.

That brother was talented. I happenned to have read "This is Living" and Temptation, quite spectacular ukizingatia kulikuwa hakuna internet ya ku plagiarize wala nini.

Sasa siku hizi sijui kuna nani zaidi ya the Shigongos of our world, Mwanakijiji pick up the baton. Unaweza kuja ki Chinua Achebe with a social justice angle kuwabana mafisadi.Jina linajulikana ni kiasi cha kuongea na Mkuki na Nyote, TPH au University Press.

Najua manuscripts zipo.
 
... nilikuwa naangalia kama vijana wanaweza kukumbuka mambo ya "Tutarudi na Roho zetu", "Kamlete Akibisha Mlipue" au "Kikosi cha Kisasi". Mambo ya "Roho Mkononi" na "Malaika wa Shetani" ya kija Joram Kiango... ..

Mwkjj, mambo ya Wazee wa Vijijini hayo!

Tunasoma "Da Vinci code" na watoto wetu wanasoma "Harry Potter and the Sorcerer's Stone" bana!

Hayo mambo ya "Njama" na " Hawala ya Fedha" na "Vuta Nikuvute," na "Ngoswe: Penzi Kitovu cha Uzembe," na "Shida," na "Kuli" na "Adili na Nduguze" hayo mambo yanaaarrribu...
 
Kuhani hayo ya Ngoswe umenikumbusha ule mchezo wa Radio wa "Ngoswe Penzi Kitovu cha Uzembe" na mambo ya "Duka la Kaya". Na hakuna character ambaye bado ananikumbusha mambo ya maisha wakati wa ufisadi kama Chonya wa Chilonwa...
 
Mwanakijiji,
Sikuwa nimejumlisha moja na moja. Shukrani kwa kutuhabarisha kuhusu uhusiano wa ajali hizi mbili na manunuzi yaliyofanywa na Vithlani.
Cha kushangaza, hakuna anayesema chochote. Wote wako Bungeni kusikiliza porojo.

Bado wako kimya kama kawaida na hakuna mwenye ujasiri wa kunyosha mkono wake.. hakuna anayemtafuta vithlani.. na wote wamekaa kimya...
 
Off topic for a min, as BRAZAMENI would have it, a commercial break.

Kamlete... akibisha...

Unakumbusha mambo ya Hammie Rajab Mzee na Musiba, what you youngunz know about Hammie and Musiba?

And don't even mention Aristablus Elvis Musiba's acrobatics in some ANC shenanigans, or soe Sierra Leonean diamond deals, the Elvis Presley of Bongo espionage dramatics! And all this was way back in 85-86.

Huku jumamosi watu wanasubiri Mfanyakazi kumsoma Muccadam Lakha katika majibizano ya kesi ya uhaini, kujua Hatibu McGhee Ghandi anatoa mpya zipi!

Way before Katabalo and Loliondo, way befiore Family Mirror and The Express, let alone This Day!

Enzi za pen pals na poetry kwenye Sunday News!

Youngunz wanadumaa na Playstation 3, enzi hizo kuona Indiana Jones and The Temple of doom ilikuwa mnakusanyana mtaa mzima kwenda kwa mzee mmoja tu mwenye TV mtaa mzima, lol!

Kununua Benzi shurti kwa kibali cha Juliasi Kaizari dikteta mwenyewe!

By the way the correct ending of akibisha.... is mlipue
Tuendelee

Mhh, haya yote yalifanyika lini?

Naona wenzetu mmezaliwa wakati wa mjirumani......lol
 
Mhh, haya yote yalifanyika lini?

Naona wenzetu mmezaliwa wakati wa mjirumani......lol

Hamna aliyezaliwa wakati wa Mjerumani, haya yote mambo ya eighties.

Kama wewe ni eighties baby naweza kukusamehe, lakini kama umezaliwa seventies kwenda nyuma labda ulizidisha kuendesha mapira na kuwinda njiwa, which is not a bad experience by any means :)
 
Hivi Musiba alikuwa haibi artwork? I have a feeling kwamba alikuwa ana "tafsiri" novel za kizungu na kuziuza nyumbani kama kazi yake. Ebu niambie story zote za CIA, KGB, et la...na mambo ya uninja kwenye novel zake alikuwa haziibi kwenye novel za kizungu? Yaani novel zake zilikuwa kama movie vile...

By the way, yuko wapi huyu mtu siku hizi?
 
Hamna aliyezaliwa wakati wa Mjerumani, haya yote mambo ya eighties.

Kama wewe ni eighties baby naweza kukusamehe, lakini kama umezaliwa seventies kwenda nyuma labda ulizidisha kuendesha mapira na kuwinda njiwa, which is not a bad experience by any means :)

Pundit, watoto wa siku hizi hata wakiamua kuwinda, ndege wote wamekwishaliwa na KUNGURU WA ZENJI...
 
Hivi Musiba alikuwa haibi artwork? I have a feeling kwamba alikuwa ana "tafsiri" novel za kizungu na kuziuza nyumbani kama kazi yake. Ebu niambie story zote za CIA, KGB, et la...na mambo ya uninja kwenye novel zake alikuwa haziibi kwenye novel za kizungu? Yaani novel zake zilikuwa kama movie vile...

By the way, yuko wapi huyu mtu siku hizi?

Musiba alikuwa anatumia theme za international espionage kama waandishi wakubwa kina Ludlum na Forsyth, kwa hiyo sishangai kama mtu atasema kuna thematic parallels.Wakati huo vitabu vilikuwa vinaandikwa with the Cold War in mind, kwa hiyo huku kwetu spin za mambo ya ukombozi, ulinzi Frontline States na espionage zilikuwa realistic.

Sijaona mtu kuweka a specific and detailed case kwamba kitabu fulani cha Musiba kimeiga kitabu kingine cha Marekani/ Ulaya.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom