Kambi ya upinzani wafurahia waziri kuitosa serikali bungeni

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,005
Date::7/12/2008
Kambi ya upinzani wafurahia waziri kuitosa serikali bungeni
Na Kizitto Noya
Mwananchi

KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Willibrod Slaa amesema kuwa, kauli ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Lawrence Masha kwamba, Kampuni ya Deep Green Finance ilifunguliwa na kufungwa kwa agizo la serikali, imefungua ukurasa mpya wa mjadala wa ufisadi nchini.

Akizungumza na gazeti hili jana, Dk Slaa alisema, kauli hiyo imeondoa utata kuhusu mmiliki wa kampuni hiyo kwa kuwa imeeleza wazi kuwa, serikali ndiyo iliyohusika kuchota mabilioni ya fedha za wananchi kupitia akaunti hiyo ya Deep Green Finance.

Alisema, anamshukuru Waziri Masha kwa ujasiri wake wa kuitosa serikali na kusema ukweli, jambo ambalo litamsaidia (Dk Slaa) kutafuta mbinu mpya za kukabiliana na wizi huo unaochangia umaskini wa Mtanzania.

"Sisi tumeipokea kauli hiyo vizuri na tumemshukuru Waziri Masha kwa kuitosa serikali na kutuonyesha mlango sahihi wa suala hilo ambao hatukuujua," alisema Dk Slaa.

Alisema, Chadema haina shaka kwamba kauli hiyo ni sahihi, kwani haijakanushwa na serikali na hivyo kuichukulia kwa uzito unaostahili katika harakati zake za kutaka fedha hizo zirejeshwe.

"Kimsingi, sina shaka kwamba kauli hiyo ni sahihi, kwani haijakanushwa wala kutolewa ufafanuzi mwingine, hivyo nitaichukua kama ilivyo ili inisaidie katika vita vyangu dhidi ya mafisadi," alisema.

Alisema, kauli hiyo imemwonyesha adui halisi katika mapambano dhidi ya ufisadi na hivyo kurahisisha mapambano hayo kwa kiasi kikubwa, tofauti na zamani ambapo kazi ilikuwa ngumu kutokana na kutomjua mhusika halisi wa suala hilo.

Wiki iliyopita, baada ya kubanwa na wapigakura wake, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Lawrence Masha, alisema kampuni yake ya Uwakili wa Immma Advocate, iliifungua na baadaye kuifunga Kampuni ya Deep Green Finance kwa agizo la serikali.

Katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika eneo la Sokoni, Butimba nje kidogo ya Jiji la Mwanza, wapigakura hao walimtaka Masha ambaye ni mbunge wao, kueleza sababu zilizomfanya akubali kuisajili Kampuni ya Deep Green Finance Company, ambayo inadaiwa kuchota mabilioni ya shilingi kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BoT), kinyemela na baada ya kutekeleza ufisadi huo kuifunga ghafla.

Mmoja wa waliohudhuria mkutano huo, Peter Charles, mkazi wa Kata ya Butimba wilayani Nyamagana, alitaka kujua endapo Waziri Masha ni mmoja wa wamiliki wa Kampuni ya uwakili ya Immma, ambayo imetoa jaji kwenye serikali ya awamu ya nne.

Baada ya Waziri Masha kukubali, mwananchi huyo alimtaka waziri amhakikishie kwamba ni msafi na kwamba hahusiki na wezi wa mabilioni ya fedha za BoT wakati kampuni aliyoifungua imetajwa kuhusika na upotevu wa fedha hizo za EPA.

"Nashukuru kwa kuuliza swali hilo katika wilaya hii, ingawa swali umelipamba sana, lakini najua umelipata katika vigazeti, mimi ni Mkurugenzi wa Immma, lakini kwa sasa nipo likizo bila malipo, nalipwa posho na Immma. Kuhusu ujaji wa Mheshimiwa Mujulizi, yeye ameteuliwa na rais kutokana na taaluma yake ya sheria.

