Kambi ya Upinzani Bungeni kusoma bajeti Jumatatu, CCM waja na mkakati wao wa mchanga

Yaani niache kusikiliza tafiti za kutoka ikulu nikae nasikiliza porojo zenu!..Mwambie Kubenea hizo porojo aziweke kwenye MwanaHalisi, Mawio na Habari Leo tutaziona tuu
 
Upuuzi mtupu. Bajeti ya nchi keshasoma Dk mpango . Ninachojua jumatatu ni mhe rais anapokea ripoti ya pili saa tatu asubuhi. over
Bajeti ya majenereta kulipa leseni ya kutumia barabara?
Pambaufu kabisa.
 
Yaani niache kusikiliza tafiti za kutoka ikulu nikae nasikiliza porojo zenu!..Mwambie Kubenea hizo porojo aziweke kwenye MwanaHalisi, Mawio na Habari Leo tutaziona tuu
Ikulu inayonajisiwa kila iitwapo leo??
 
Upuuzi mtupu. Bajeti ya nchi keshasoma Dk mpango . Ninachojua jumatatu ni mhe rais anapokea ripoti ya pili saa tatu asubuhi. over
Kilichosomwa na Dk. Mpango ni "Bajeti Pendekezwa" Bunge ndilo hupitisha Bajeti, kwahiyo tunapaswa kuisikiliza kwa makini "Bajeti Pendekezwa" ya upande wa Upinzani ili kuona kama kuna mambo yanaweza kuiboresha hiyo ya Dk Mpango, ila ni iwapo tunajitambua!
 
Kilio changu ni elimu....naitetea nafsi yangu.....watoto wangu wamekosa mikopo ya elimu ya juu wako watatu.
END OF THE ROAD
 
Kama upinzani unajiamini una bajeti mbadala, nzuri na inayotekelezeka, Mwanahabari Huru wasiwasi wa nini? Upinzani una ushawishi mkubwa kwenye vyombo vya habari, hivyo hiyo bajeti itafuatiliwa tu, au!!!
kwanini na nyie mnafanya maigizo mnaogopa nini kufunikwa?
 
kwanini na nyie mnafanya maigizo mnaogopa nini kufunikwa?
Suala la maigizo ni hisia zako kuhalalisha woga wenu wa bajeti isiyo na mashiko kwa kuwa hamjiamini.

Unajua vigezo vya wazi vya mtu asiyejiamini, mojawapo ni kushutumu watu wengine, na mara nyingi kwa hisia tu. Kila baya analolifanya au kutokufanikiwa, atadai kuna mkono wa mtu. Wakati mwingine anasingizia uchawi.
 
Suala la maigizo ni hisia zako kuhalalisha woga wenu wa bajeti isiyo na mashiko kwa kuwa hamjiamini.

Unajua vigezo vya wazi vya mtu asiyejiamini, mojawapo ni kushutumu watu wengine, na mara nyingi kwa hisia tu. Kila baya analolifanya au kutokufanikiwa, atadai kuna mkono wa mtu. Wakati mwingine anasingizia uchawi.
Kama haina mashiko kwanini mnafanya maigizo jibu swali tulieni tuwafundishe kazi siyo maigizo kwenye mambo ya msingi
 
Naamini mtasikilizwa, ilimradi muache mbwebweni zisizo na msingi. Si Mara moja, Bali Mara kadhaa nimeona Serikali ya CCM ikitekeleza maoni ya upinzani yanayoonekana yanafaa na yanamanufaa kwa Taifa.

Hivyo acheni inferiority complex, simameni kiume muwasilishe bajeti yenu mbadala.
Mkuu Nemesis,upinzani mara nyingi huwa wanacheza muziki wa maCCM tena kwa tone ya maCCM. Uahauri wako ni wa maana sana kama ukitekelezwa. Wao wajikite kwenye issues zinazomgusa mwananchi wa kawaida na si makelele yasio na mashiko. Upinzani wakiacha "retaliations" za mapovu dhidi ya maCCM,wakaja na hoja za msingi,wananchi watawaelewa,na serikali ya maCCm pia itayafanyia kazi japokuwa huwa ni kwa mlango wa nyuma na kimyakimya ili upinzani usipate credits.
 
Kama haina mashiko kwanini mnafanya maigizo jibu swali tulieni tuwafundishe kazi siyo maigizo kwenye mambo ya msingi
Mimi si mwanachama wa chama chochote cha siasa kama unvyotaka iwe, nikunukuu (maandishi mekundu). Mimi ni Raia mwema ambaye huvutwa na kuunga mkono vitendo vyenye kuleta mafanikio. Na iko mifano mingi ya utekelezaji wa maneno kwa vitendo wa Serikali iliyoko madarakani - sina haja ya kuorodhesha.

Kwamba Serikali iliyoko madarakani inafanya maigizo, ni mtu au kikundi cha watu wazoefu wa maigizo ndio waweza kusema hivyo. Hao si nani ni viongozi wa vyama vya upinzani na wabunge wao, ambao leo wakisema hili kesho wanalikanusha, au kufanya vioja hadharani na sehemu zenye heshima kama bunge. Kwa mfano, kiongozi mwenye busara huchagua neno na lugha staha kumwambia kiongozi mwenzake kakosea. Lakini lugha kama "sijapata kuona uongozi wa hovyo kama huu" ni mwendawazimu tu anaweza kuyatamka maneno hayo.

Kama kuigiza siyo huko, basi tunatofautiana tafsiri ya neno maigizo.
 
Back
Top Bottom