Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Siku ya tatu sasa tangu mauaji ya raia kutokea mjini Songea na hadi hivi sasa tayari tumesikia kauli toka Polisi Mkoa wa Ruvuma na uongozi wa kisiasa wa mkoa huo ambao umesema utaunda tume kuchunguza mauaji hayo. Wakati huo huo tumesikia Jeshi la Polisi Makao Makuu limemtuma Kamanda anayesimamia mafunzo Bw. Paul Chagonja kwenda kuchunguza kuhusika kwa jeshi hilo katika mauaji hayo. Hadi hivi sasa chombo pekee kilichopewa wajibu wa kikatiba wa kusimamia haki za binadamu nchini yaani Kamisheni ya Haki za Binadamu na Utawala Bora iko kimya ikiachilia wahusika na watuhumiwa kuhusika na mauajia kuchungazana wenyewe.
Inashangaza kuwa hadi hivi sasa Kamisheni hii iko kimya wala kuonesha uharaka wa kuingilia kati sakata ili ili ukweli nao usiwe mhanga wa kwanza wa tukio hili. Tunafahamu hadi hivi sasa siyo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma wala Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wana uwezo na uhuru wa kutosha kusimamia uchunguzi wowote na hatua za kuwakamata polisi wane kuwahoji ni kuchezea akili za Watanzania kwani viongozi hao tayari wameshahalalisha mauaji hayo na lolote litakalotokea yumkini itakuwa ni kuwabebesha lawama askari hao huku wakuu waliotoa baraka silaha za moto kutumika wakiachwa bila kuguswa.
Kamisheni hii imewekwa Kikatiba kuwa ni kimbilio kwa Watanzania na mlinzi wa haki za Watanzania. Ukiondoa mahakama chombo hiki kimeundwa kikiwa na wajibu wa pekee wakusimamia vyombo vingine vyote linapokuja suala la haki za binadamu. Na kati ya haki hizo za binadamu hakuna haki ya msingi zaidi kama haki ya kuishi – kwani haki nyingine zote zinadhania uwepo wa haki hii. Haki ya kuishi haiwezi na haipaswi kuvunjwa kiholela na bila kujali matokeo (with impunity). Jeshi la Polisi nchini – chini ya Said Mwema na Mkuu huyu huyu wa Operesheni Bw. Paul Chagonja limekuwa ni tishio la haki hii ya msingi.
Kamisheni hii haiitaji mtu aje kuitaarifu kuwa kuna uvunjivu wa haki za binadamu. Ibara ya 15:1a imeipa kamisheni hii madaraka ya kuanzisha uchunguzi wake yenyewe bila kuombwa au kupigiwa kelele na mtu mwingine. Ni kutokana na hili wananchi wengi hata hawajui uwepo wa kamisheni hii au uwezo wake. Ni nani anajua kuwa kamisheni hii ina madaraka ya kuleta mashtaka kwenye mahakama yoyote baada ya kukusanya ushahidi wake? Lakini hadi leo hii nani amewahi kusikia kamisheni hii imeleta mashtaka yoyote baada ya matukio ya uvunjaji wa haki za binadamu?
Tunafahamu kuwa Kamisheni hii ina uwezo wa kumuita na kumhoji mtu yeyote na binafsi ningependa kusikia Kamisheni hii inawaita kina Kagonja ambaye bila kuangalia ushahidi amesimama hadharani na kuyahukumu maandamano ya wananchi wa Songea kuwa ni ya "kihuni". Ningependa kusikia Mkuu wa Polisi wa Ruvuma ambaye alisimama na kujaribu kuhalalisha mauaji hayo anaitwa na kweli kabisa hao askari wanne wanaoshikiliwa na Polisi waitwe nao kutoa maelezo yao walipewa amri na nani.
Ni matumaini yangu – na bila ya shaka – matumaini ya wapenda haki wote kuona kuwa Kamisheni hii inafanya kazi yake kwa haraka, uwazi na kwa uthubutu bila woga wala upendeleo wowote. Vinginevyo, maisha ya Watanzania yataendelea kuwa katika rehani ya polisi na polisi wataendelea kuyapopoa maisha hayo wakijua kuwa wanakingiwa kifua na wakuu wao na kwamba uongozi wa kisiasa hauna uthubutu wa kuingilia kati.