Ni kweli kampuni yangu ilisajili Deep Green na tukaifunga kwa maelekezo ya serikali. Immma haikuchota mabilioni, naomba ieleweke. Na hili, sijawahi kuficha ni kweli. Kampuni hiyo ya Deep Green baada ya kusajiliwa, ilifungwa kwa maagizo ya serikali ya Jamhuri ya Muungano," alisema Masha katika majibu yake.

Kampuni ya Deep Green Finance Co. Ltd ilianzishwa Machi 18, 2004 na kwa kipindi cha miezi minne, kati ya Agosti 1 na Desemba 1, 2005 inadaiwa kupokea jumla ya Sh 10,484,005,815.39 kutoka BoT. ??Kipindi hicho kilikuwa cha mchakato au kampeni za Uchaguzi Mkuu uliofanyika Desemba 14, 2005 na kwamba kuanzia Desemba 11 mwaka huo, hakuna fedha iliyoingizwa katika akaunti ya kampuni hiyo hadi Februari 27, 2007 ilipovunjwa kwa hiari ya wanahisa wake. ?

Wakurugenzi wake (majina tunayo), ambao wanadai kupokea fedha hizo katika mazingira ya kutatanisha mmoja ni kutoka New Zealand na wawili ni kutoka Afrika Kusini. ?

Wakurugenzi hao wote ni wakazi wa Afrika Kusini na ni maofisa au wafanyakazi wa Nedbank Ltd ya Afrika Kusini. ?

Kwa mujibu wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), wanahisa wa awali wa kampuni hiyo, walikuwa ni mawakili wawili Watanzania ambao pia ni mawakili wa Kampuni ya Tangold ambayo nayo imo kwenye orodha ya wanaotajwa kuchota fedha BoT. ?

Taarifa za kibenki zinaonyesha kwamba, Mei 1, 2004, Deep Green Finance ilifungua akaunti Na. 011103024840 katika tawi la Corporate la Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Dar es Salaam. ?

Siku ya ufunguzi wa akaunti hiyo ilikuwa Siku Kuu ya Wafanyakazi (Mei Mosi) na ilikuwa mapumziko na kwamba, kampuni hiyo iliruhusiwa kufungua akaunti bila kuingiza wala kutoa fedha kwa zaidi ya mwaka mmoja, kuanzia Mei Mosi, 2004 hadi Julai 31, 2005. ?

Kampuni hiyo haikuwepo kwenye orodha ya taasisi za kifedha iliyotolewa na Benki Kuu Agosti 21, 2007 ili kuonyesha kwamba imesajiliwa. ?

Kampuni nyingine ya Tangold, kama ilivyo kuwa kwa kampuni ya Deep Green Finance ilifunguliwa siku ya Sikukuu ya Mwaka Mpya ambayo ilikuwa mapumziko, Januari Mosi, 2003 kwa akaunti Na. 011103024852 NBC tawi la Corporate.
 
Tunahesabu tu siku kwani kila mtu atajaribu kujiosha na kujikuta wanakili uchafu waliofanya. Sasa hivi wanajikosha ila tunapokaribia uchaguzi mtasikia santuri zilezile lakini that time kutakuwa na Remix.

Kuna umuhimu wa Bunge kutunga sheria kuwa unapopata Presidential Appointment unatakiwa uchukuwe POLYGRAPH TEST. Naamini kwa fedha Tanzania iliyonayo haiwezi kukosa ya kununulia LIE DETECTOR MACHINE. Hapa kwa msemo wa M.M.M hawa jamaa wanaendelea kuzuga tu.
 
Tatizo langu ni resources... wapinzani wanazozitumia wakidhani zitakuwa silaha zao kwenye chaguzi!

Kila Mtanzania anajua kuna mchezo mchafu... sasa ingekuwa ni muafaka sasa akina Dr. Slaa kufanyia kazi mambo mengine sasa... Kajengeni chama sasa...
 
Tatizo langu ni resources... wapinzani wanazozitumia wakidhani zitakuwa silaha zao kwenye chaguzi!

