Kambi mbili za upizani katika Bunge

Mwiba

JF-Expert Member
Oct 23, 2007
7,607
1,744
Huenda tukawa na kambi mbili za upizani katika Bunge moja.Hili limetokana na uovu wa Chadema wa kutotaka kushirikisha chama kingine katika kambi yao tofauti na CUF wakati ilipokuwa ikiongoza kambi ya upinzani.

Chadema imekuwa ikijificha na kujivalisha ngozi ya kondoo kumbe ni waovu na wabaya sana ,udini na ukabila wanauficha kiasi inakuwa vigumu kwa watu au wananchi wa kawaida kuing'amua hali waliyonayo Chadema.

Migongano kibao ndani ya Chadema imesababishwa na sababu ambazo zimewafanya wasimchague mtu kushiriki katika kambi ya upinzani bungeni.Huu ni ubaya walionao Chadema kwenye uchaguzi wanataka waachiwe wao ,sehemu wanayohitajika kuachia wanakuwa na mazonge kibao na wanakuwa wagumu ,kwa ufupi wanataka wafanyiwe wao tu.

Mbowe ni mmoja ya watu walioonesha hadharani kama Mzanzibar hawezi kujitawala na hata kufika kumsema maiti kwenye mikutano ya hadhara kama Rais wa Zanzibar marehemu sheikh Idrisa Abdull Wakili alifika darasa la saba tuu na akawa Rais wa Zanzibar hili lina maana kubwa na mpaka leo hajaomba radhi kwa Wazanzibar wala Ukoo wa Marehemu hilo tuliwache

Sasa basi kutokana na Chadema kukosa mbunge hata wa dawa kwa upande wa pili wa Jamhuri ya Muungano nikimaanisha Zanzibar ,CUF moja kwa moja watalazimika kuwa kambi ya pili ya upinzani ili kuiwakilisha Zanzibar .
 
Si mkawakilishe huko kwenye mkoa wenu?si mnalo lile sijui bunge sijui baraza!huku bwana ni pipoooos malizia.....naöna mnataka kujifanya eti bila nyie mambo hayaendi...cio lazima kila m2 apate cheo bwana ccm imewalemaza ndio maana mnapewa vyeo feki mnashangilia kumbe mmeliwa(maalim)
 
Huenda tukawa na kambi mbili za upizani katika Bunge moja.Hili limetokana na uovu wa Chadema wa kutotaka kushirikisha chama kingine katika kambi yao tofauti na CUF wakati ilipokuwa ikiongoza kambi ya upinzani.

Chadema imekuwa ikijificha na kujivalisha ngozi ya kondoo kumbe ni waovu na wabaya sana ,udini na ukabila wanauficha kiasi inakuwa vigumu kwa watu au wananchi wa kawaida kuing'amua hali waliyonayo Chadema.

Migongano kibao ndani ya Chadema imesababishwa na sababu ambazo zimewafanya wasimchague mtu kushiriki katika kambi ya upinzani bungeni.Huu ni ubaya walionao Chadema kwenye uchaguzi wanataka waachiwe wao ,sehemu wanayohitajika kuachia wanakuwa na mazonge kibao na wanakuwa wagumu ,kwa ufupi wanataka wafanyiwe wao tu.

Mbowe ni mmoja ya watu walioonesha hadharani kama Mzanzibar hawezi kujitawala na hata kufika kumsema maiti kwenye mikutano ya hadhara kama Rais wa Zanzibar marehemu sheikh Idrisa Abdull Wakili alifika darasa la saba tuu na akawa Rais wa Zanzibar hili lina maana kubwa na mpaka leo hajaomba radhi kwa Wazanzibar wala Ukoo wa Marehemu hilo tuliwache

Sasa basi kutokana na Chadema kukosa mbunge hata wa dawa kwa upande wa pili wa Jamhuri ya Muungano nikimaanisha Zanzibar ,CUF moja kwa moja watalazimika kuwa kambi ya pili ya upinzani ili kuiwakilisha Zanzibar .


Kabla hujaandaa thread inatakiwa ufanye tathmini ya unachotaka kutoa. sio unatuletea utumbo mjinga mkubwa wewe! CHADEMA na CUF nani alikataa kuungana na mwenzake? Acha kukurupuka, kasome magazeti ya leo ujue nini kilitokea. Sio wachangiaji wote ni wajinga kama wewe!!!
 