Hili ni kweli siyo katika suala hili tu la juzi la Songea bali pia hata katika lile sakata la madaktari ambapo uongozi wa kisiasa ulionekana kushindwa kujua umuhimu wa nini cha kufanya na kuhatarisha maisha ya wananchi. Tulitarajia wengine kamisheni ya haki za binadamu ingeangalia jambo lile kwa kutumia mwanga wa haki za binadamu na kuingilia kati ili kutetea maisha ya Watanzania ambao walijikuta kwenye njia panda ya wale wenye nguvu. Lakini Kamisheni hii haikutoa kauli yoyote wala kuonekana inatekeleza wajibu wake na hili ni aibu hasa kamisheni inayoongozwa na mmojawapo ya majaji wetu maarufu na waliobobea Bw. Amir Manento.
Kama kamisheni hii haitoweza kusimamia na kupigania haki za wananchi na kuwa ya kwanza kupaza sauti yake unapotokea uvunjaji wa haki za binadamu Watanzania watumainie nini au nani? Kama hawa waliokula kiapo cha kufanya kazi zao kwa uadilifu bila upendeleo hawawezi kukemea jeshi la polisi kama walivyolaani mauaji ya wale 17 kule Mara nani mwingine ataweza kufanya hivyo? Kama kamisheni hii inashindwa kumkemea Bw. Paul Kagonja ambaye ni kamanda wa Mafunzo na Operesheni ambaye ni wazi mafunzo anayowapa polisi wetu ni mabovu na hatari kwa raia nani atamkemea? Ni mara ngapi sasa tumeona polisi waliopewa mafunzo chini ya Chagonja wakiuawa wananchi bila kujali (with impunity) halafu ni huyo huyo Kagonja anatumwa kwenda kuchunguza?
Hivi nani anamchunguza Kagonja wakati Kagonja anawachunguza wenzake? Nani anamuuliza aina ya mafunzo ambayo polisi wetu wamepewa chini ya Kagonja? Nani anaweza kumuuliza Mwema kuhusu suala la haki za raia na binadamu katika jeshi la Polisi? Kama siyo Kamisheni hii nani basi? Au tusubiri viongozi vijana – kama kweli wapo – wahoji juu ya hili? Au tusubiri wapinzani kwa sababu ndio wana uchungu zaidi na maisha ya Watanzania?
Na wananchi wasipoiuliza kamisheni hii wakati haki zao zinavunjwa na utu wao kudharauliwa nani aiulize?
Ukitaka kujua zaidi juu ya Kamisheni hii BONYEZA HAPA
Inashangaza kuwa hadi hivi sasa Kamisheni hii iko kimya wala kuonesha uharaka wa kuingilia kati sakata ili ili ukweli nao usiwe mhanga wa kwanza wa tukio hili. Tunafahamu hadi hivi sasa siyo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma wala Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wana uwezo na uhuru wa kutosha kusimamia uchunguzi wowote na hatua za kuwakamata polisi wane kuwahoji ni kuchezea akili za Watanzania kwani viongozi hao tayari wameshahalalisha mauaji hayo na lolote litakalotokea yumkini itakuwa ni kuwabebesha lawama askari hao huku wakuu waliotoa baraka silaha za moto kutumika wakiachwa bila kuguswa.
Kamisheni hii imewekwa Kikatiba kuwa ni kimbilio kwa Watanzania na mlinzi wa haki za Watanzania. Ukiondoa mahakama chombo hiki kimeundwa kikiwa na wajibu wa pekee wakusimamia vyombo vingine vyote linapokuja suala la haki za binadamu. Na kati ya haki hizo za binadamu hakuna haki ya msingi zaidi kama haki ya kuishi – kwani haki nyingine zote zinadhania uwepo wa haki hii. Haki ya kuishi haiwezi na haipaswi kuvunjwa kiholela na bila kujali matokeo (with impunity). Jeshi la Polisi nchini – chini ya Said Mwema na Mkuu huyu huyu wa Operesheni Bw. Paul Chagonja limekuwa ni tishio la haki hii ya msingi.