Kila Mtanzania anajua kuna mchezo mchafu... sasa ingekuwa ni muafaka sasa akina Dr. Slaa kufanyia kazi mambo mengine sasa... Kajengeni chama sasa...

Pole Kasheshe,Kujenga Chama au vyama ni kitu endelevu, na kumkoma nyani giledi pia ni endelevu na usitegemee kwamba hii itakuja kwisha au at a point of time things will cool, Never but it will keep poping out till kimeeleweka
 
Masha anapaswa kujua kuwa muhimu si sehemu muuliza swali alikopata information kuhusu Deep Green. Iwe toka kwenye vigazeti, magazeti... Muhimu aeleze anachojua kuhusu hii kampuni. Hongera muuliza swali kwa kutuma ujumbe serikalini kuwa wananchi wanajua mengi kuhusu ufisadi wa wakubwa kuliko wakubwa wanavyofikiri !
 
Kasheshe,

Hawa jamaa wameishiwa, nahisi ni opportunists au hawajui nini kinatakiwa kufanyika ili kuwa WIN wananchi.

Ukienda kijijini kwangu Mchamba wima hawaelewi hata kidogo ukiongelea DEEP green finance wamechota hela serikalini, hata ukiihusisha na madawati na madawa hospitalini, bado hawaelewi.

Inatakiwa wapinzani wajijenge kichama zaidi. Hili najua ni ngumu kwasababu wengi wao wapo after matumbo yao, najua wapo hodari; ila wamezungukwa na wenye tamaa na wasio na uwezo wa kujenga hoja!

Tutaendelea kuwatawala milele!

FairPlayer
 
Hii style ya kudharau vitu kama fedha au vyombo vya habari inatuonesha ni viongozi gani tunaowachagua.Kama jinsi Chenge alivyoyaita mamilioni ´Vijisenti´ sasa pia Masha anaita vyombo vya habari ´vigazeti`.Inashangaza manake hawa jamaa siku zote ni kuonesha dharau kwa wananchi kwa namna fulani ambayo inajionesha wazi katika matamshi yao.Huyo mwanachi kauliza swali la msingi na hata kama kapata sources zake kwenye magazeti mbona sasa ni ukweli mtupu ambao unaelekea kumbana Masha.Masha ajiulize bila vyombo vya habari wananchi wapate vipi habari kuhusu nchi yao?
 
Kasheshe,

Hawa jamaa wameishiwa, nahisi ni opportunists au hawajui nini kinatakiwa kufanyika ili kuwa WIN wananchi.

Ukienda kijijini kwangu Mchamba wima hawaelewi hata kidogo ukiongelea DEEP green finance wamechota hela serikalini, hata ukiihusisha na madawati na madawa hospitalini, bado hawaelewi.

Inatakiwa wapinzani wajijenge kichama zaidi. Hili najua ni ngumu kwasababu wengi wao wapo after matumbo yao, najua wapo hodari; ila wamezungukwa na wenye tamaa na wasio na uwezo wa kujenga hoja!

Tutaendelea kuwatawala milele!

FairPlayer

Mkuu Fair player pamoja na kwamba two wrongs can not make a right....... Je CCM tuwaiteje???? Do you really believe kwamba wapinzani wakienda kijijini kuzungumzia say kilimo, maji safi, shule n.k wataeleweka........ This is from your point of view kuhusu mchamba wima
 
Piga ua lakini siku za mwizi ni 40 tu! Zikifika nyie wezi hamtajua kua niwa Tanzania wale mlio waibia siku za sikukuu mkafungua akaunti zenu kinyemela mkidhani wamelala nyumbani na wengine wamelewa mtaani. Mtapondwa mawe kipigo cha mbwa mwizi!
 
Kasheshe,

Hawa jamaa wameishiwa, nahisi ni opportunists au hawajui nini kinatakiwa kufanyika ili kuwa WIN wananchi.

Ukienda kijijini kwangu Mchamba wima hawaelewi hata kidogo ukiongelea DEEP green finance wamechota hela serikalini, hata ukiihusisha na madawati na madawa hospitalini, bado hawaelewi.

Inatakiwa wapinzani wajijenge kichama zaidi. Hili najua ni ngumu kwasababu wengi wao wapo after matumbo yao, najua wapo hodari; ila wamezungukwa na wenye tamaa na wasio na uwezo wa kujenga hoja!

Tutaendelea kuwatawala milele!

FairPlayer

Watajijenga kichama vipi kama wataacha kuzungumzia ujambazi unaofanywa na serikali dhidi ya mali ya umma?

Dr. Slaa kama mbunge ana haki na wajibu wa kuendeleza haya mapambano, ya huko wilayani kuna wengine wataenda na kwa pamoja ndio nguvu ya chama hujengeka.

Watanzania tusipozuia wizi wa fedha za umma, tusitegemee maendeleo yoyote siku za mbeleni. Lazima hata hao majambazi wapate hofu, wakijua kuna uwezekano wa kukamatwa au kuumbuliwa.

Labda kinachokosekana ni nguvu ya pamoja ya upinzani na wapenda maendeleo wengine kumpa support Dr. Slaa ili aweze kuendesha haya mapambano kwa ufanisi zaidi na zaidi.

Dr. Slaa, mafanikio mema, juhudi zako wengine tunaziheshimu na kukuombea mafanikio mema zaidi katika kuwaumbua hawa majambazi. Hata wasipopelekwa jela lakini bado hawatakula hizo fedha wakiwa kivulini.
 
Watajijenga kichama vipi kama wataacha kuzungumzia ujambazi unaofanywa na serikali dhidi ya mali ya umma?

Dr. Slaa kama mbunge ana haki na wajibu wa kuendeleza haya mapambano, ya huko wilayani kuna wengine wataenda na kwa pamoja ndio nguvu ya chama hujengeka.

Watanzania tusipozuia wizi wa fedha za umma, tusitegemee maendeleo yoyote siku za mbeleni. Lazima hata hao majambazi wapate hofu, wakijua kuna uwezekano wa kukamatwa au kuumbuliwa.

Labda kinachokosekana ni nguvu ya pamoja ya upinzani na wapenda maendeleo wengine kumpa support Dr. Slaa ili aweze kuendesha haya mapambano kwa ufanisi zaidi na zaidi.

Dr. Slaa, mafanikio mema, juhudi zako wengine tunaziheshimu na kukuombea mafanikio mema zaidi katika kuwaumbua hawa majambazi. Hata wasipopelekwa jela lakini bado hawatakula hizo fedha wakiwa kivulini.


Mapambano dhidi ya ufisadi ni jambo jema sana Lakini wao wanakosea wanapotaka kufanya hilo kua ngazi ya kupandia na kufanya jambo la kishujaa.

Kwani wewe Mtanzania kama ungekua mbunge na mikataba mibovu umeipata hapa JF ungeshindwa kusema na kulipigia kelele? Hapo iuonekane je shujaa kwa hilo wakati ni haki yako ya msingi??

Hizi siasa za kupandilia migongo ya watu mie ndio naona ni mbinu chafu ambayo iko encapsulated na mbinu na mbinu sahihi ili wafikie malengo yao, sasa malengo yatakapofikiwa na kua striped out hiyo encapsulation ndio tutakapoona sura halisi.

Nawachanganya wana siasa hawa Mzidakaya na Kigunge kati yao mmoja naye alijijengea umaarufu kwa siasa hizi za encap na kupandilia migongo ya watu ,mwana siasa huyu wa ccm alisifika kwa kufurumua ma skendo na hatimaye kuwatemesha mawaziri mzigo.Tathimini leo utamwamini tena kama aliwapenda watanzania??

Mwana siasa apimwe kwa mchango wake kimaendeleo ktk jamii .Haya mambo ya kupandiliana ukimpa seleli,mwakyembe,anna kilango na wengine wengi hizo mikataba mibovu ama wizi naamini wata lisimamia kidete.