CUF wakaungane wa wavaa pedo wenzao....kwani lazima wawe wao kambiya upinzani???? hii mijitu ya DINi hii mipumbavi sana..ndo maana mliambiwa mnazaliana kama kuku
 
Kabla hujaandaa thread inatakiwa ufanye tathmini ya unachotaka kutoa. sio unatuletea utumbo mjinga mkubwa wewe! CHADEMA na CUF nani alikataa kuungana na mwenzake? Acha kukurupuka, kasome magazeti ya leo ujue nini kilitokea. Sio wachangiaji wote ni wajinga kama wewe!!!

KAMA SI BWANA ALIYEKUWA PAMOJA NASI ISRAELI NA ASEME SASA. (ZAB.124:1).
siamini nikionacho kwa Mkristo huyu....maneno yote hayo unayatoa sababu ya siasa?! au?! JE NI KUNDI LIPI UNALIWAKILISHA? YESU ASEMA NI HERI KUWA BARIDI AU MOTO...KULIKO KUWA VUGUVUGU...ATATAPIKWA MTU.....!
 
Kabla hujaandaa thread inatakiwa ufanye tathmini ya unachotaka kutoa. sio unatuletea utumbo mjinga mkubwa wewe! CHADEMA na CUF nani alikataa kuungana na mwenzake? Acha kukurupuka, kasome magazeti ya leo ujue nini kilitokea. Sio wachangiaji wote ni wajinga kama wewe!!!

yaani una uchungu na chadema kiasi hicho? mbona utapata presha na kutukana hivyo humu

unadhani woote wanafanana na wewe?

gazeti gani ulilolisoma na limeandika nini? na kwa nini usitumegee ulichokisoma kueleza kitu gani kilitokea, badala ya kutukana??
 
Mbona CUF ilisha wahi kuungwa mkono na CHADEMA katika kugombea kiti cha uraisi mwaka fulani, je CUF ina historia hiyo! Kama CCM ni waungwana si wawakaribishe CUF au "Dovutwa Party"!
 
mi naona bora CCM itawale tu manake hv vyama vingine vimejaa ukabila na udini tu
umeulizwa ni chama gani ungependa kitawale Tanzania au una dandia tu kaa kushoto....udini/ukabila unauona chadema tu? vipi CUF na hao bwana zako CCM, baadala ungalie ugumu wa maisha ya ndugu zako kulala kwenye matembe, elimu duni, mfumko wa bei...maisha ambayo kwa ufinyu wa akili yako unaona bora tundelee na hao Mafisadi.... wake up mumy
 
Upinzani watofautina bungeni Send to a friend Thursday, 11 November 2010 20:42 0diggsdigg

Boniface Meena na Habel Chidawali, Dodoma

VYAMA vya upinzani vimemeguka bungeni baada ya Chadema kuchukuanafasi zote za juu za uongozi wa Kambi ya Upinzani bungeni bila kuvihusisha vyama vingine.

Baada ya Chadema kutangaza jana kuwa imewateua Freeman Mbowe, Zitto Kabwe na Tundu Lissu kuwa viongozi wake wakuu bungeni, vyama vyama vya CUF, TLP na NCCR Mageuzi, viliamua kuunda kambi nyingine ya upinzani isiyorasmi.

Mkurugenzi wa Masuala ya Bunge wa Chadema, John Mrema aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa chama hicho kimemteua Mbowe kuwa Kiongozi wa Kambi ya Upinzani bungeni, Naibu wake ni Zitto na Tundu Lisu anakuwa Mnadhimu Mkuu.
Mbowe ni Mbunge mteule wa jimbo la Hai, Zitto Kigoma Kaskazini na Tundu Lissu, Singida Mashariki.


"Tuna asilimia 12.5 ya wabunge na hiyo inatupa nafasi ya kuunda kambi ya upinzani bungeni," alisema Mrema.

Hata hivyo, akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa kambi ya upinzani bungeni, Mrema alieleza kuwa amepata taarifa kuwa CUF kimeungana na NCCR Mageuzi na TLP kuunda kambi yao.

Mrema alisema CUF kimewaeleza kuwa kimeunda kambi yao kwa kushirikiana na NCCR-Mageuzi na TLP.

"Sijui wanaunda kambni gani, lakini Hamad Rashid ametueleza kuwa wao wameungana na NCCR na TLP kuunda kambi yao," alisema Mrema.

Kauli hiyo ya Mrema iliungwa mkono na aliyekuwa Kiongozi wa Upinzani bungeni, Hamad Rashid Mohamed aliyesema kuwa CUF imeamua kuunda kambi yao inayojulikana kwa jina la ‘Minority opposition' ambayo ina viongozi wake.

"Kama baadaye wenzetu wa Chadema watataka tushirikiane tutafanya hivyo, lakini hiyo ndiyo kambi yetu tuliyoiunda," alisema Hamad na kufahamisha kuwa yeye ndiye kiongozi wa kambi hiyo.

Alisema kambi hiyo inaongozwa na yeye (Hamad) kama mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti ni Khalifa Suleiman na Katibu Mkuu ni David Kafulila wa NCCR.

Kwa mujibu wa Hamad, CUF imeamua kuunda kambi yake kwa kuwa Chadema kimetangaza kuwa chama kikuu cha upinzani bungeni.

Kitendo cha kuunda kambi mbili za upinzania bungeni kinaonyesha kuwa bado kuna tatizo la ushirikiano miongozi mwa vyama hivyo, ambavyo vimekuwa vikivutana kwa muda mrefu kuhusu kuunganisha nguvu.

Mgororo huo umesabisha kutoshirikiana wakati wa uchaguzi, ambapo kila chama husimamisha mgombea wake katika majimbo ambayo chama kimojawapo kina nguvu zaidi.

Utengeno huo umesababisha vyama hivyo kupoteza ushindi dhidi ya CCM kwa kugawana kura, kama ilivyotokea Tarime mkoani Mara katika Uchaguzi Mkuu uliopita.

Katika jimbo hilo ambalo ni ngome ya Chadema, chama hicho kilimsimamisha Mwita Waitara na CUF walimsimamisha Charles Mwera aliyekuwa mbunge wa Chadema, lakini aliunguliwa wakati wa mchakato kuteua wagombea.

Hatua hiyo ilisababisha wagombea hao kugawana kura ambazo zingejumlishwa zingewezesha jimbo hilo kuwa mikononi mwa Chadema, lakini likaenda CCM.

Pia katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Mbeya Vijini mwaka mapema mwaka jana CUF ambayo haikuwa na nguvu Mbeya Vijijini ilimsimamisha mgombea na kuvishawishi vyama vingine kukiunga mkono.

Katika uchaguzi wa mwaka huu, Chadema nayo ilisimamisha wagombea katika majimbo yote ya mikoa ya Kusini mwa Tanzania ambako ni ngome ya CUF


source : mwananchi

au mwananchi nayo imenunuliwa, they have reported what happened, na kama ni hivyo kazi ipo!!!!!!!!!!
 
Upinzani watofautina bungeni Send to a friend Thursday, 11 November 2010 20:42 0diggsdigg

Boniface Meena na Habel Chidawali, Dodoma

VYAMA vya upinzani vimemeguka bungeni baada ya Chadema kuchukuanafasi zote za juu za uongozi wa Kambi ya Upinzani bungeni bila kuvihusisha vyama vingine.

Baada ya Chadema kutangaza jana kuwa imewateua Freeman Mbowe, Zitto Kabwe na Tundu Lissu kuwa viongozi wake wakuu bungeni, vyama vyama vya CUF, TLP na NCCR Mageuzi, viliamua kuunda kambi nyingine ya upinzani isiyorasmi.

Mkurugenzi wa Masuala ya Bunge wa Chadema, John Mrema aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa chama hicho kimemteua Mbowe kuwa Kiongozi wa Kambi ya Upinzani bungeni, Naibu wake ni Zitto na Tundu Lisu anakuwa Mnadhimu Mkuu.
Mbowe ni Mbunge mteule wa jimbo la Hai, Zitto Kigoma Kaskazini na Tundu Lissu, Singida Mashariki.


"Tuna asilimia 12.5 ya wabunge na hiyo inatupa nafasi ya kuunda kambi ya upinzani bungeni," alisema Mrema.

Hata hivyo, akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa kambi ya upinzani bungeni, Mrema alieleza kuwa amepata taarifa kuwa CUF kimeungana na NCCR Mageuzi na TLP kuunda kambi yao.