Kamisheni hii haiitaji mtu aje kuitaarifu kuwa kuna uvunjivu wa haki za binadamu. Ibara ya 15:1a imeipa kamisheni hii madaraka ya kuanzisha uchunguzi wake yenyewe bila kuombwa au kupigiwa kelele na mtu mwingine. Ni kutokana na hili wananchi wengi hata hawajui uwepo wa kamisheni hii au uwezo wake. Ni nani anajua kuwa kamisheni hii ina madaraka ya kuleta mashtaka kwenye mahakama yoyote baada ya kukusanya ushahidi wake? Lakini hadi leo hii nani amewahi kusikia kamisheni hii imeleta mashtaka yoyote baada ya matukio ya uvunjaji wa haki za binadamu?
Tunafahamu kuwa Kamisheni hii ina uwezo wa kumuita na kumhoji mtu yeyote na binafsi ningependa kusikia Kamisheni hii inawaita kina Kagonja ambaye bila kuangalia ushahidi amesimama hadharani na kuyahukumu maandamano ya wananchi wa Songea kuwa ni ya "kihuni". Ningependa kusikia Mkuu wa Polisi wa Ruvuma ambaye alisimama na kujaribu kuhalalisha mauaji hayo anaitwa na kweli kabisa hao askari wanne wanaoshikiliwa na Polisi waitwe nao kutoa maelezo yao walipewa amri na nani.
Ni matumaini yangu – na bila ya shaka – matumaini ya wapenda haki wote kuona kuwa Kamisheni hii inafanya kazi yake kwa haraka, uwazi na kwa uthubutu bila woga wala upendeleo wowote. Vinginevyo, maisha ya Watanzania yataendelea kuwa katika rehani ya polisi na polisi wataendelea kuyapopoa maisha hayo wakijua kuwa wanakingiwa kifua na wakuu wao na kwamba uongozi wa kisiasa hauna uthubutu wa kuingilia kati.
Hili ni kweli siyo katika suala hili tu la juzi la Songea bali pia hata katika lile sakata la madaktari ambapo uongozi wa kisiasa ulionekana kushindwa kujua umuhimu wa nini cha kufanya na kuhatarisha maisha ya wananchi. Tulitarajia wengine kamisheni ya haki za binadamu ingeangalia jambo lile kwa kutumia mwanga wa haki za binadamu na kuingilia kati ili kutetea maisha ya Watanzania ambao walijikuta kwenye njia panda ya wale wenye nguvu. Lakini Kamisheni hii haikutoa kauli yoyote wala kuonekana inatekeleza wajibu wake na hili ni aibu hasa kamisheni inayoongozwa na mmojawapo ya majaji wetu maarufu na waliobobea Bw. Amir Manento.
Kama kamisheni hii haitoweza kusimamia na kupigania haki za wananchi na kuwa ya kwanza kupaza sauti yake unapotokea uvunjaji wa haki za binadamu Watanzania watumainie nini au nani? Kama hawa waliokula kiapo cha kufanya kazi zao kwa uadilifu bila upendeleo hawawezi kukemea jeshi la polisi kama walivyolaani mauaji ya wale 17 kule Mara nani mwingine ataweza kufanya hivyo? Kama kamisheni hii inashindwa kumkemea Bw. Paul Kagonja ambaye ni kamanda wa Mafunzo na Operesheni ambaye ni wazi mafunzo anayowapa polisi wetu ni mabovu na hatari kwa raia nani atamkemea? Ni mara ngapi sasa tumeona polisi waliopewa mafunzo chini ya Chagonja wakiuawa wananchi bila kujali (with impunity) halafu ni huyo huyo Kagonja anatumwa kwenda kuchunguza?
Hivi nani anamchunguza Kagonja wakati Kagonja anawachunguza wenzake? Nani anamuuliza aina ya mafunzo ambayo polisi wetu wamepewa chini ya Kagonja? Nani anaweza kumuuliza Mwema kuhusu suala la haki za raia na binadamu katika jeshi la Polisi? Kama siyo Kamisheni hii nani basi? Au tusubiri viongozi vijana – kama kweli wapo – wahoji juu ya hili? Au tusubiri wapinzani kwa sababu ndio wana uchungu zaidi na maisha ya Watanzania?
Na wananchi wasipoiuliza kamisheni hii wakati haki zao zinavunjwa na utu wao kudharauliwa nani aiulize?
Ukitaka kujua zaidi juu ya Kamisheni hii BONYEZA HAPA