Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 233
Kwa kuwa sasa hivi kamati za ulinzi na usalama zinaonekana kujiingiza katika masuala ya kipolisi, yaani kuwaelekeza polisi nani akamatwe – wale wanaohatarisha ulinzi na usalama, basi ingefaa kamati hizo sasa ziwe zinaelekeza kukamatwa kwa mafisadi, kwani ufisadi ni jinai inayoweza kuhatarisha usalama na amani na utulivu wa nchi.
Haya ninayosema siyatungi kichwani mwangu kwani yameandikwa katika Sheria ya Kupambana na Rushwa (PCCB Act No. 11 of 2007). Ninanukuu hapa sentensi ya kwanza ya Utangulizi (preamble) ya Sheria hiyo iliyopitishwa na Bunge letu:
"WHEREAS corruption is an obstacle to principles of democracy, good governance and human rights and poses a threat to peace, tranquillity and security in the society;…..
Hivyo basi ufisadi unahatarisha usalama wan chi, hivyo hizi kamati za ulinzi na usalama zisaidie kutoa amri kwa polisi kuwasaka na kuwakama mafisadi wote katika maeneo yao.
Wasijikite tu katika kukamata watu, hasa viongozi wa upinzani wanaotoa hoja mbadala majukwaani kwa kuwaita eti wanatishia usalama, ufisadi (na hivyo mafisadi) wameandikwa kabisa in black and white katika sheriua kwamba ni wavunjifu wakubwa wa amani na usalama wan chi.
Wanabodi nawasilisha…
Haya ninayosema siyatungi kichwani mwangu kwani yameandikwa katika Sheria ya Kupambana na Rushwa (PCCB Act No. 11 of 2007). Ninanukuu hapa sentensi ya kwanza ya Utangulizi (preamble) ya Sheria hiyo iliyopitishwa na Bunge letu:
"WHEREAS corruption is an obstacle to principles of democracy, good governance and human rights and poses a threat to peace, tranquillity and security in the society;…..
Hivyo basi ufisadi unahatarisha usalama wan chi, hivyo hizi kamati za ulinzi na usalama zisaidie kutoa amri kwa polisi kuwasaka na kuwakama mafisadi wote katika maeneo yao.
Wasijikite tu katika kukamata watu, hasa viongozi wa upinzani wanaotoa hoja mbadala majukwaani kwa kuwaita eti wanatishia usalama, ufisadi (na hivyo mafisadi) wameandikwa kabisa in black and white katika sheriua kwamba ni wavunjifu wakubwa wa amani na usalama wan chi.
Wanabodi nawasilisha…