Mrema alisema CUF kimewaeleza kuwa kimeunda kambi yao kwa kushirikiana na NCCR-Mageuzi na TLP.

"Sijui wanaunda kambni gani, lakini Hamad Rashid ametueleza kuwa wao wameungana na NCCR na TLP kuunda kambi yao," alisema Mrema.

Kauli hiyo ya Mrema iliungwa mkono na aliyekuwa Kiongozi wa Upinzani bungeni, Hamad Rashid Mohamed aliyesema kuwa CUF imeamua kuunda kambi yao inayojulikana kwa jina la ‘Minority opposition’ ambayo ina viongozi wake.

"Kama baadaye wenzetu wa Chadema watataka tushirikiane tutafanya hivyo, lakini hiyo ndiyo kambi yetu tuliyoiunda," alisema Hamad na kufahamisha kuwa yeye ndiye kiongozi wa kambi hiyo.

Alisema kambi hiyo inaongozwa na yeye (Hamad) kama mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti ni Khalifa Suleiman na Katibu Mkuu ni David Kafulila wa NCCR.

Kwa mujibu wa Hamad, CUF imeamua kuunda kambi yake kwa kuwa Chadema kimetangaza kuwa chama kikuu cha upinzani bungeni.

Kitendo cha kuunda kambi mbili za upinzania bungeni kinaonyesha kuwa bado kuna tatizo la ushirikiano miongozi mwa vyama hivyo, ambavyo vimekuwa vikivutana kwa muda mrefu kuhusu kuunganisha nguvu.

Mgororo huo umesabisha kutoshirikiana wakati wa uchaguzi, ambapo kila chama husimamisha mgombea wake katika majimbo ambayo chama kimojawapo kina nguvu zaidi.

Utengeno huo umesababisha vyama hivyo kupoteza ushindi dhidi ya CCM kwa kugawana kura, kama ilivyotokea Tarime mkoani Mara katika Uchaguzi Mkuu uliopita.

Katika jimbo hilo ambalo ni ngome ya Chadema, chama hicho kilimsimamisha Mwita Waitara na CUF walimsimamisha Charles Mwera aliyekuwa mbunge wa Chadema, lakini aliunguliwa wakati wa mchakato kuteua wagombea.

Hatua hiyo ilisababisha wagombea hao kugawana kura ambazo zingejumlishwa zingewezesha jimbo hilo kuwa mikononi mwa Chadema, lakini likaenda CCM.

Pia katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Mbeya Vijini mwaka mapema mwaka jana CUF ambayo haikuwa na nguvu Mbeya Vijijini ilimsimamisha mgombea na kuvishawishi vyama vingine kukiunga mkono.

Katika uchaguzi wa mwaka huu, Chadema nayo ilisimamisha wagombea katika majimbo yote ya mikoa ya Kusini mwa Tanzania ambako ni ngome ya CUF


source : mwananchi

au mwananchi nayo imenunuliwa, they have reported what happened, na kama ni hivyo kazi ipo!!!!!!!!!!
 
CUF ni chama kikuu cha upinzani Zanzibar ambacho kwa sasa kimo ndani ya serikali ya CCM.
 
Nijuavyo mimi ni kuwa CUF imeungana na ccm ndo maana pale visiwani Maalim ni Makamu wa rais au huyu anaongelea cuf nyingine!
 
Toka lini Wazanzibari wakaaminika? Sijui kwanini Tunaukumbatia Utanzania ni Bora Tuwe na Tanganyika Yetu Salama

Walipokuwa Wanagabunge Wengu Bunge Lilipita Walijichagua kwenye Madaraka yote Makuu; Yeah Sasa Wamemkumbatia John Cheyo ambaye Walimfukuza Bunge lilipita... Sasa Wao ni CCM B

Wanyamaze Mbona wao hawakuweka Wabunge Maeneo Mengi ina Maana ni Udini au just stratergy na Vyama Vingi havina Pesa Kama CCM; Nadhani wanajua lakini wanaleta Chuki... Wajaribu kutatua CHUKI KATI YA PEMBA - CUF na UNGUJA - CCM
 
Kafu kichekesho kule imeungana na CCM huku inataka kuungana na Chadema kwa nini wasiombe kuungana na CCM?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom