Kambi ya Upinzani: Kauli ya Spika kutoshirikiana na CAG ni ya Ndugai siyo ya Bunge.

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,271
47,271
KAMBI rasmi ya Upinzani Bungeni imemtaka Spika wa Bunge Job Ndugai kutengua uamuzi wake wa kusitisha kufanya kazi na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG).

WhatsApp Image 2019-01-16 at 12.09.15 PM.jpeg


Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dodoma akiwa ameambatana na wabunge wa upinzani, Msemaji wa kambi hiyo, John Mnyika amesema kama Spika hatatengua uamuzi wake watatumia kila njia za kibunge ikiwemo Mbunge kuwasilisha hoja ya kutokuwa na imani na Spika.

“Kamati ya bunge ya uongozi haijawahi kukaa kikao chochote cha kusitisha kufanya kazi na CAG, huu uamuzi ni uamuzi binafsi wa spika ambao kambi hatuungi mkono na hatukubaliani nao,”amesema.

Ametoa wito kwa Spika kujitokeza kwa umma kueleza kuwa ni kikao gani alikaa na akina nani kufanya huo uamuzi huo.

“Uamuzi huo umeenda sambamba na kusambaratisha kamati za bunge za Hesabu za serikali(PAC) na Hesabu za serikali za mitaa(LAAC), Kamati za bunge hizo zimesitishwa kufanya kazi zake kuanzia 14-25 januari,mwaka huu na kwa mujibu wa ratiba ya bunge kamati zinamaliza kazi zake tarehe 25,”amesema.

Mnyika amesema Spika amesitisha kamati kufanya kazi zao za kikatiba kwa mujibu wa ratiba.

“Tunapinga hatua hii na tunapinga huu uamuzi, tunataka Spika abadilishe mara moja huu uamuzi na kamati zikutane na kufanya kazi ya kikatiba,”alisema.

Ameongeza “Spika anasema kwasababu CAG ameitwa tarehe 21 januari kwenye kamati kwa madai kuna mgogoro kati ya Bunge na CAG wakati hakuna kamati ya bunge iliyotangaza Bunge lina mgogoro na CAG na kauli hiyo ni binafsi si kauli ya bunge wala taasisi ya bunge,”

Chanzo: IPP
 
Safi kabisa Ndugai hafai kabisa kuwa spika,hana uchungu na mali za umma.Unamkataa CAG halafu nani adhibiti na kukagua mali za umma?
Mwaka huu tunataka hesabu za ATCL na TANROADS bungeni ziletwe na CAG zijadiliwe maana miaka ya nyuma hazikukaguliwa wala kuletwa bungeni
 
Safi kabisa Ndugai hafai kabisa kuwa spika,hana uchungu na mali za umma.Unamkataa CAG halafu nani adhibiti na kukagua mali za umma?
Mwaka huu tunataka hesabu za ATCL na TANROADS bungeni ziletwe na CAG zijadiliwe maana miaka ya nyuma hazikukaguliwa wala kuletwa bungeni
Safi sana, CAG hana hana hadhi tena ya kuendelea na kazi kama mkaguzi mkuu. Laana ya chadema imemla ndezi sana yule. Toa yeyeeeeeeee

Sent using Jamii Forums mobile app
 
  • Thanks
Reactions: mmh
Walao kuna hata upinzani unasema chochote....

Haya majinga hayana utu kabisa!

Sasa unamtoa CAG sijui serikali kwenye mambo ya fedha utaidhibiti vipi?

Huyu mzee ana laana mbaya sana anakua mrefu kushuka chini....!

Well,Ndugai....sijui tumetokana nae wapi masikini..
Wanataka kumweka mtu wao ambaye hatagusa maslahi yao. Hakuna dhamira ya dhati ya kupambana na ufisadi!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom