#COVID19 Kamishna Jenerali, Gerald Kusaya: Baadhi ya Watanzania waliomba kibali kwenda kutibiwa India na wakabeba madawa ya kulevya

Nyendo

JF-Expert Member
Jun 4, 2017
1,191
4,104
Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA)imesema katika kipindi cha Ugonjwa wa Covid-19 baadhi ya Watanzania walitumia mwanya huo kujifanya Wagonjwa na kwenda kutibiwa nchini India ilhali wakiwa wamebeba dawa za kulevya. Hata hivyo licha ya kutumia mbinu ya kupata vibali vya kutibiwa nje ya nchi walikamatwa kutokana na intelejensia ya Wakaguzi kutoka Nchi mbalimbali zinazodhibiti dawa hizo.

Akizungumza Jijini Arusha wakati wa utoaji mafunzo kwa Watumishi wa Idara mbalimbali za Serikali ikiwemo uhamasishani wa mradi wa upunguzaji madhara kwa Watumiaji wa Dawa za Kulevya Mkoani Arusha, Kamishna Jenerali, Gerald Kusaya amesema Wasafirishaji wana mbinu mbalimbali za kusafirisha dawa hizo lakini Mamlaka hiyo imedhibiti

Kusaya ameomba Watumishi wa Afya kuwa makini wanapotoa vibali vya Wagonjwa kusafiri "Haiwezekani Mtu anaomba kibali kwenda kutibiwa nje ya Nchi anapewa halafu katika ugonjwa wa covid-19 anaenda kutibiwa ukimwangalia huyo mgonjwa mwenyewe unajiuliza sana Watu wa afya mtusaidie katika hili maana Watumiaji wa dawa za kulevya au Wasafirishaji wana mbinu nyingi na ukiondoka hata Tanzania salama utakamatwa nje ya Nchi na dawa zako na kifungo ni maisha au miaka 20 na 30 jela"
 
Kama ameshindwa kuwataja hadharani ama kupeleka malalamiko polisi, anatamka hayo ili iweje?

Sio serikali miaka ya nyuma ndo ilitaka watanzania wananchi wa kawaida wasaidie polisi kuhusu madawa? Kama kamishna jenerali anashindwa kufanya hivi, raia anayesumbuka na kupata milo mitatu kwa ndo ataweza?

Afrika kweli tupo nyuma mno.
 
Cheti cha dakitari alipataje, means wagonjwa walitokea hospitalini.

Waseme tu lilikuwa dili
 
Cheti cha dakitari alipataje, means wagonjwa walitokea hospitalini.

Waseme tu lilikuwa dili
Ngozi nyeusi ni ngumu sana kuiongoza, yani 90% zinawaza kutoboa life kwa njia mkato tu kimagumashi, sijui tunakwama wapi.

Kuna yale mataaira yatakuja kushangilia hapa kuwa hao ndiyo wenye akili maana wasingestukiwa, wangekuwa wameula.
 
Mkuu wa funguo za kuifungua nchi ana maoni gani kwani? Ama hilo hakuwa amelifungua, kama nchi imefunguliwa mie nadhani ni muda wa kutumia fursa
 
Back
Top Bottom