Skendo ndani ya serikali ya ccm hazijaanza kuubuliwa na chadema na wala na Dr Slaa wala zito.
Waziri simba skendo lake limekomaliwa na wana ccm ,na wengi mawaziri.sema bahati nzuri hili la Boat na madini limeangukia mikononi mwa chadema .Lakini wengi twa tambua kabisa masikendo hayajaanzishwa nao na hii isiwape warrant eti wao ni wasafi wala mashujaa.Hizi ni siasa za kufumaniana tu.
 
Mweleze mtanzania maana jamaa saa nyingine ananimaliza...Mwambiye chama ni watu na watu ni sisi na wananchi wengineo waloko vijijivi na kila mahali huko bongo!
Sasa hivi ni muhimu hata kura za Wahadzabe na hata Mang'ati.
Kama wananchi waliopiga kura hawazidi milioni kumi na wakati taifa lina wananchi karibia milioni arubaini then ni muhimu waende huko vijijini na wahakikishe wana keep in touch na wana wa organize wananchi hao kwa kila hali na kuwasomesha.
 
Mapambano dhidi ya ufisadi ni jambo jema sana Lakini wao wanakosea wanapotaka kufanya hilo kua ngazi ya kupandia na kufanya jambo la kishujaa.

Kwani wewe Mtanzania kama ungekua mbunge na mikataba mibovu umeipata hapa JF ungeshindwa kusema na kulipigia kelele? Hapo iuonekane je shujaa kwa hilo wakati ni haki yako ya msingi??

Hizi siasa za kupandilia migongo ya watu mie ndio naona ni mbinu chafu ambayo iko encapsulated na mbinu na mbinu sahihi ili wafikie malengo yao, sasa malengo yatakapofikiwa na kua striped out hiyo encapsulation ndio tutakapoona sura halisi.

Nawachanganya wana siasa hawa Mzidakaya na Kigunge kati yao mmoja naye alijijengea umaarufu kwa siasa hizi za encap na kupandilia migongo ya watu ,mwana siasa huyu wa ccm alisifika kwa kufurumua ma skendo na hatimaye kuwatemesha mawaziri mzigo.Tathimini leo utamwamini tena kama aliwapenda watanzania??

Mwana siasa apimwe kwa mchango wake kimaendeleo ktk jamii .Haya mambo ya kupandiliana ukimpa seleli,mwakyembe,anna kilango na wengine wengi hizo mikataba mibovu ama wizi naamini wata lisimamia kidete.

Skendo ndani ya serikali ya ccm hazijaanza kuubuliwa na chadema na wala na Dr Slaa wala zito.
Waziri simba skendo lake limekomaliwa na wana ccm ,na wengi mawaziri.sema bahati nzuri hili la Boat na madini limeangukia mikononi mwa chadema .Lakini wengi twa tambua kabisa masikendo hayajaanzishwa nao na hii isiwape warrant eti wao ni wasafi wala mashujaa.Hizi ni siasa za kufumaniana tu.

Ndugu yangu we mgeni hapa jf?
Unakumbuka kashafa za BOT zilipoletwa hapa na samvula?
Unakumbuka jinsi serikali ilipoanza kwa ku panic na hata mpambe wao aliyejiita usalama wa taifa anayekwenda kwa jina la shy kuanza vitisho?
Ama umeshasahau yaliyowakumba robots esp kina Invisible.
Kwahiyo wewe kudai hata kama yeye angekuwa mbunge angefanya hivi ama vile ni upotoshaji.
Kwani si bado kuna wabunge mafisadi ambao bado wako bungeni tena na wengine ni warogi?
 
Ndugu yangu we mgeni hapa jf?
Unakumbuka kashafa za BOT zilipoletwa hapa na samvula?
Unakumbuka jinsi serikali ilipoanza kwa ku panic na hata mpambe wao aliyejiita usalama wa taifa anayekwenda kwa jina la shy kuanza vitisho?
Ama umeshasahau yaliyowakumba robots esp kina Invisible.
Kwahiyo wewe kudai hata kama yeye angekuwa mbunge angefanya hivi ama vile ni upotoshaji.
Kwani si bado kuna wabunge mafisadi ambao bado wako bungeni tena na wengine ni warogi?


Mwakyembe ni CHADEMA??
 
Mapambano dhidi ya ufisadi ni jambo jema sana Lakini wao wanakosea wanapotaka kufanya hilo kua ngazi ya kupandia na kufanya jambo la kishujaa.

Kwani wewe Mtanzania kama ungekua mbunge na mikataba mibovu umeipata hapa JF ungeshindwa kusema na kulipigia kelele? Hapo iuonekane je shujaa kwa hilo wakati ni haki yako ya msingi??

Hizi siasa za kupandilia migongo ya watu mie ndio naona ni mbinu chafu ambayo iko encapsulated na mbinu na mbinu sahihi ili wafikie malengo yao, sasa malengo yatakapofikiwa na kua striped out hiyo encapsulation ndio tutakapoona sura halisi.

Nawachanganya wana siasa hawa Mzidakaya na Kigunge kati yao mmoja naye alijijengea umaarufu kwa siasa hizi za encap na kupandilia migongo ya watu ,mwana siasa huyu wa ccm alisifika kwa kufurumua ma skendo na hatimaye kuwatemesha mawaziri mzigo.Tathimini leo utamwamini tena kama aliwapenda watanzania??

Mwana siasa apimwe kwa mchango wake kimaendeleo ktk jamii .Haya mambo ya kupandiliana ukimpa seleli,mwakyembe,anna kilango na wengine wengi hizo mikataba mibovu ama wizi naamini wata lisimamia kidete.

Skendo ndani ya serikali ya ccm hazijaanza kuubuliwa na chadema na wala na Dr Slaa wala zito.
Waziri simba skendo lake limekomaliwa na wana ccm ,na wengi mawaziri.sema bahati nzuri hili la Boat na madini limeangukia mikononi mwa chadema .Lakini wengi twa tambua kabisa masikendo hayajaanzishwa nao na hii isiwape warrant eti wao ni wasafi wala mashujaa.Hizi ni siasa za kufumaniana tu.

Mbona anayoyafanya Dr Slaa ni katika kusimamia tu sera bora ya CHADEMA ya UTAWALA BORA? Soma hapa:http://www.chadema.net/nyaraka/sera/bora.php

Pia anasimamia misingi ya chama, falsafa ya chama ni NGUVU YA UMMA inataka watanzania wanufaike na kodi na rasilimali zao: http://www.chadema.net/nyaraka/falsafa.php

http://www.chadema.net/nyaraka/itikadi.php

Pia anasimamia Sera ya Chama ya UADILIFU NA UKWELI kama
http://www.chadema.net/chama/bendera.php

inavyowakilishwa na rangi nyeupe ya Bendera ya Chama, soma hapa:

http://www.chadema.net/chama/bendera.php

Halafu bado inasemwa kwamba wapinzani hawana sera!

Asha
 
Mbona anayoyafanya Dr Slaa ni katika kusimamia tu sera bora ya CHADEMA ya UTAWALA BORA? Soma hapa:http://www.chadema.net/nyaraka/sera/bora.php

Pia anasimamia misingi ya chama, falsafa ya chama ni NGUVU YA UMMA inataka watanzania wanufaike na kodi na rasilimali zao: http://www.chadema.net/nyaraka/falsafa.php

http://www.chadema.net/nyaraka/itikadi.php

Pia anasimamia Sera ya Chama ya UADILIFU NA UKWELI kama
http://www.chadema.net/chama/bendera.php

inavyowakilishwa na rangi nyeupe ya Bendera ya Chama, soma hapa:

http://www.chadema.net/chama/bendera.php

Halafu bado inasemwa kwamba wapinzani hawana sera!

Asha


Rekebisheni chama chenu hizo siasa za ufumanizi sio za ujiko ni wajibu wa kila mmoja kufumania.

Mpeni Mwl Kitila Mkumbo
kama umri hujafika kugombea urais chadema silazima wasimamishe mgombea wa Urais.
 
Rekebisheni chama chenu hizo siasa za ufumanizi sio za ujiko ni wajibu wa kila mmoja kufumania.

Mpeni Mwl Kitila Mkumbo
kama umri hujafika kugombea urais chadema silazima wasimamishe mgombea wa Urais.

Nakuunga mkono kuhusu Kitila, ni vyema akarudi nchini mapema kuja kushika uongozi kwenye chama chake. Lakini hilo la kufamiana inaelekea umezidiwa hoja saa umezua vioja nikianza mipasho najua unanijua. Lakini rudi hapa hapo juu, nimekuonyesha kuwa anachokifanya Dr Slaa ni kuonyesha kwa maneno kwamba CHADEMA ikiwa madarakani itasimamia kwa vitendo sera yake ya Utawala Bora, Uadilifu na ukweli. Pitia hizo links okosoe kama una hoja, kama huna nyamaza

Asha
 
Mimi naona hakuitosa serikali alikuwa anajua nini anakisema na anajua nini kitatokea - makele mengi na siku zinaenda - hawa jamaa wameshakufa wadudu kwa vile wanajua Wtzni makondoo hawana watachokifanya na wao wataendelea kupeta.

Ufisadi wote ulowekwa hadharani wahusika wamefanya nini bado wanatetewa na kupokewa kama wafalme katika ajimbo yao na Chama chao kikiwasafisha.
 
Mwakyembe ni CHADEMA??

Hivi ni lini tutaacha mambo ya itikadi za vyama katika mambo ya Utaifa??

Mkamap,
Sidhani kama waTanzania wanaomsifu Anne Kilango ni wanaCCM tu! Wapo pia wapinzani tena wengi, kwani aliyoyasema si masuala ya chama bali Taifa!

Asha,
Sidhani kwamba wote wanao-support Upinzani hata kwa kuwapa "nyaraka za serikali" si kwasababu ni wanaCHADEMA, CUF, TLP .. hapana ni kwasababu watu hao wanasukumwa na Utaifa! Sidhani kama anayoyafanya Dr Slaa ama Zitto ni kwaajili ya wanaCHADEMA tu!

Sasa tuache kumpandisha mmoja (CCM/ CHADEMA) zaidi ya mwingine (CHADEMA/CCM)! Tunachopenda ni mbunge yeyote asimame na kutetea maslahi ya Taifa na si chama ama wanachama wao! Na katika hili tutashinda katika UMASKINI huu!

Suala la kwamba hoja hii ilianzisha na CCM ama CHADEMA wala haiingii akilini kwa mtu mwenye kupenda na kujali UTAIFA. Tunachotaka ni yeyote (awe CCM ama CHADEMA) kuionyesha serikali wapi walipokosea, na tutafurahi zaidi iwapo mtoa hoja huyo (awe CCM ama CHADEMA) atasimamia hoja yake mpaka mwisho!

Mkamap,
Kuhusu suala la Mwakyembe, nadhani unafahamu ni watu gani waliompokea kwa shangwe aliporudi jimboni kwake, na nadhani unafahamu ni chama gani kilikataa kushiriki kwenye mapokezi hayo!

Sasa tusiendelee kuendekeza itikadi za vyama wakati tunakufa na UMASKINI, tena UMASKINI ule ule uliomuua BABU yetu!

Katika UMASKINI huu, tunachotaka ni HEROS awe CCM ama CHADEMA, tunataka HEROS!!
 
Date::7/12/2008

Akizungumza na gazeti hili jana, Dk Slaa alisema, kauli hiyo imeondoa utata kuhusu mmiliki wa kampuni hiyo kwa kuwa imeeleza wazi kuwa, serikali ndiyo iliyohusika kuchota mabilioni ya fedha za wananchi kupitia akaunti hiyo ya Deep Green Finance.

