Janja PORI
JF-Expert Member
- Jul 31, 2011
- 825
- 245
Ikiwa kila siku tunaona kilio Bungeni na TIC wakililia mazingira ya uwekezaji kuwa rahisi na kupunguza ukiritimba, bado tunaona kuna Wizara zinajitunguia miongozo inayo kinzana na Sheria iliyopitishwa na Bunge na kusababishia Ugumu kwa wawekezaji kupata vibali vya kazi au vya makazi.
Jana nimeona tangazo la Kamishina wa kazi kwamba kwa mwekezaji anayetaka kibali cha kazi ni lazima kusubmit Vyeti halisi na sio nakala. Binafsi kama mdau katika sekta ya uwekezaji Nchini naona tunajipiga risasi miguuni na kuleta mazingira magumu bila sababu, nasema hivi kwa sababu zifuatazo
i) Sheria ya vibali vya kazi imetamka mahitaji ya mwekezaji anapoomba kibali cha kazi, sheria inasema certified copies ( nakala ya vyeti husika) sasa leo tunaona Kamishna anajitungia miongozo yake kwa kusema lazima kuwe na Vyeti Original
2) Sheria ya Uhamiaji na ya Vibali vya Kazi zinatamka wazi kwamba lazima maombi ya vibali yafanyike mwekezaji au mwajiriwa akiwa nje ya nchi, sasa unajiuliza nini maana ya kuwa na online system kama bado utamtaka mtu asafiri mfano toka Marekani kuleta vyeti halisi Dodoma ? ama nani ambaye yupo razi kutuma vyeti vyake nchini wakati hana uhakika wa kupata hicho kibali??
3) Unakuta mtu ana mtaji wa dola million 1 anataka kuwekeza nchini anaomba kibali cha kazi Class A, bado mnamuomba vyeti vya shule, nani kawaambia wawekezaji wote wameenda shule, mbona wafanyakazi tumekariri sana jamaniii.
OMBI LA HARAKA
Waziri wa uwekezaji naomba tumia mamlaka yako kufuta huu mwongozo mpya mnazidi kufukuza wawekezaji na kusababisha mazingira kuwa magumu ya kuwekeza nchini.
Jana nimeona tangazo la Kamishina wa kazi kwamba kwa mwekezaji anayetaka kibali cha kazi ni lazima kusubmit Vyeti halisi na sio nakala. Binafsi kama mdau katika sekta ya uwekezaji Nchini naona tunajipiga risasi miguuni na kuleta mazingira magumu bila sababu, nasema hivi kwa sababu zifuatazo
i) Sheria ya vibali vya kazi imetamka mahitaji ya mwekezaji anapoomba kibali cha kazi, sheria inasema certified copies ( nakala ya vyeti husika) sasa leo tunaona Kamishna anajitungia miongozo yake kwa kusema lazima kuwe na Vyeti Original
2) Sheria ya Uhamiaji na ya Vibali vya Kazi zinatamka wazi kwamba lazima maombi ya vibali yafanyike mwekezaji au mwajiriwa akiwa nje ya nchi, sasa unajiuliza nini maana ya kuwa na online system kama bado utamtaka mtu asafiri mfano toka Marekani kuleta vyeti halisi Dodoma ? ama nani ambaye yupo razi kutuma vyeti vyake nchini wakati hana uhakika wa kupata hicho kibali??
3) Unakuta mtu ana mtaji wa dola million 1 anataka kuwekeza nchini anaomba kibali cha kazi Class A, bado mnamuomba vyeti vya shule, nani kawaambia wawekezaji wote wameenda shule, mbona wafanyakazi tumekariri sana jamaniii.
OMBI LA HARAKA
Waziri wa uwekezaji naomba tumia mamlaka yako kufuta huu mwongozo mpya mnazidi kufukuza wawekezaji na kusababisha mazingira kuwa magumu ya kuwekeza nchini.