Wrong call Dr!Kauli hii haijaondoa utata huu by any stretch ingawa imeconfirm kuhusika kwa serikali katika suala hili.I thought we had this filed ages ago though.

"Kimsingi, sina shaka kwamba kauli hiyo ni sahihi, kwani haijakanushwa wala kutolewa ufafanuzi mwingine, hivyo nitaichukua kama ilivyo ili inisaidie katika vita vyangu dhidi ya mafisadi," alisema.

Tempting but not so fast...Sikatai uwezekano wa kuwepo ukweli katika kauli ya Mheshimiwa Masha hata hivyo,kutotolewa kwa maelezo kusitupe hakika ya jambo hili.Nadhani maelezo ya uchunguzi wa kituko cha ushirikina bungeni yalitupa insight into the extent to which some can go to protect their skins.In the midst of their shortsighted,human relations abilities of course.At this point,we do not want to underestimate the power of ignorance in high doses.

Date::7/12/2008 Alisema, kauli hiyo imemwonyesha adui halisi katika mapambano dhidi ya ufisadi na hivyo kurahisisha mapambano hayo kwa kiasi kikubwa, tofauti na zamani ambapo kazi ilikuwa ngumu kutokana na kutomjua mhusika halisi wa suala hilo.

Hapana bwana!Adui serikali mbona ameingia katika genre ya myths tangu zamani?Glad that my oppa told me bedtime stories for it was through them that I understood what is real and what is not.Bila kujua maadui wetu kwa majina,most of our energy is gone in vain.Hatuwezi kusema tumeonyeshwa adui halisi kama hata mbuzi mwenyewe hajatolewa guniani.


"Nashukuru kwa kuuliza swali hilo katika wilaya hii, ingawa swali umelipamba sana, lakini najua umelipata katika vigazeti, mimi ni Mkurugenzi wa Immma, lakini kwa sasa nipo likizo bila malipo, nalipwa posho na Immma. Kuhusu ujaji wa Mheshimiwa Mujulizi, yeye ameteuliwa na rais kutokana na taaluma yake ya sheria.Ni kweli kampuni yangu ilisajili Deep Green na tukaifunga kwa maelekezo ya serikali. Immma haikuchota mabilioni, naomba ieleweke. Na hili, sijawahi kuficha ni kweli. Kampuni hiyo ya Deep Green baada ya kusajiliwa, ilifungwa kwa maagizo ya serikali ya Jamhuri ya Muungano," alisema Masha katika majibu yake.

Cheap shots Hon.Uko likizo,unalipwa,hulipwi,na nani...none of our business.Umesajili na kuifungia Deep Green kwa maagizo ya hell knows who....now,this is our business!Natumaini hukudhamiria kusahau kuwa siku zote tunasema Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kuepuka sending the wrong idea kwa watu wanaofahamu the strength of words.That aside,sidhani kama ofisi yako ina uwezo wa kuhold watu wote wanaocomprise serikali.Break it down bwana,at least to single digits and while at it,don't forget to drop in the names.

(majina tunayo),
Aghhrr!

... kampuni hiyo iliruhusiwa kufungua akaunti bila kuingiza wala kutoa fedha kwa zaidi ya mwaka mmoja, kuanzia Mei Mosi, 2004 hadi Julai 31, 2005. ?

I am getting cramps just trying to find sensible explanations here.So,kampuni haikutakiwa kuingiza wala kutoa pesa kutoka kwenye akaunti yao.At the same time,fedha kutoka BOT ziliingizwa kwenye akaunti hiyo katika kipindi hiki.Ina maana uvunjwaji wa sheria hii ya benki hauna concequences zozote?Maana,I don't want to imagine the bank authorities failing to pick this up.

Kampuni hiyo haikuwepo kwenye orodha ya taasisi za kifedha iliyotolewa na Benki Kuu Agosti 21, 2007 ili kuonyesha kwamba imesajiliwa. ?

Dah!

Dr. rejoice not,for the journey has just begun.
 
Back
Top Bottom